Hivi Tanzania kuna Wizara ya Kilimo?

Blackafrica

Senior Member
Jun 26, 2021
141
401
Nimejikuta najiuliza hilo swali, swali ambalo naamini wananchi wengi wafanyabiashara na wakulima wamekuwa wakijiuliza. Baada ya kumaliza chuo kwa msaada fulani niliopata, niliamua kujihusisha na shughuli za kilimo kununua na kuuza mazao lakini vile vile kulima.

Haya mambo ya kilimo, ukisimuliwa ni rahisi kudhani yana faida, lakini ukweli ni kwamba kilimo cha Bongo ni kilimo cha kijanja janja, kuanzia kwa mkulima mpaka mfanyabiashara. Haya makundi mawili kila kundi lina wakati wake wa kulia lakini wakati mwingine makundi yote hulia kwa pamoja.

Najua unashangaa lakini ndio ukweli wa mambo ulivyo wakati mkulima analima kwa shida shambani, mfanyabiashara anakuja kulangua mazao kwa bei ya chini hapo ni kilio cha mkulima. Wakati mwingine kukiwa na uhaba mfano kwa sasa alizeti ipo juu hapo mkulima anapeta, lakini maajabu ni wakati mwingine mkulima kuuza mazao yake kwa bei ya chini na mfanyabiashara kukosa soko la kuuza mazao yake mfano kwa sasa mpunga na mahindi yako bei chini soko la kuuza hakuna, hapo makundi yote mawili yanateseka kuanzia mkulima mpaka mfanyabiashara.

Swali je Wizara ya kilimo ipo? Na kama ipo kazi yake nini? Kweli inashindwa kutafuta masoko ya wakulima? Kweli hii wizara inashinda kutengeneza mazingira ambayo yatamsaidia mkulima kupata faida lakini pia mfanyabiashara kuuza kwa soko la uhakika lenye faida.

Katika utafiti wangu nimegundua asilimia kubwa ya wakulima Tanzania hutegemea soko la ndani, hili soko la ndani limeshikwa na watu wachache ambao ndio wanafaidika nalo na mkulima hufaidi kidogo sana, leo hii ukijitutumua wewe mkulima au mfanyabiashara ukatafuta soko la nje ya nchi utakwama tu na itafika mahari utajiuliza hivi hii nchi ya Tanzania ina Wizara ya kilimo kweli?

Kwa taarifa tu Wakulima wengi wa Tanzania tunashindwa kuuza mazao yetu nje ya nchi kwa sababu hatuna mikakati au mbinu ya kushindania bei ya kimataifa (international price) leo hii ukitaka kuuza zao lolote la kilimo nje ya nchi kitu cha kwanza cha kuzingatia lazima upange bei ambayo inaendana na bei ya kimataifa, yaani kama mahindi katika soko la dunia yanauzwa sh 100 kwa kg basi itakulazimu na wewe kuuza kwa kg mahindi yako kwa sh 100
Hili ndio tatizo lako ambalo linahusiana na bei ya kimataifa tatizo la pili ni uwingi quanitity mara zote ukitaka kuuza mazao nje ya nchi lazima uwe na msuri wa kutosha wa kuwa na mzigo wa kutosha, yaani kama ulizoea soko la ndani kuuza tone mia tano au elfu moja ya mchele usijidanganye kulitaka soko la kimataifa huko wanaanziaga tone ya chini sana ni tone elfu kumi kuendeleaaaaa!

Sasa najiuliza sana Wizara ya kilimo ipo? Na kama ipo kazi yake ni nini? Maana mapungufu makubwa yanayotokea kwenye sekta ya kilimo yanasababishwa na hii wizara kutoshiriki ipasavyo katika kuinua kilimo, ambapo kilimo pekee tu kama hii serikali yetu ingekuwa serious kingetosha kujenga uchumi wa nchi hii, kwa mwananchi mmoja mmoja mpaka Taifa nzima.

Tunakwama kwa sababu tuna kilimo cha hovyo mikakati ya hovyo sera za kilimo za hovyo, lakini vile vile tumeruhusu watu wachache wanufaike na mfumo wa hovyo wa kilimo uliopo sasa na ndio maana unaona mara mkulima analia mara mfanyabiashara analia wakati mwingine wanalia wote je wizara haiyaoni haya? Je wizara haiyajui haya? Lakini je wizara haina uwezo wa kuyatatua haya? Ukijiuliza yote hayo itafika sehemu utajiuliza wizara ya kilimo kazi yake ni nini? Tutafakari kwanza haya afu nitaludi tena.

Kila jambo lina mwisho wake mwambie na mwenzako.
 
Sidhani kama shida ni wizara ya Kilimo.Shida ni vipaumbeke vya Taifa letu havijulikani na kama vinajulikana basi sio harisi kama inavotakiwa.

Sasa kila kiongozi anakuja na kutekeleza yale anayo yaona yeye yanafaaa. Mwisho wa siku hakuna linalo endelea miaka nenda miaka rudi.

Mwisho wa siku Taifa zima linakosa dira ya maendeleo. Kila mtu anajenga anacho kipenda. Hvyo badotunasafari ndefu sana, mpaka pale tutakapo pata viongozi wenye akili na maarifa kichwani, ambao wako tayari kulitumikia hili taifa.
 
Sidhani kama shida ni wizara ya Kilimo.Shida ni vipaumbeke vya Taifa letu havijulikani na kama vinajulikana basi sio harisi kama inavotakiwa.

Sasa kila kiongozi anakuja na kutekeleza yale anayo yaona yeye yanafaaa. Mwisho wa siku hakuna linalo endelea miaka nenda miaka rudi.

Mwisho wa siku Taifa zima linakosa dira ya maendeleo. Kila mtu anajenga anacho kipenda. Hvyo badotunasafari ndefu sana, mpaka pale tutakapo pata viongozi wenye akili na maarifa kichwani, ambao wako tayari kulitumikia hili taifa.
Well nadhani tunakubaliana hii wizara ya kilimo ina watendaji mbali mbali je watendaji kazi zao ni kukaa tu ofisini? Majukumu yao ni yepi? Je wanatimiza majukumu yao? Kwa sababu ishu ya soko ishu ya kilimo bora chenye tija hilo ni suala dogo ambalo liko ndani ya wizara kutengeneza miundombinu ya kufika huko, mkulima analindwa na nani? Right nakubaliana nawe hatuna ajenda muhimu au vipaumbele muhimu, warsha na makongamano wanayokaa kila wakati sina hakika kama kuna tija yoyote
 
Nimejikuta najiuliza hilo swali, swali ambalo naamini wananchi wengi wafanyabiashara na wakulima wamekuwa wakijiuliza. Baada ya kumaliza chuo kwa msaada fulani niliopata, niliamua kujihusisha na shughuli za kilimo kununua na kuuza mazao lakini vile vile kulima.

