Hivi Tanzania tumerogwa au ni kitu gani tulichokosea?

Wolle Melkas Fernando

JF-Expert Member
May 4, 2016
218
297
Salaam nyingi sana waungwana!

Tunaadhimisha miaka 60 ya Uhuru wa kujitawala na kujifanyia maamuzi ya mambo yetu wenyewe.

Miaka 60 sio mchezo na haina kisingizio cha kusema sisi tuko nyuma kimaendeleo kwasababu bado wachanga katika masuala ya kiuchumi, kisiasa, kijamii na kiteknolojia (We don't have an excuse).

Naangalia tenda za serikalini katika masuala mbalimbali hususan ya Miradi ya Ujenzi zinapewa Kampuni za Kigeni, ninachojiuliza kwahiyo miaka 60 yote sisi hatuna mainjinia wa kufanya hiyo kazi tukawalipa na pesa tubaki nayo hapa nyumbani?

Ndani ya Miaka 60 ya Uhuru Mainjinia wetu wamekuwa wakihitimu tu katika vyuo vikuu mbalimbali ndani na nje ya nchi lakini tenda kubwa kubwa za Constructions wanapewa wageni halafu wenyeji ambao ni mainjinia wetu wanaajiriwa na wageni na serikali inajitapa kuwa mradi huu umetengeneza ajira.

Mara nyingi kama sio zote Wenyeji hupewa tenda za kuziba viraka kwenye barabara zetu au kuweka makaravati, hiki ni kichekesho kinachoumiza.

Hivi kuna haja gani ya Taifa kusomesha wataalam mfano wa masuala ya madini, gesi, mafuta?

Mwalimu Nyerere aliwahi kuzuia uchimbwaji wa madini akisisitiza mpaka wazawa wasome waje wachimbe wenyewe, kilichopo sasa sote tunajua, wazawa wasomi na wataalamu wa Jiolojia wamebaki kuwa vibarua wa makampuni makubwa ya madini kutoka nje ambao hufanya utafiti kupata madini nchini mwetu na sisi tunaambulia kulamba asilimia chini ya kumi na tunajitapa tuna wataalam tunasonga mbele.

Serikali imekuwa ikipiga chapuo ya vijana kujiajiri na kusema vijana waende VETA ili wakimaliza wajiajiri, wapo wengi kwenye vikundi wengine useremala, wengine ushonaji n.k.

Lakini cha kushangaza serikali inaruhusu makampuni yaliyowekeza hapa nchini kuagiza nje Furnitures kwaajili ya ofisi zao hapa nchini huku yakiacha kuwaungisha vijana wetu, Makampuni yanaagiza uniforms za wafanyakazi wao kutoka nje, yanashindwa kununua hapa nchini kwa vikundi vizuri kabisa vya ushonaji, nina ushahidi wa haya.

Hivi huku ni kulogwa au tatizo ni nini waungwana, kuna maana gani ya kuadhimisha miaka 60 ya Uhuru kama tunaruhusu Uhuru wa Kazi na Kipato kwa Vijana wetu kupokwa na Wageni kwa kile tunaita kuwapa Uhuru Wawekezaji?
 
Hao wanafunzi wa VETA hawana ubora wa kukidhi kutoa huduma nzuri kwa hayo makampuni. na mambo ya kulazimishana yalishapitwa na wakati
 
Halafu masuala ya kutuuliza kwamba aliyeturoga nn wakati unajua kabisa toka tupate uhuru mpaka sasa anayeongoza inchi ni nani au ww hauishi hapa Tanzania unatukejeli!!!
Pia nitatizo mtoa Mada anazungumza kanakwamba ngeni sijui mabegi ya kura na mapanga kwenye chaguzi unategemea miujiza
 
Salaam nyingi sana waungwana!

Tunaadhimisha miaka 60 ya Uhuru wa kujitawala na kujifanyia maamuzi ya mambo yetu wenyewe.

Miaka 60 sio mchezo na haina kisingizio cha kusema sisi tuko nyuma kimaendeleo kwasababu bado wachanga katika masuala ya kiuchumi, kisiasa, kijamii na kiteknolojia (We don't have an excuse)

Naangalia tenda za serikalini katika masuala mbalimbali hususan ya Miradi ya Ujenzi zinapewa Kampuni za Kigeni, ninachojiuliza kwahiyo miaka 60 yote sisi hatuna mainjinia wa kufanya hiyo kazi tukawalipa na pesa tubaki nayo hapa nyumbani?

