Hivi Tanzania hatuna succession plan ya rasilimali watu? Mtu ana miaka 70 bado anateuliwa tena jamani...

Prof Iddris Kikula ameteuliwa tena kuwa mwenyekiti wa Tume ya Madini kwa sasa Prof Kikula anamiaka 78 maana yake katika kipindi hichi cha miaka mitatu atamaliza mkataba akiwa na umri wa miaka 81 , sasa tujiulize ina maana Tanzania hatuna succession plan mpaka tumteue mzee wa miaka 78 kusimamia taasisi nyeti kama hiyo? hawa wanaosoma , wataalam waliopo je hawafai ... sikosoi uteuzi ila najiuliza hatuna succession plan ya rasilimali watu?

Hawa wastaafu wengi ndiyo wanadanganywa na wakuu wa taasisi ili kupitisha mambo yao ya hovyo. Kinacho waponza wastaafu wengi kwenye Bodi mbalimbali ni ukata. Wengi wanarubuniwa kwa fedha ndogo za posho, usafiri, umeme nk.

Bodi zinahitaji watu wenye nguvu na wenye kusoma makabrasha ya taasisi husika kwenye vikao ili waweze kuhoji yale yanayo endelea.
 
Unaulizwa Tanzania hatuna succession plan, unataja akina Bidden na Pellosi! Unajua Bidden na Pellosi wamepatikanaje?

Mleta uzi anazungumzia Tanzania hizi nafasi za teuzi kwa mamlaka ya Rais, kwa nini katika watanzania milioni 60 na zaidi iwe a 78 years old man!
Nimekuambia ujuzi hauzeeki, nimekupa mfano tu.sio kila kazi ina limit ya umri...
 
Joe Biden ana miaka mingapi?Spika wa bunge wa Marekani ana miaka 81..afu ujuzi hauzeeki
Hivi una hakika umesoma na umeelewa alichoandika mtoa mada kweli??

Jitahidi kutofautisha alichokisema na nafasi za kisiasa!
 
Hivi una hakika umesoma na umeelewa alichoandika mtoa mada kweli??

Jitahidi kutofautisha alichokisema na nafasi za kisiasa!
Yy kashangaa kwann mzee wa miaka 78 kuteuliwa,anadhani hakuna mtu wa kurithi, nimempa mfano kua watu wnye umri mkubwa na wanashikilia sehemu nyeti,na nikammalizia kua ujuzi hauzeeki...alafu hizi pia ni teuzi ,kwahiyo zinaendana na haja ya Rais,kuteuliwa kwa mtu wa miaka 78,hakumaanishi hakuna watu wadogo zaidi bali ameaminiwa
 
Prof Iddris Kikula ameteuliwa tena kuwa mwenyekiti wa Tume ya Madini kwa sasa Prof Kikula anamiaka 78 maana yake katika kipindi hichi cha miaka mitatu atamaliza mkataba akiwa na umri wa miaka 81 , sasa tujiulize ina maana Tanzania hatuna succession plan mpaka tumteue mzee wa miaka 78 kusimamia taasisi nyeti kama hiyo? hawa wanaosoma , wataalam waliopo je hawafai ... sikosoi uteuzi ila najiuliza hatuna succession plan ya rasilimali watu?

Kazi za ujuzi kwa level ya prof. Kikula unaweza kufanya hata ukiwa miaka 95 maana the more unafanya ndio inakuwa mbobezi zaidi. Tukisema watu wasome wanaibuka kina msukuma wanaongea mavimavi tu. Vijana hatuwezi kuajiriwa wote serikalini especially kwenye level kama hizo za Prof. Wacha wacheche waliobahatika wapate experience waongeze na elimu wengine tupige jalamba kulima parachichi mzee.
 
Wazee wa Tanzania hawajipangi kimaisha baada ya kustafu, so wao wanacho waza ni kuto wapa ujuzi vijana ili wakistafu wawe wanaitwa wao

Sent using Jamii Forums mobile app
Prof yupo vizuri sana aisee, na watoto wamesoma nje na Wana kazi serikalini huko. Tatizo ni uzoefu wake wa kusimamia kazi nadhani unamfanya ateuliwe na huwezi kukataa mkuu akikuamini.
 
Back
Top Bottom