Haya mambo ya kilimo, ukisimuliwa ni rahisi kudhani yana faida, lakini ukweli ni kwamba kilimo cha Bongo ni kilimo cha kijanja janja, kuanzia kwa mkulima mpaka mfanyabiashara. Haya makundi mawili kila kundi lina wakati wake wa kulia lakini wakati mwingine makundi yote hulia kwa pamoja.

Najua unashangaa lakini ndio ukweli wa mambo ulivyo wakati mkulima analima kwa shida shambani, mfanyabiashara anakuja kulangua mazao kwa bei ya chini hapo ni kilio cha mkulima. Wakati mwingine kukiwa na uhaba mfano kwa sasa alizeti ipo juu hapo mkulima anapeta, lakini maajabu ni wakati mwingine mkulima kuuza mazao yake kwa bei ya chini na mfanyabiashara kukosa soko la kuuza mazao yake mfano kwa sasa mpunga na mahindi yako bei chini soko la kuuza hakuna, hapo makundi yote mawili yanateseka kuanzia mkulima mpaka mfanyabiashara.

Swali je Wizara ya kilimo ipo? Na kama ipo kazi yake nini? Kweli inashindwa kutafuta masoko ya wakulima? Kweli hii wizara inashinda kutengeneza mazingira ambayo yatamsaidia mkulima kupata faida lakini pia mfanyabiashara kuuza kwa soko la uhakika lenye faida.
Katika utafiti wangu nimegundua asilimia kubwa ya wakulima Tanzania hutegemea soko la ndani, hili soko la ndani limeshikwa na watu wachache ambao ndio wanafaidika nalo na mkulima hufaidi kidogo sana, leo hii ukijitutumua wewe mkulima au mfanyabiashara ukatafuta soko la nje ya nchi utakwama tu na itafika mahari utajiuliza hivi hii nchi ya Tanzania ina Wizara ya kilimo kweli?

Kwa taarifa tu Wakulima wengi wa Tanzania tunashindwa kuuza mazao yetu nje ya nchi kwa sababu hatuna mikakati au mbinu ya kushindania bei ya kimataifa (international price) leo hii ukitaka kuuza zao lolote la kilimo nje ya nchi kitu cha kwanza cha kuzingatia lazima upange bei ambayo inaendana na bei ya kimataifa, yaani kama mahindi katika soko la dunia yanauzwa sh 100 kwa kg basi itakulazimu na wewe kuuza kwa kg mahindi yako kwa sh 100
Hili ndio tatizo lako ambalo linahusiana na bei ya kimataifa tatizo la pili ni uwingi quanitity mara zote ukitaka kuuza mazao nje ya nchi lazima uwe na msuri wa kutosha wa kuwa na mzigo wa kutosha, yaani kama ulizoea soko la ndani kuuza tone mia tano au elfu moja ya mchele usijidanganye kulitaka soko la kimataifa huko wanaanziaga tone ya chini sana ni tone elfu kumi kuendeleaaaaa!

Sasa najiuliza sana Wizara ya kilimo ipo? Na kama ipo kazi yake ni nini? Maana mapungufu makubwa yanayotokea kwenye sekta ya kilimo yanasababishwa na hii wizara kutoshiriki ipasavyo katika kuinua kilimo, ambapo kilimo pekee tu kama hii serikali yetu ingekuwa serious kingetosha kujenga uchumi wa nchi hii, kwa mwananchi mmoja mmoja mpaka Taifa nzima.
Tunakwama kwa sababu tuna kilimo cha hovyo mikakati ya hovyo sera za kilimo za hovyo, lakini vile vile tumeruhusu watu wachache wanufaike na mfumo wa hovyo wa kilimo uliopo sasa na ndio maana unaona mara mkulima analia mara mfanyabiashara analia wakati mwingine wanalia wote je wizara haiyaoni haya? Je wizara haiyajui haya? Lakini je wizara haina uwezo wa kuyatatua haya? Ukijiuliza yote hayo itafika sehemu utajiuliza wizara ya kilimo kazi yake ni nini? Tutafakari kwanza haya afu nitaludi tena.

Kila jambo lina mwisho wake mwambie na

Sidhani kama shida ni wizara ya Kilimo.Shida ni vipaumbeke vya Taifa letu havijulikani na kama vinajulikana basi sio harisi kama inavotakiwa.

Sasa kila kiongozi anakuja na kutekeleza yale anayo yaona yeye yanafaaa. Mwisho wa siku hakuna linalo endelea miaka nenda miaka rudi.

Mwisho wa siku Taifa zima linakosa dira ya maendeleo. Kila mtu anajenga anacho kipenda. Hvyo badotunasafari ndefu sana, mpaka pale tutakapo pata viongozi wenye akili na maarifa kichwani, ambao wako tayari kulitumikia hili taifa.
Kuna ufafanuzi wa kina, juu ya hayo masuala pitieni haya maandiko.
1: UTANGULIZI.
Tanzania katika miaka ya hivi karibuni imepata maendeleo mazuri katika nyanja za kisiasa kiuchumi na katika ustawi wa jamii. Ingawa bado nchi inakumbana na changamoto kubwa za kimaendeleo, kama vile rushwa ongezeko kubwa la watu magonjwa na kukosa usawa wa mgawanyo wa mapato nchini. Wakati huo huo kuna fursa mpya zinazaliwa.

Tanzania inasifika kwa kua na rasilimali nyingi, lakini richa ya hayo yote nchi imekosa muunganiko mzuri kati ya rasilimali zilizopo na kiwango cha maendeleo tulichofikia. Ni kivipi? Tuangazie mchanganuo huu kidogo.

=> Rasilimali; huhusisha vitu vyote vinavyopatikana katika mazingira yanayotuzunguka ambavyo vinaweza kutusaidia kukidhi mahitaji yetu. Tanzania imebarikiwa kuwa na rasilimali mbalimbali na za kujitosheleza. Mfano; Tanzania ina...;

Ardhi yenye rutuba inayofaa kwa kilomo takribani hekari milioni 44, ila asilimia 33% tu ya hilo eneo ndio hulimwa. Pia tumezungukwa na vyanzo vya maji, bahari mito na mabonde, na maziwa makuu yasiyopungua matano(5).

Inamadini adimu duniani yanayopatikana kwa wingi kama vile Almasi, dhahabu, Tanzanite, ulanga, nikeli, uraniumu, lithium nk. Pia kuna gasi asilia inayokadiliwa kua na ujazo wa futi cubic trilioni 25-30, Kwa mujibu wa PFC Energy.

Vivutio vya utalii vinapatikana kila pembe na katikati ya nchi, hifadhi za taifa zipatazo 22, ambazo kwa ujumla wake zinachukua asilimia 15% ya eneo la nchi ambalo ni sawa na nchi ya Croatia.

Rasilimali watu/nguvu kazi ya taifa inakadiliwa Tanzania inaidadi kubwa ya watu wapatao milioni 61, ambao wanaweza kutumika katika sekta mbalimbali za uzalishaji.