Ndani ya Miaka 60 ya Uhuru Mainjinia wetu wamekuwa wakihitimu tu katika vyuo vikuu mbalimbali ndani na nje ya nchi lakini tenda kubwa kubwa za Constructions wanapewa wageni halafu wenyeji ambao ni mainjinia wetu wanaajiriwa na wageni na serikali inajitapa kuwa mradi huu umetengeneza ajira.

Mara nyingi kama sio zote Wenyeji hupewa tenda za kuziba viraka kwenye barabara zetu au kuweka makaravati, hiki ni kichekesho kinachoumiza.

Hivi kuna haja gani ya Taifa kusomesha wataalam mfano wa masuala ya madini, gesi, mafuta?

Mwalimu Nyerere aliwahi kuzuia uchimbwaji wa madini akisisitiza mpaka wazawa wasome waje wachimbe wenyewe, kilichopo sasa sote tunajua, wazawa wasomi na wataalamu wa Jiolojia wamebaki kuwa vibarua wa makampuni makubwa ya madini kutoka nje ambao hufanya utafiti kupata madini nchini mwetu na sisi tunaambulia kulamba asilimia chini ya kumi na tunajitapa tuna wataalam tunasonga mbele.

Serikali imekuwa ikipiga chapuo ya vijana kujiajiri na kusema vijana waende VETA ili wakimaliza wajiajiri, wapo wengi kwenye vikundi wengine useremala, wengine ushonaji n.k.

Lakini cha kushangaza serikali inaruhusu makampuni yaliyowekeza hapa nchini kuagiza nje Furnitures kwaajili ya ofisi zao hapa nchini huku yakiacha kuwaungisha vijana wetu, Makampuni yanaagiza uniforms za wafanyakazi wao kutoka nje, yanashindwa kununua hapa nchini kwa vikundi vizuri kabisa vya ushonaji, nina ushahidi wa haya.

Hivi huku ni kulogwa au tatizo ni nini waungwana, kuna maana gani ya kuadhimisha miaka 60 ya Uhuru kama tunaruhusu Uhuru wa Kazi na Kipato kwa Vijana wetu kupokwa na Wageni kwa kile tunaita kuwapa Uhuru Wawekezaji?
Musukuma kesha iva kwenye uzamivu.
 
Sio tuu majengo kakaa
Yaan miaka 60 ya uhuru tumeshindwa na hata Kagame ambae sasa anatengeneza kiwanda chake cha uzalishaji Magari.

Sisi mpaka leo tuna shughulikia matundu ya Choo Jamani...

Mi huwa na Jiuliza sisi wa Tanzania tunaweza nini kusimama pekeyetu kwa chochote bila ya Mchina wala Mturuki...

Sent from my SM-A125F using JamiiForums mobile app
 
Tumeajiri wazawa watujengee ghorofa pale ghoba Kwa awadhi wametuangusha,wakaangusha na ghorofa yenyewe,acha tuendelee kuamini wageni
 
Sasa kama ma-engineer wenyewe ndo kama ivi unafikiri ukimpa daraja kama la KIJAZI,unategemea nini kitatokea kama si bendera kushushwa nusu mlingoti
JamiiForums-131224730.jpg
 
Salaam nyingi sana waungwana!

Tunaadhimisha miaka 60 ya Uhuru wa kujitawala na kujifanyia maamuzi ya mambo yetu wenyewe.

Miaka 60 sio mchezo na haina kisingizio cha kusema sisi tuko nyuma kimaendeleo kwasababu bado wachanga katika masuala ya kiuchumi, kisiasa, kijamii na kiteknolojia (We don't have an excuse).

Naangalia tenda za serikalini katika masuala mbalimbali hususan ya Miradi ya Ujenzi zinapewa Kampuni za Kigeni, ninachojiuliza kwahiyo miaka 60 yote sisi hatuna mainjinia wa kufanya hiyo kazi tukawalipa na pesa tubaki nayo hapa nyumbani?

