Hawa wastaafu wengi ndiyo wanadanganywa na wakuu wa taasisi ili kupitisha mambo yao ya hovyo. Kinacho waponza wastaafu wengi kwenye Bodi mbalimbali ni ukata. Wengi wanarubuniwa kwa fedha ndogo za posho, usafiri, umeme nk.Prof Iddris Kikula ameteuliwa tena kuwa mwenyekiti wa Tume ya Madini kwa sasa Prof Kikula anamiaka 78 maana yake katika kipindi hichi cha miaka mitatu atamaliza mkataba akiwa na umri wa miaka 81 , sasa tujiulize ina maana Tanzania hatuna succession plan mpaka tumteue mzee wa miaka 78 kusimamia taasisi nyeti kama hiyo? hawa wanaosoma , wataalam waliopo je hawafai ... sikosoi uteuzi ila najiuliza hatuna succession plan ya rasilimali watu?
Bodi zinahitaji watu wenye nguvu na wenye kusoma makabrasha ya taasisi husika kwenye vikao ili waweze kuhoji yale yanayo endelea.