Ina jiografia nzuri iliyokaa kimkakati na kifaida zaidi, kuna bahari inayotumika kusafirisha na kuingizia mizigo wakati huo huo kuna nchi jirani zisizopungua nane(8), kati ya hizo kuna nchi sita(6) zisizokuwa na bahari hivyo kwa namna moja au nyingine zitaitegemea Tanzania katika usafirishaji.

=> Uchumi ni nini; ni namna ambavyo jamii ya nchi husika inaweza kuzichunga/kuzitunza na kuzitenga rasilimali zao adimu kimkakati zaidi ili ziwaletee maendeleo. Kuna uchumi mbalimbali kulingana na rasilimali zilizopo mfano; uchumi wa bluu(blue economy) unatokana na shughuli za majini, uchumi wa viwanda, uchumi wa kilimo , madini, utalii biashara, huduma mbalimbali nk.

=> Maendeleo ni nini; ni mchakato mzima unaepelekea kuimarika ama kufanikiwa kwa uchumi na maisha bora kwa raia(ustawi wa jamii) katika nchi husika. Kwa mfano; kuimarika kwa miundombinu ya mawasiliano na usafirishaji, viwanda, biashara na huduma za kijamii.

Maendeleo endelevu ni maendeleo yalio bora zaidi kwakua yanahakikisha upatikanaji wa mahitaji ya kizazi cha sasa pasipo kuathiri upatikanaji wa hayo mahitaji kwa kizazi cha baadae.

Kutokana na kukua maradufu kwa idadi ya watu inatakiwa hayo maendeleo yaendane na sayansi na teknologia iliyopo kinyume na hapo itakua ni uvunaji wa rasilimali uliokithili na utaharibu sana rasilimali kwa faida kidogo.

Kwa kuangalia mchanganuo huo tunapata mwangaza na kujitasmini sisi kama taifa, Je? tunastahili kuwa katika kiwango hiki cha maendeleo ( cha uchumi wa kati kiwango cha chini), tukilinganisha na utajili wa rasilimali tulizonazo. Hebu tufanye tasmini ndogo isiyohitaji hata milinganyo ya kihesabu.

Je, Tunamiundombinu ya uchukuzi na mawasiliano iliyojitosheleza na imara, kama vile reli balabala madalaja bandari na viwanja vya ndege pia kasi na mtawanjiko wa mikongo ya njia za mawasiliano. Itakayo rahisisha biashara na shughuli nyingine za kijamii na kiuchumi.

Je, Huduma ya elimu nchini imeimarika, yaani elimu bora kwa wote, kuna vitendeakazi vyakutosha, viti vyakutosha, madalasa na je shule zinajitosheleza nchini?.

Je, huduma za afya nchini zimeimalika, vifaatiba na madawa yanapatikana , matabibu vitanda na hospitali zinatosha kanda mbalimbali nchini.

Je, Huduma za maji safi na salama pamoja na umeme vinapatikana kwa uhakika(masaa 24).

Je, Ulinzi na usalama wa raia na mali zao unaridhisha hapa nchini, vitengo vya polisi na zimamoto utendaji wake ukoje wanavitendea kazi vya kisasa.

Bila shaka maendeleo tuliyonayo tokea uhuru (miaka 61) ukilinganisha na rasilimali tulizonazo haviendani (ni mbingu na ardhi). Fikilia nchi kama Korea, Israel au hata Rwanda wangekua na hizi rasilimali, Tanzania tungekua kwenye orodha ya nchi zinazopokea msaada kutoka kwao.

Pia maendeleo tuliyonayo hayaendani na kasi ya mabadiliko ya sayansi na teknolojia, serikali haina muamko. raia ndio tunawahamasisha kila siku kama vile, kuboresha masuala ya miamala ya kidijitali.

Sasa kama ni hivyo tatizo ni nini/tunakwama wapi.?

2: Sababu Zinazopeleke Kukwama au Kusuasua Kwa Maendeleo Tanzania.

=> Kukosa mfumo madhubuti wa uongozi:

Katika sehemu ya ndani kabisa/kiini cha nchi(sistimu) ilishidwa kufanikisha kuundwa kwa mfumo imara usio teteleka na vuguvugu za kisiasa (vyama mbalimbali). Ilitakiwa nchi kama nchi iwe na misimamo yake halafu hayo matakwa ya ilani za vyama yawe kama mapendekeza tu na sio nchi kutekeleza kwa kegezo kua chama fulani kinaongoza.

Kuna baadhi ya vitengo hasa kitengo cha intelijensia vimekosa weledi yawezekana kuna mamluki waliopenyezwa kwa maslahi ya watu shilika au kampuni binafsi, kama sio sasa wanashidwaje kutoa taarifa mamlaka husika na kwa wakati sahihi nakushinikiza hatua zichukuliwe kwa wahisiwa. Matukio ya ufisadi mkubwa, rushwa, madawa ya kulevya kwanini hatua za makusudi hazichukuliwi kukomesha haya. Laiti kama pesa zilizopotea kwa ufisadi zingetumika kama ilivyopangwa leo hii tusingekua tunahangaika kukatana tozo kwaajili ya ujenzi wa vituo vya afya, tungekua hatua nyingine kabisa. Wananchi tunajitahidi kuchagua viongozi bora ili tupate utawala bora, lakini unazongwazongwa na kupoteza mvuto.

Tuangalie mfano huu unaoendana na asilimia 80% ya watanzania wanaotegemea kilimo (uti wa mgogo wa taifa).

Fikilia kwamba;
•Serikali ==> shamba,
•Wananchi ==> wakulima,
•Viongozi ==> mazao yaliyopo shambani bado ambayo yametokana na wakulima kuchagua mbegu bora kwa kutarajia kupata mazao mengi yenye ubora.

Wakulima wanashauriwa kua makini katika kuandaa shamba na mbegu, mara baada ya kupanda na mimea kumea, magugu huwa yanatokea kusikojulikana, lakini huwa yanakua na mbegu zake ambazo inawezekana zilifika shambani kwa kuletwa na wanyama, upepo, zilizochangamana na mbegu za mazao zilizopandwa na mkulima(seed mimicry), ama zilikuepo tu shambani miaka na miaka(Striga weed seeds).

Kiasili magugu huwa yanakua na nguvu kushinda mazao, yanastawi pasipo hata matunzo yoyote, yakiachwa bila kuondolewa kwa wakati hasa kipindi ambacho mazao yanakaribia kuchanua utakosa kabisa mavuno, huku magugu yakiwa yamesheheni mazao yake.

Ni hivyo hivyo hata kwa wadudu waharibifu, (ukicheka na nyani utavuna mabua).

=> Rushwa/Siasa rushwa (Malpolitics):
Nimatumizi ya nguvu ya dola yanayofanywa na baadhi ya watumishi wa serikali au/na mitandao ya watu wao wa karibu kwa kujipatia au kufanikisha jambo lao binafsi kwa njia isiyo halali. Hapa siajabu ukakuta kiongozi anashilikiana na wafanyabiashara,makampuni makubwa nchini na nnje ya nchi tokea kipindi cha kampeni mpaka anapata madaraka, tutarajie nini hapa? Watakua wananufaika hao wafanyabiashara na makampuni kwa kutekeleza miladi isiyokua na tija kwa taifa bali wao tu.

Kwahiyo rushwa ni adui wa haki na maendeleo katika nyanja zote uchumi,kijamii na kisiasa.

=> Kufifia kwa hari ya uzalendo na uwajibikaji kwa viongozi na raia kwa ujumla (patriotism):
Asilimia kubwa ya viongozi hapa nchini huwa wanakua wazalendo mwanzoni, wakishakaa madalakani mitazamo na misimamo inabadilika hii ni kwasababu wanajitenga na jamii, makazi yao na harakati zao zinafanyika mazingira ya hadhi fulani kila siku, wanakua kwenye obwe la faraja(comfort zone). Hapa siajabu ukakuta wabunge wanajadili mambo muhimu katika hari ya mzaha mzaha na kupitisha vitu ambavyo kwa wananchi ni mkuki, pasipo kupata maoni kwa wananchi hawatastuka kuwa tunawabebesha mizigo mizito wananchi, (aliyeshiba hamkumbuki mwenye njaa).

Tungekuwa wazalendo haya mambo yangekuwa yamerekebishika, viongozi wangetembelea wilaya majimbo na vijiji mbalimbali kijionea hari halisi na kutatua changamoto mbalimbali, na pia wananchi wamekua ni watu wakuiraumu na kuisusia serikali.

=> Kukosa dira ya maendeleo yenye kupewa nguvu na kipaumbele:
Dira ya maendeleo haipewi kipaumbele/uzito wake unaostahili katika utekelezaji wake. Yaani dira ya maendeleo inachukuliwa kama ahadi za kwenye kampeni, itekelezwe isitekelezwe sawa tu.

Tanzania hatuna vipaumbele maalumu katika kujenga uchumi, na ndio maana kila serikali inayoundwa inakuja na sera zake mpya zitakazo tegemea ilani ya chama husika. Kila awamu malengo yanabadilikabadilika kabla hili halijakamilika linaletwa lingine mara kilimo kwanza mara tanzania ya viwanda. Sasa kama taifa kwa mfumo huu ni ngumu kufanikiwa, tunakosa msingi na uchumi wa nchi unakosa muunganiko mzuri. Kuna msemo unasema "Badilisha mbinu/njia za kuyafikia malengo, usibadilishe malengo).

3: Ni Nini Kifanyike Ili Kuinua Uchumi Wa Tanzania Uendane na Rasilimali Zilizopo:

=> Kuimarisha mfumo mzima wa uongozi na utendajiwake wa kazi:

Maboresho zaidi yanahitajika katika sheria na katiba ya nchi, kuwe na kiwango kikubwa cha uwazi haki na utawala wa sheria. Pia kufanyike maboresho makubwa katika vitengo vya ulinzi na usalama hasa kitengo cha intelijensia, hivi vitengo utendaji wake wa kazi unatia shaka. Vichunguzwe je? Kuna watumishi wanaofaa wenye weledi wajuu na wanaoweza kuendana na hii kasi ya sayansi na teknolojia.

Hayo maboresho yataongeza uwajibikaji na uzalendo kwa viongozi na raia na kupunguza vitendo vya kiharifu kama vile rushwa, ufisadi na ubadhirifu wa mali za uma kwa wananchi na viongozi kwa ujumla.

=> Kupambana na rushwa na ufisadi kwa nguvu zote:
Hadi kufikia kiwango ambacho hakitaathiri mwenendo wa uchumi wa nchi. Hili litafanikiwa endapo tutakua na uongozi imara, wenye sheria itakayo muwajibisha yeyote pasipo kujali hadhi yake katika jamii. Isiwe kama hili, makosa yanafanywa na raia wa matawi yote ila wanao onekana magelezani ni masikini tu.

Ufisadi umechangi pakubwa mno kwenye kudidimia kimaendeleo nchini, pesa ambayo ilipotea kwenye skendo za ufisadi hapo nyuma ingetatua changamoto za huduma za afya elimu na maji mijini na vijijini kipindi kile, leo hii tungekua tunafanya hatua nyingine za maendeleo za juu zaidi. Inatakiwa haya mambo mabaya yasijirudie tena ili tuweza kusonga mbele, inatakiwa hili swala la ufisadi na rushwa lipewe nguvu ya kisheri ili mali ya umma iwe ya moto kwa fisadi yeyote yaana asiitamani kabisa ili tusonge mbele.

=> Kuandaa dira ya maendeleo ambayo itapewa nguvu/uzito na kipaumbele kwa mujibu wa sheria:
Dira ijumuishe mambo muhimu yenye maslahi mapana kwa taifa ambayo yatakua kama dira au maono, ambapo kabla maamuzi hayajachukuliwa juu ya utekelezaji wa jambo lolote inatakiwa turudi(kurejelea ) katika dira na kuona dira inasemaje? Unakua ndio msingi kupitia huo mambo mengine yanafanyika(Organizing principle). Inatakiwa pia hiyo dira iwe inaweza kunyumbulika ili kuendana na mabadiliko ya rasilimali sayansi na teknolojia,(Architectural thinking).

Dira ambayo itaangazia katika sekta mbalimbali huku kipaumbele kikielekezwa katika tafiti za kisayansi na teknolojia mahususi katika sekta husika kama vile;

sekta ya sayansi na teknolojia: ili tuweze kua na uchumi wenye nguvu na ushindani ni muhimu kujiimalisha katika hii sekta, tuweze kuendana na kasi ya mabadiliko ya teknolojia kwa kujikita katika tafiti za tiba vyombo vya moto na tehama(wenzetu huko duniani wako kwenye mapindizi ya nne ya viwanda (fourth industrial revolution)).

Je tunaweza kupambana na vita ya kiuchumi, mashambulio yakimtandao, uharifu wa kibiolojia? Tumejipanga vipi na hizi changamoto?

Tuige mfano hata kwa majilani zetu Rwanda kwa hatua wanazopiga wakati huohuo sisi tunaangalia tu nasioni jitihada zozote zikichukuliwa.

Kama ilivyo Israel pale mashariki ya kati inawezekana Rwanda ikawa hivyo huku kwetu kusini mwa jagwa la Sahara hapo baadae, tuchunge sana.

Sekta ya kilimo: bajeti iongezeke maradufu katika sekta ya kilimo ili kuchochea tafiti za mbegu bora kuendana na kanda husika, kuongeza wataalamu wa kilimo wa ngazi ya juu kufanya kilimo kiwe cha kisasa zaidi, harafu viongozi waache siasa kwenye kilimo, kilimo ni sayansi kama sayansi nyingine! Wengi wetu hatujui hilo kwasababu asilimia kubwa ya wakulima wetu wanafanya kilimo cha kienyeni kwa matumizi ya nyumbani. Kwenye kilimo cha kisasa na chenye tija haitakiwi kuharibu kanuni, pembejeo iwe mbegu mbolea au viwatilifu zinatakiwa kutumika kwa kiwango sahihi, mahali husika na kwa wakati sahihi kinyume na hapo kilimo kimekushinda. Ni sawa tu sayansi ya umeme ili taa iwake inatakiwa kuwe na chaji hasi (-) na chanya (+) katika mfatano maalumu ukienda tofauti na hapo taa haiwaki.

Sasa je? Kama kweli kilimo ni uti wa mgongo wa taifa na asilimia 80% ya raia wanategemea kilimo, inakuwaje tena pembejeo hazifiki kwa wakati, wakati huohuo bei ni ghari sana. Sasa kilimo ni uti wa mgongo au unyayo? Maana selikali mnabebwa sana na kilimo ila hambebeki. Asilimia 65% ya mizigo ilivyo safirishwa nje kibiashara ni inatokana na kilimo, pia kilimo kinachangia pato kubwa zaidi kuliko sekta nyingine yoyote ile asilimia 28% ya pato la taifa.

Tanzania haistahili kwenda kujifunza kilimo kwenye nnchi yenye jangwa na ndogo vile(Israel).

Kwahiyo kilimo nako kuwe na muelekeo ili tuweze kujitosheleza kwa chakula na mazao yanayobakia yasafirishwe sokoni pia ni moja ya malighafi viwandani kwa ukuaji wa uchumi.

Sekta ya viwanda:
Viwanda vya ngazi zote dira iangazie huku pia. Idadi ya viwanda nchini hairidhishi vinatakiwa viwanda vingi hasa vinavyotegemea malighafi za kilimo na madini. Tena viwanda vikishamili vitasaidia kupunguza tatizo la ajira nchini kwa kiwango kikubwa.

Nisawa kunauwezekano tusiweze kuendesha viwanda vyenye teknolojia kubwa lakini je?tutashidwa kupunguza uagizaji wa mitumba na nguo dalaja la tatu kwa ubora, na kuanzisha viwanda vyandani vya nguo bora kabisa mbona pamba tunalima ya kutosha.! Mafuta yakula, sukali vipuri na magurudumu ya gari je?

Changamoto zingine kama upungufu wa ajira kwa vijana utakao kuja kushuhudiwa ndani ya muongo mmoja na nusu baadae ni kujitakia tu kwa serikali, hivyo dira maalumu inahitajika sasa.

Madini yanayohitajika kwenye ulimwengu wa sasa (mapindizi ya nne ya viwanda) wa magari na treni za umeme, uundwe mpango maalumu wa kutafuta wawekezaji ikiwezekana zitengenezwe bidhaa ziliyokamilika hapahapa nchini. Mfano Lithium hadi kua betiri (batteries) za magari.

Ukiangalia rasilimali za madini ya Lithium, chuma, makaa ya mawe na nasikia kuna Helium ya kutosha, kwa malighafi hizi naona zimeendana na Elon Musk kabisa, tunaweza tukamshawishi aje awekeza tawi la Tesla(terafactory) na utafiti wa anga za juu hapa Tanzania (Space X branch in Tanzania).

=> Ushirikishwaji wa raia katika kutunza na kuendeleza rasilimali za taifa:

Raia wanakua wanafuatilia kwa umakini kabisa rasilimali, miradi inayoendelea mikataba yake ikoje, pamoja na mapato na matumizi yanaenda sawa sawa.? Hii itakuwa kama tu vile raia tunavyoshilikishwa kwenye ulinzi na usalama , utalii na katika utunzaji wa mazingira. Ila hii yasafari hii itakua rahisi kutokana na kukua kwa sayansi na teknolojia hasa katika mawasiliano, tutatumia mitandao ya kijamii kwa mujibu wa sheria serikali inaweza ikaanda jukwaa maalumu pengine hata katika mtandao wa Jamiiforum, watu maalumu au wote wataruhusiwa kuperuzi takwimu mbalimbani na kuhoji au kutoa michango yao.

Hii itaongeza uwajibikaji, uwazi na kupunguza vitendo viovu kama vile ufisadi ubdhilifu rushwa na utoroshwaji wa mali za taifa.

4: HITIMISHO.
Licha ya kuwa na maendeleo ya wastani, Tanzania tumekua na amani mshikamano na umoja tangu uhuru. Ukiachilia mbali jitihada kubwa tulizozichukua kupigania uhuru wetu na wamajirani zetu,Kumtia adabu Iddy Amin Dada na majanga yakiasili yaliyojitokeza huku tukiwa bado taifa changa, hatuna budi kujipongeza na kuzishukuru serikali na viongozi wote wa Jamhuri Ya Muungani wa Tanzania.

#Kazi Iendelee...!
Na andiko hili pia 👇🏿
Utangulizi
Dira kwa maana fupi ni muelekeo. Dira ya Maendeleo ya Tanzania (Tanzania Development Vision (TDV) 2025 ilianzishwa mwaka 1994 na kuzinduliwa rasmi mwaka 1999 ambapo utekelezaji wake ulianza mwaka 2000 lengo kuu likiwa kuongoza harakati za maendeleo ya uchumi na jamii zitakazoiwezesha Tanzania kufikia uchumi wa kati na kuondokana na umaskini uliokithiri ifikapo mwaka 2025. 'www.tanzania.go.tz' (tovuti kuu ya serikali)

Melengo makuu matano yalioainishwa katika Dira ya Maendeleo 2025 ni pamoja na kuboresha hali ya maisha ya kila Mtanzania, kuwepo kwa mazingira ya amani usalama na umoja,kujenga utawala bora,kujenga jamii iliyoelimika na kujenga uchumi imara unaokabiliana na ushindani. (Nukuu kutoka Dira ya Maendeleo ya Taifa 2025).

Katika andiko hili, nitaangazia malengo makuu matano kama yalivyoainishwa katika Dira ya Maendeleo 2025. Andiko langu litaangazia pia utekelezaji wa malengo haya na uhalisia wa maisha ya Mtanzania.

Katika uhalisia, Maendeleo ya Nchi yetu kwa asilimia kubwa yamekua yakitegemea Ilani ya chama tawala pamoja vipaumbele vya Rais aliye madarakani. Mfano halisi ni ununuzi wa ndege na ujenzi wa madaraja ambao uliingiza nchi katika madeni makubwa na umaskini. Ni wazi kwamba Dira ya Maendeleo ni kijarida tu ambacho kimetengenezwa kutimiza wajibu lakini hakina nafasi kubwa katika utekelezaji wa shughuli za maendeleo.