Ndani ya Miaka 60 ya Uhuru Mainjinia wetu wamekuwa wakihitimu tu katika vyuo vikuu mbalimbali ndani na nje ya nchi lakini tenda kubwa kubwa za Constructions wanapewa wageni halafu wenyeji ambao ni mainjinia wetu wanaajiriwa na wageni na serikali inajitapa kuwa mradi huu

Salaam nyingi sana waungwana!

Tunaadhimisha miaka 60 ya Uhuru wa kujitawala na kujifanyia maamuzi ya mambo yetu wenyewe.

Miaka 60 sio mchezo na haina kisingizio cha kusema sisi tuko nyuma kimaendeleo kwasababu bado wachanga katika masuala ya kiuchumi, kisiasa, kijamii na kiteknolojia (We don't have an excuse).

Naangalia tenda za serikalini katika masuala mbalimbali hususan ya Miradi ya Ujenzi zinapewa Kampuni za Kigeni, ninachojiuliza kwahiyo miaka 60 yote sisi hatuna mainjinia wa kufanya hiyo kazi tukawalipa na pesa tubaki nayo hapa nyumbani?

Ndani ya Miaka 60 ya Uhuru Mainjinia wetu wamekuwa wakihitimu tu katika vyuo vikuu mbalimbali ndani na nje ya nchi lakini tenda kubwa kubwa za Constructions wanapewa wageni halafu wenyeji ambao ni mainjinia wetu wanaajiriwa na wageni na serikali inajitapa kuwa mradi huu umetengeneza ajira.

Mara nyingi kama sio zote Wenyeji hupewa tenda za kuziba viraka kwenye barabara zetu au kuweka makaravati, hiki ni kichekesho kinachoumiza.

Hivi kuna haja gani ya Taifa kusomesha wataalam mfano wa masuala ya madini, gesi, mafuta?

Mwalimu Nyerere aliwahi kuzuia uchimbwaji wa madini akisisitiza mpaka wazawa wasome waje wachimbe wenyewe, kilichopo sasa sote tunajua, wazawa wasomi na wataalamu wa Jiolojia wamebaki kuwa vibarua wa makampuni makubwa ya madini kutoka nje ambao hufanya utafiti kupata madini nchini mwetu na sisi tunaambulia kulamba asilimia chini ya kumi na tunajitapa tuna wataalam tunasonga mbele.

Serikali imekuwa ikipiga chapuo ya vijana kujiajiri na kusema vijana waende VETA ili wakimaliza wajiajiri, wapo wengi kwenye vikundi wengine useremala, wengine ushonaji n.k.

Lakini cha kushangaza serikali inaruhusu makampuni yaliyowekeza hapa nchini kuagiza nje Furnitures kwaajili ya ofisi zao hapa nchini huku yakiacha kuwaungisha vijana wetu, Makampuni yanaagiza uniforms za wafanyakazi wao kutoka nje, yanashindwa kununua hapa nchini kwa vikundi vizuri kabisa vya ushonaji, nina ushahidi wa haya.

Hivi huku ni kulogwa au tatizo ni nini waungwana, kuna maana gani ya kuadhimisha miaka 60 ya Uhuru kama tunaruhusu Uhuru wa Kazi na Kipato kwa Vijana wetu kupokwa na Wageni kwa kile tunaita kuwapa Uhuru Wawekezaji?
Fuatilia barabara za lami zilizojengwa na kampuni za kibongo ndo utapata jibu. Pia barabara za vumbi kalavati zimevimba kama matuta ya viazi. Zaidi tembelea shule, vituo vya afya na zahanati zilizojengwa na hao mainjinia utapata jibu.
 
Halafu masuala ya kutuuliza kwamba aliyeturoga nn wakati unajua kabisa toka tupate uhuru mpaka sasa anayeongoza inchi ni nani au ww hauishi hapa Tanzania unatukejeli!!!
Tena na picha anaona za bibi wa kiarabu zilivyo tandazwa na ndio uhuru wenyewe..
 
Mkuu shida ya kampuni zetu na watalaam wetu ni mtaji tu.
Watu wetu wana uwezo mkubwa sana ila shida ni mitaji.
Wenzetu wanasaidiwa na serikali zao katika suala mitaji, nchi nyingi zinafanya ujasusi wa kiuchumi ili raia wake waweze kufanya biashara nchi nyingine.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom