Hivi Tanzania Ina Uongozi Bora? Mheshimiwa Balozi wa Marekani?

Communist

JF-Expert Member
Jun 1, 2012
5,400
1,181
Kwa mujibu wa Mwananchi (2013), Maoni hayo yanatolewa wakati juzi Balozi wa Marekani nchini, Alfonso Lenhardt alitaja sababu za Obama kuja Tanzania kwamba ni kutokana na sifa nzuri za Tanzania. Sifa hizo zilizomvuta Rais Obama ni utawala bora, demokrasia na mazingira bora ya uwekezaji yanayosabisha kukua kwa uchumi.

Balozi wa Marekani alisema Tanzania ni nchi ya mfano linapokuja suala la uongozi bora na ndiyo maana imekuwa na amani, utulivu kwa muda mrefu ikilinganishwa na nchi nyingi za Kusini mwa Jangwa la Sahara.

Napata wasi wasi sana na hizi sifa za kutuvimbisha vichwa ili tuibiwe vizuri. Yaani hayo, maePa, Meremeta, Rada, Mauswisi ndio huyu jamaa anatusifia?

Yaani aache kwenda Rwanda kwa sifa hizi aje hapa kwa wezi wakura. Bado namkumbuka jamaa aliekuwa anakimbia na box la kura kule Segerea. (Utawala Bora?)
 
Mkuu hayo majungu na wivu kama unaona rwanda panakufaa kwa nini hujaenda kuomba uenyeji huko rwanda uhame tanzani ili ukaishi kwa amani kwa mujibu wa matakwa yako,wengi tunajua tunautawala bora kagame kawahi kunyonga watu 200 kwa mkupuo halafu unamsifia kagame.
 
Kama ukiwa kibaraka wa Marekani na ukawa tayari kukidhi their interest utasemwa nao kama mfano wa kuigwa lkn if you are against utakuwa ktk black list yao
 
Mkuu hayo majungu na wivu kama unaona rwanda panakufaa kwa nini hujaenda kuomba uenyeji huko rwanda uhame tanzani ili ukaishi kwa amani kwa mujibu wa matakwa yako,wengi tunajua tunautawala bora kagame kawahi kunyonga watu 200 kwa mkupuo halafu unamsifia kagame.
kama kusifia utawala bora ni kuamia nchi unayoisifia, mbona usimuambii Obama aamie tanzania kwa kuwa ameisifia?
 
balozi gani kama ni balozi kweli ingeletwa tanzania mavi ya kuku kaletwa aje atembelee wajomba zake
 
Hali ya Rushwa Tanzania haijabadilika-Balozi
swiss_ambassador_adri_c1e98.jpg
Akiwa katika hali ya huzuni, Balozi wa Uswisi nchini Tanzania hivi karibuni aliueleza umma wa watanzania na wanadiplosia kuwa, hali ya rushwa nchini Tanzania, toka miezi 13 nyuma alipoizungumzia, haijabadilika na madhara yake yanaendelea kutafuna juhudi za maendelo huku watu wengi wakishindwa kupata huduma.Balozi huyo aliongezea usemi wake kwa kusema, inasikitisha zaidi kuona kuwa tatizo la rushwa ndio kwanza linaendelea kubaki pale pale au kuongezeka na hivyo basi, nguvu zaidi inabidi ielekezwe katika kupambana na adui huyo.

Soma zaidi: Hali ya Rushwa Tanzania haijabadilika-Balozi
 
Deus Bugaywa​
NI jambo la kusikitisha kwamba nchi yetu ni kama inaelekea kuwa nchi ya kuendeshwa kwa matukio, tunajielekeza kuwa taifa lisilo na mipango wala mikakati ya kutekeleza mambo yake isipokuwa kwa kutikiswa na migomo ndiyo tunakumbuka kwamba kuna jambo linahitaji kushughulikiwa.
Unapokuwa na taifa ambalo lina watawala (au viongozi?) ambao wanaona kutimiza wajibu wao bila shinikizo ni tatizo au wanapuuza wajibu huo mpaka watu waingie mitaani ni dalili za wazi za kutokuwa na uongozi thabiti, ni kupungukiwa na uwezo wa kuongoza.
Tanzania ya leo ni kama vile kila kiongozi aliye katika ofisi ya umma yenye mamlaka ya kuamua kitu kwa maslahi ya jamii pana ya taifa hili, amekuja nchini jana, yaani haelewi kabisa mambo gani yanatakiwa yafanyike na kwa namna gani, ni kama yupo pale alipo kwa bahati mbaya.

Soma zaidi: Migomo na ombwe la uongozi!

 
Katika kipindi cha pili cha uongozi wa awamu ya pili, Mwalimu Nyerere aliamini kwamba kulikuwa na ombwe (vacuum) la uongozi katika chama na serikali ya CCM. Na kwa vile hulka (nature) inayo tabia ya kutovumilia ombwe, Mwalimu aliamini kwamba ombwe hilo la uongozi ama lingezibwa na chama cha upinzani (japo hakuona chama kizuri hata kimoja) au CCM iliyojirekebisha. Alisema yafuatayo
Soma zaidi
MATONDO: MWALIMU NYERERE NA OMBWE LA UONGOZI TANZANIA
 
"Waingereza wana msemo: "Nature abhors a vacuum", "hulka huchukia ombwe". Hata siasa huchukia ombwe. Kama uongozi ni mbovu, upo kama haupo, au upo kwa maslahi ya wenyewe, watatokea watu waujaze uwazi uliopo; hauwezi kuachwa wazi hivi hivi. Lakini uongozi mbovu ni kama mzoga, una tabia ya kukaribisha mafisi na mainzi. Tusidhani kuwa hulka ya siasa yetu ni tofauti na hulka ya siasa ya watu wengine; kwamba sisi tunaweza kuvumilia uongozi mbovu na tusivune matunda ya hulka ya uongozi mbovu" (Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania, Zimbabwe Publishing House 1993:52)

Ati, CCM imeshajirekebisha na kuziba ombwe hilo la uongozi chamani na serikalini mwake? Kama bado, wapinzani wana nafasi yo yote ya kuliziba katika uchaguzi wa mwaka kesho? Wapinzani wenyewe, wanao uwezo wa kuweka uongozi imara usiotetereka na wenye kuweka maslahi ya wananchi mbele? Kwa maneno mengine, kuna chama cha upinzani makini ambacho kinaweza kuchukua nafasi ya CCM, na kuleta mabadiliko yatakayolinufaisha taifa?
 
Back
Top Bottom