Serikali imeunda mipango mingi kwa ajili ya utekelezaji wa maendeleo kama vile mpango wa maendeleo wa miaka mitanpo (Five Year Development Plan), MKUKUTA, Mpango wa Big Results Now (Matokeo Makubwa Sasa), Mpango wa maboresho ya utumishi wa Umma,pamoja na Maleongo ya Maendeleo ya Millenia chini ya nchi za Umoja wa Mataifa.

Katika mipango tajwa, yote ina malengo yanayolandana kwa maana ya kutokomeza umaskini kwa kuboresha huduma za afya, elimu, nishati, kilimo, maji, biashara, mahusiano ya kimataifa, ajira, kuboresha utumishi wa umma, kuweka usawa wa kijinsia pamoja na mengine mengi.

Hebu tuangazie miaka kumi nyuma tulinganishe na utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya Taifa 2025 na hali halisi ya Watanzania mpaka leo hii.

Hali ya maisha ya Mtanzania imezidi kuwa duni pamoja na kwamba nchi yetu ipo katika uchumi wa kati wa chini, Mtanzania wa kawaida anashindwa kumudu gharama ndogo za mlo wa siku ilhali tunatangaziwa uchumi wetu umekua kwa asilimia 7% ( NBS 2019/2020).

Katika kujenga utawala bora, hali imezidi kuwa tete, ni wazi kwamba utawala wa sheria umekua jambo gumu katika nchi yetu hali inayopelekea kutokuwajibika kwa pamoja na ubadhirifu wa mali za umma (Rejea ripoti ya CAG 2020).

Katika Dira ya Mendeleo 2025, serikali imeonyesha nia ya kujenga jamii iliyoelimika na inayojifunza kila siku kulingana na mazingira na nyakati tulizopo, tukirudi kwenye uhalisia, kiwango cha ubora wa elimu zetu hakikidhi viwango vitakavyowawezesha wasomi wetu kuingia katika ushindani ndani na nje ya Tanzania, shule zetu nyingi hazina waalimu wa kutosha wala vifaa vya kufundishia, matamko ya kisiasa kwa upande mwingine yamekua yakiathiri mifumo ya elimu.

Kwa mfano mnamo mwezi Desemba 2020, Rais JPM aliagiza somo la historia ya Tanzania lianze kufundishwa katika shue za msingi mpaka sekondari, Wizara ya elimu iliandaa machapisho kwa ajili ya somo husika lakini baada ya Rais Samia kuingia madarakani somo hilo lilisitishwa rasmi.

Kwa upande mwingine serikali ilichangia kupotosha jamii badala ya kuelimisha. Nitoe mfano mdogo wa janga la Covid 19. Serikali ilisimama kidete kuuaminisha umma kwamba janga hili ni vita ya mabeberu dhidi yetu badala ya kutumia wataalamu wa afya kutoa elimu kuhusu namna bora ya kujikinga ili kuepuka maambukizi. Serikali ilienda mbali zaidi na kuhamasisha tiba mbadala na njia za asili ambazo zilitumika katika vituo vya afya pia.

Kauli ya serikali pamoja na viongozi wakuu wa nchi imeleta mkanganyiko pamoja na hisia tofauti juu ya janga hili na kusababisha watu kuishi pasipo kuchukua tahadhari hata baada ya serikali kubadili msimamo na kuamua kufuata njia za kitaalamu. Ukijaribu kuongea na watanzania kumi, tisa kati yao wanaogopa chanjo na kuamini kwamba mabeberu wanataka kutumaliza.
View attachment 1862120View attachment 1862121
(picha kutoka mtandaoni)

Katika uboreshaji wa utumishi wa umma, vilio vimekua vingi, utekelezaji wa dhima hii umesahaulika kwa miaka zaidi ya mitano iliyopita, vilio vingi vya wafanyakazi kuhusu nyongeza za mishahara pamoja na kupanda madaraja, makato makubwa, na mishahara duni ambayo haikidhi maisha ya kila siku.

Mambo ya muhimu yaliyotajwa katika utekelezaji wa malengo ya milenia ni pamoja na kukuza mahusiano ya kimataifa, kutokomeza umaskini wa kipato na njaa. Kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita, Tanzania imepuuza kwa kiasi kikubwa sana mahusiano ya kimataifa kutokana na misimamo ya kiongozi aliyekua madarakani. Vipato vya wananchi vimeshuka kutokana na tozo kubwa katika bidhaa na huduma, mfumuko wa bei umeathiri pembejeo za kilimo na bidhaa mbalimbali, uonevu kwa wafanyabiashara,ubambikaji wa kesi na kodi uliosababisha biashara nyingi kufungwa. Tunao mfano halisi wa sasa katika tozo ya miamala ambayo imeleta taharuki kubwa kwa wananchi masikini ambao hata kula yao ni ya tabu.

Mapendekezo
• Serikali ianzishe taasisi maalumu kwaajili ya kuandaa na kusimamia Dira ya Maendeleo ya Taifa. Chombo hicho kiwe na kazi ya kuandaa, kusimamia pamoja na kuishauri serikali iliyopo madarakani bila kujali chama.Taasisi hii ihakikishe sera sera na mipango ya taasisi mbalimbali za serikali pamoja na wizara zina uelekeo mmoja na zinashirikiana ka ukaribu. Kwa mfano suala la kuzalisha wahitimu wenye weledi ni lazima liendane na uboreshaji mfumo wa elimu, kwa hiyo ni lazima wizara ya kazi na wizara ya elimu zishirikiane kubaini mapungufu yanayoonekana kwa wahitimu wanaoajiriwa ili waweze kubaini njia bora ya kuboresha.

Taasisi hii ipewe mamlaka ya kusimamia serikali kama ilivyo bunge na mahakama na kwamba ilani ya chama cha kiongozi aliyeko madarakani ilenge kutafuta au kuonyesha njia sahihi za kuipeleka nchi kule ambako dira inaonyesha, hii itasaidia kutekeleza miradi iliyoachwa au iliyoanzishwa na kiongozi aliemaliza muda wake, mfano wakati Rais JPM naingia madarakani alisitisha ujenzi wa bandari ya Bagamoyo kwa madai kwamba mikataba ilikua mibovu na iliyojaa unyonyaji, siku chache baada ya Rais Samia kuingia madarakani mapitio ya ujenzi wa bandari yameanza, hii ni kwa sababu hakuna mfumo wa kusimamia viapaumbele vya maendeleo ya Taifa badala yake kila kiongozi anajiamulia kile anachopenda.

• Ipatikane katiba imara ambayo itasaidia kudhibiti na kusimamia viongozi walioko madarakani na hata baada ya kustaafu kama ilivyo kwa nchi nyingine kama Marekani na Afrika ya Kusini. Hii itahakikisha viongozi wote wanafanya kazi kwa kuheshimu haki za binadamu na sheria na taratibu zilizopo bila kuathiri malengo ya Taifa kwa ujumla. Katiba imara pia itasaidia kuweka uwajibikaji na usawa kati ya watumishi/viongozi, kuondoa ubadhirifu na matumizi mabaya ya madaraka.

• Serikali ijikite zaidi katika kuvumbua vyanzo vipya vya mapato badala ya kujikita katika kuongeza kodi katika huduma mbalimbali za kijamii ili kupunguza mzigo mkubwa wa kodi kwa wananchi na badala yake wananchi wapate unafuu wa maisha. Mfano sekta ya utalii na madini zinaweza kuwa vyanzo vizuri vya mapato kama tukiweka usimamizi mzuri na mifumo ya kuaminika ili kuepusha mianya ya ubadhirifu. Pia serikali ijikite katika kuboresha mfumo wa elimu ili kuruhusu vijana wengi kujiajiri katika nyanja mbalimbali badala ya kutegemea ajira kutoka serikalini.

• Bajeti za maendeleo zilizoidhinishwa na bunge zisitumike kinyume na lengo ili tuweze kutekeleza mipango iliyopangwa katika mwaka wa fedha wa serikali. Huko nyuma tulishuhudia pesa zikipelekwa katika matumizi ambayo hayakuidhinishwa na bunge hali iliyochangia kukwamishwa kwa miradi mingi ya maendeleo iliyoidhinishwa na bunge. Bajeti inayoidhinishwa pia iende sambamba na Dira ya Maendeleo ya Taifa.

• Serikali iunde mfumo shirikishi utakaosaidia wananchi kushiriki katika kuonyesha vipaumbele vya maendeleo pamoja na utekelezaji. Hii itasaidia wananchi kuwa wasimamizi wa moja kwa moja wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika maeneo yao.

• Serikali iwatumie wataalamu wa masuala ya uchumi walioko nchini badala ya kutumia wanasiasa pekee katika kuandaa bajeti na matumizi ya serikali, pia serikali ijenge utamaduni wa kuwatumia wataalamu waliobobea katika fani mbalimbali nchini katika kuandaa na kusimamia sera mbali mbali kwaajili ya kukuza uchumi na kuleta maendeleo ya Taifa pamoja na kuheshimu mawazo na maelekezo ya wataalamu katika sekta mbalimbali hata pale yanapotokea majanga yanayohitaji ufumbuzi wa kitaalamu. Kwa kufanya hivi, tutapunguza au kudhibiti matamko ya kisiasa katika mambo nyeti yanayohitaji ufumbuzi wa kitaalamu kama vile Afya, Elimu na Uchumi.

Hitimisho
Natoa wito kwa viongozi/wenye mamlaka, na watunga sera wa nchi, maamuzi yoyote wanayofanya yanaathiri au kufaidisha jamii nzima, wao ni sehemu ya jamii na hivyo wataathirika au kufaidika na maamuzi hayo kwa namna moja au nyingine. Ni vyema kufanya uchambuzi yakinifu kabla ya kufanya maamuzi ili kuepuka athari zozote zitakazoisababishwa na maamuzi yao ikiwa ni pamoja na kurudisha nyuma maendeleo ya Taifa.

Asanteni Sana​
 
Well nadhani tunakubaliana hii wizara ya kilimo ina watendaji mbali mbali je watendaji kazi zao ni kukaa tu ofisini? Majukumu yao ni yepi? Je wanatimiza majukumu yao? Kwa sababu ishu ya soko ishu ya kilimo bora chenye tija hilo ni suala dogo ambalo liko ndani ya wizara kutengeneza miundombinu ya kufika huko, mkulima analindwa na nani? Right nakubaliana nawe hatuna ajenda muhimu au vipaumbele muhimu, warsha na makongamano wanayokaa kila wakati sina hakika kama kuna tija yoyote
Watendaji wapo kutekeleza sera. Sera lazima ziwe na dira ya pamoja na endelevu. So hata waje wazungu hapa wapewe wizara hii. Bado serikali kama inasera mbovu bado impact haita onekana miaka nenda rudi.

Sera zinaungwa na chama husika kinacho shika dora. So hapa tunazungumzia kufeli kwa CCM kwa miaka zaidi ya 50 ya uhuru imeshindwa kuleta ukombozi wa kiuchumi wa mkulima mpaka leo hiii. Na kwa mindset zilizopo bado sana serikali hii kumkomboa mkulima bado sana.
 
SERA zipo kwenye makablasha yao huko Dom, tena wanavyojua kudaka ushuru hao wasione gari la mazao!
 
Watendaji wapo kutekeleza sera. Sera lazima ziwe na dira ya pamoja na endelevu. So hata waje wazungu hapa wapewe wizara hii. Bado serikali kama inasera mbovu bado impact haita onekana miaka nenda rudi.

Sera zinaungwa na chama husika kinacho shika dora. So hapa tunazungumzia kufeli kwa CCM kwa miaka zaidi ya 50 ya uhuru imeshindwa kuleta ukombozi wa kiuchumi wa mkulima mpaka leo hiii. Na kwa mindset zilizopo bado sana serikali hii kumkomboa mkulima bado sana.
Nakubaliana nawe eneo moja muhimu serikali imeshindwa kuleta mageuzi ya kilimo, upande wa pili serikali hii hii kuna maeneo kwenye hii hii sekta ya kilimo wana sera nzuri sana ambazo zipo tu kwenye maandishi lakini utekelezaji ni sifuri, hapa ndio naanza kupata akili na ninatamani ajenda ya kuwa na katiba mpya iwe ni ajenda ya wananchi na siyo wanasiasa, sisi wananchi tukiamua kwa dhati tunahitaji katiba mpya ambayo italeta ushindani sawa wa kuwania mamlaka, naamini ambao watapata nafasi ya kushika mamlaka watakuwa serious na kazi zao, tofauti na sasa washika mamlaka hawapo serious hata kidogo maana wanajiamini hata wakifanya vibaya wataendelea kushirikilia mamlaka
 
Umejazia nyama mambo mengi sana mwisho kabisa lazima tukubali serikari imeshindwa kuleta mageuzi ya kilimo
Ndio mkuu...pia kuna mapendekezo ya nini kifanyike kuboresha na kuimarisha sekta tofauti tofauti ikiwemo na kilimo.
 
Nakubaliana nawe eneo moja muhimu serikali imeshindwa kuleta mageuzi ya kilimo, upande wa pili serikali hii hii kuna maeneo kwenye hii hii sekta ya kilimo wana sera nzuri sana ambazo zipo tu kwenye maandishi lakini utekelezaji ni sifuri, hapa ndio naanza kupata akili na ninatamani ajenda ya kuwa na katiba mpya iwe ni ajenda ya wananchi na siyo wanasiasa, sisi wananchi tukiamua kwa dhati tunahitaji katiba mpya ambayo italeta ushindani sawa wa kuwania mamlaka, naamini ambao watapata nafasi ya kushika mamlaka watakuwa serious na kazi zao, tofauti na sasa washika mamlaka hawapo serious hata kidogo maana wanajiamini hata wakifanya vibaya wataendelea kushirikilia mamlaka
Katiba yenyewe iliyopo watanzania tunaifahamu? Isije ikawa tunaidai mpya huku iliyopo hatujawahi isoma hata mstari mmoja
 
Hovyo kabisa hawa watu
Ukikuta wanavyo ongea utasema mambo si ndiyo haya watu tunamashamba unajiuliza nilime nini, ukiwaza pesa yakudunduliza nipeleke shamba, je! Huko nitatoka kweli au ndiyo kutoka mikono kichwani, kuna yule naibu waziri hua namtizama tu!
 
Katiba yenyewe iliyopo watanzania tunaifahamu? Isije ikawa tunaidai mpya huku iliyopo hatujawahi isoma hata mstari mmoja
Hizi ni hoja nyepesi sana mkuu, nchi ilipofikia inahitaji katiba ambayo itatusaidia kutuletea maendeleo watanzania. Katiba iliyopo kwa sasa haina msaada kwa taifa bali inawabeba watawala kututawala wanavyotaka wao, ndio maana umri wa nchi na maendeleo yaliopo ni vitu viwili tofauti
 
Hizi ni hoja nyepesi sana mkuu, nchi ilipofikia inahitaji katiba ambayo itatusaidia kutuletea maendeleo watanzania. Katiba iliyopo kwa sasa haina msaada kwa taifa bali inawabeba watawala kututawala wanavyotaka wao, ndio maana umri wa nchi na maendeleo yaliopo ni vitu viwili tofauti
Ujua inaweza kuwa hoja nyepesi, lakini hao hao wanaosema ndiyo wanayoitekereza ndiyo hao hao watasema iwe hivi, inatakiwa hii iliyopo watu tuelimishwe kisha tuweke sasa inayotusaidia, unakumbuka ile rasimu ya Mzee nani vile......Iko wapi!
 
Nakubaliana nawe eneo moja muhimu serikali imeshindwa kuleta mageuzi ya kilimo, upande wa pili serikali hii hii kuna maeneo kwenye hii hii sekta ya kilimo wana sera nzuri sana ambazo zipo tu kwenye maandishi lakini utekelezaji ni sifuri, hapa ndio naanza kupata akili na ninatamani ajenda ya kuwa na katiba mpya iwe ni ajenda ya wananchi na siyo wanasiasa, sisi wananchi tukiamua kwa dhati tunahitaji katiba mpya ambayo italeta ushindani sawa wa kuwania mamlaka, naamini ambao watapata nafasi ya kushika mamlaka watakuwa serious na kazi zao, tofauti na sasa washika mamlaka hawapo serious hata kidogo maana wanajiamini hata wakifanya vibaya wataendelea kushirikilia mamlaka
Absolute.

Ifike pahara watanzania(Hasa vijana) sijui tusiwe na chama kabisa yaani. Yaani hatufungamani na upande wowote ule, tunaangalia sera pekeee za mgombea na chama chake ndo tunapiga kura.Hii itafanya baadhi ya wachumia tumbo wasipate nafasi kushika madaraka.


Mtu anakua Rais hajawai andika hata kitabu, sera na msimamo wake juu ya mambo mbali mbali havijulikani. Anaishia kusema tu ety Tutatekeleza irani yetu ya chama seriously....?

Nilitamani hata 2020 tungekua hata na presidential debate. Wagombea wa nafasi ya urais wawekwe mtu kati. Waandishi wahabari wawaulize maswali ili wawapime mtazamo na uelewa wao juu ya mambo mbali mbali kabla ya kuwapiga kura. Ni lazma watanzania wajue rais tunae taka kumchagua ana msimamo gani juu ya Muungano, Vp kuhusu katiba mpya, Madawa ya kulevya, Democrasia, Rushwaa, Ushoga, Ajira kwa vijana n.k n.k Kwa kufanya hivyo mbivu na mbichi lazima vijitenge tyu...

Mwaka jana mtu anaomba kura chama fulani ety anataka kwenda bungeni ili akamsaidie mueshimiwa rais kazi na watu wanapiga makofi seriously......?

Sema tuendeleee kuiombea nchi yetu, labda kizazi kijacho tutapata viongozi wenye akili
 
Yaliyoandikwa ndani ya huu uzi Ni ukweli mchungu...kiufupi taifa langu Ni km mtoto Alie dumaa hata umlishe vp hawezi kuwa sawa kiakili hata kimwili...

Utendaji wa wizara ya kilimo hauridhishi,Ni km idara tu
 
Absolute.

Ifike pahara watanzania(Hasa vijana) sijui tusiwe na chama kabisa yaani. Yaani hatufungamani na upande wowote ule, tunaangalia sera pekeee za mgombea na chama chake ndo tunapiga kura.Hii itafanya baadhi ya wachumia tumbo wasipate nafasi kushika madaraka.


Mtu anakua Rais hajawai andika hata kitabu, sera na msimamo wake juu ya mambo mbali mbali havijulikani. Anaishia kusema tu ety Tutatekeleza irani yetu ya chama seriously....?

Nilitamani hata 2020 tungekua hata na presidential debate. Wagombea wa nafasi ya urais wawekwe mtu kati. Waandishi wahabari wawaulize maswali ili wawapime mtazamo na uelewa wao juu ya mambo mbali mbali kabla ya kuwapiga kura. Ni lazma watanzania wajue rais tunae taka kumchagua ana msimamo gani juu ya Muungano, Vp kuhusu katiba mpya, Madawa ya kulevya, Democrasia, Rushwaa, Ushoga, Ajira kwa vijana n.k n.k Kwa kufanya hivyo mbivu na mbichi lazima vijitenge tyu...

Mwaka jana mtu anaomba kura chama fulani ety anataka kwenda bungeni ili akamsaidie mueshimiwa rais kazi na watu wanapiga makofi seriously......?

Sema tuendeleee kuiombea nchi yetu, labda kizazi kijacho tutapata viongozi wenye akili
Kabisa mkuu tuwe kama Zambia tu kila awamu kama hukueleweka basi tunamleta madarakani mwingine
 
Yaliyoandikwa ndani ya huu uzi Ni ukweli mchungu...kiufupi taifa langu Ni km mtoto Alie dumaa hata umlishe vp hawezi kuwa sawa kiakili hata kimwili...

Utendaji wa wizara ya kilimo hauridhishi,Ni km idara tu
Mkuu kuna nchi hawana chakula wanakufa njaa kuna sehemu hawana chakula cha kutosha, jambo la kushangaza wakulima kila mwaka wanakosa masoko ya uhakika, lakini hii wizara inashindwa kuwajengea uwezo wakulima wetu kwa ajili ya kupenya kwenye masoko ya kimataifa, viongozi wamejaa blah blah tu
 
Back
Top Bottom