Hivi TANESCO na Tanga Cement kunani lakini?

Ndugu Mtz na Dar,

so far Tanesco hawana ukiritimba tena wa kuzalisha umeme. Kuna players ktk power generation wengine kama IPTL, ambao umfumo huu unaitwa Public Private Partnership. Tatizo bado ku liberalize power supply.

Tusisahau pia kuwa u ghali wa kuendesha Tanesco unatokana na kulipa wazalishaji binafsi pesa nyingi sana, na hii ni matokeo ya mikataba mibovu.

Mfano, 2004 Tanesco walikusanya sh 188.5 bn, wakawalipa wachovu IPTL na wengine sh 124.6 bn (usishangae, unashangaa nini? sijakosea, maji yamezidi unga), 2005,walikusanya sh 221.5 bn, wakawalipa hao washkaji wengine sh 176 bn. 2006, wamekusanya 232 bn, wakawapa hao wazalishaji wengine 242 bn. Mwaka huu, miezi 9 ya mwanzo, wamekula hasara ya zaidi ya 58 bn.

Kuna tatizo la ki ufundi pia, kwamba umeme mwingi unaibiwa kuliko ule unaolipiwa na wateja.

Taasisi nyingi za serikali ni wanaiwa wakubwa. Siasa zinatumika ku neutralize hii.

Mbalamwezi,

Lengo la PPP ni kwamba iko proved kwamba private companies are more efficient when it comes to delivering services compared to public organisations, hence a need to use private companies in delivering these services. Lakini kinachotumika hapo ni kinyume maana umeme wa IPTL ni aghali zaidi na mara nyingi hata hawazalishi lakini wanalipwa. Kwa maoni yangu hiyo si PPP tena bali ni ufisadi.

Serikali inatakiwa ifungue soko la solar energy ili wasindane na Tanesco hasa kwenye maeneo ya mikoani.

Tanesco hawatakiwi kusaini mkataba na mtu au shirika lolote, wanachotakiwa sana sana ni MOU kuonyeshakwamba kama bei itakuwa reasonable watanunua umeme huo. Hivyo mtu yeyeote mwenye uwezo anaweza kuanza kutengeneza umeme na kuwauzia Tanesco. Kitakachoamua ni bei. Hii ni kinyume kabisa na ilivyo sasa.

Nakubaliana na wewe kwamba serikali yenyewe ni wadaiwa. Hapa Tanesco inabidi wawe wakali, ukiondoa idara nyeti kama hospitali, naona idara zingine wakatiwe tu kama hawalipi.
 
Mbalamwezi,

Serikali inatakiwa ifungue soko la solar energy ili wasindane na Tanesco hasa kwenye maeneo ya mikoani.

Ni kweli, wa subsidize zaidi solar equipments na accessories, wa-study umeme wa wind mills pia, na kustep up the use of bio-gas.
 
Samahani, nilikuwa nimetoka. Mimi nadhani tatizo moja la Tanesco ni kutokuwa wabunifu. Wao wanang'ang'ania kukamua jiwe badalöa ya kupanua wigo la watumiaji umeme. Kwa mfano badala ya kuongeza bei ya kuunganisha wangetangaza kuwa wanapuza gharama za kuunganisha kwa asilimia 50 na mteja ataweza kulipa kwa installments na yeyote aliyeunganisha bila ruhusa wataangalia namna ya kumhalalisha. Mimi nadhani watu wengi wangejitokeza na hivyo kupanua wigo la wanaolipa umeme kwa mwezi. Kampuni za simu za mkono ulaya ziko tayari kukupa simu hata bure ili mradi uingie nao mkataba wa kuwa mteja wao kwa miaka kadhaa. Wangeongeza product line kwa kujichimbia kwenye solar,wind na vyanzo vingine mbadala vya nishati. Wauze hizi products na kukubaliana na jamaa kuwa watanunua umeme wowote utakaozidi. Haya yanafanyika kwa wenzetu. Wangeshirikiana na TPDC kuwekeza kwenye bio-diesel. Wawahakikishie wakulima wa alizeti au palm-oil kuwa wako tayari kununua mazao yao ili kuyageuza kuwa diesel. Wenzetu washikauwa na mpango kabambe kuondokana na diesel ya waarabu. Wangeondokana na transformer zinazotumia mafuta. Wangewavuta karibu watumiaji na walipa umeme wakubwa na kuwahakikishia kuwa wako pale kwa ajili yao. Wangekaa na serikali kukubaliana namna subsidy itaweza kuwa phased out. Wangewafungia kazi wadaiwa sugu kwa kuwakatia na kuwafungulia mashtaka. Madeni yasiyolipika wangeyafuta kwenye hesabu zao. Kabla ya yote haya, hata hivyo wanabidi wamwangukie TCC na kuomba mambo yaishie nje ya mahakama ili kuepuka hizo US$ 500 kwa saa watakazowalipa mawakili wao. Wakijidai wabishi watalipa hizi pamoja na bilioni 2 na gharama za TCC. Pengine TCC atakubali milioni 500 na public apology. Dr akumbuke ghafla kuwa ile barua yake ya kujiuzulu alikuwa hajaifuta. hivi huko tanesco hakuna mawakili ambao wangemshauri MD wao? Ikiwa fundi wa kawaida tu alishaona hatma ya haya mavutano kwa nini wao walishindwa kumshauri mwenzao? Au walitaka aingie mkenge!
 
hivi huko tanesco hakuna mawakili ambao wangemshauri MD wao? Ikiwa fundi wa kawaida tu alishaona hatma ya haya mavutano kwa nini wao walishindwa kumshauri mwenzao? Au walitaka aingie mkenge!

Inawezekana Dr Rashid hana team work spirit? Haya ni kinyume kabisa na matarajio waliyonayo waTz kwake! Anawalet down sana!
 
Unamlinganisha Msouth wa Millenium Hotel na TCC? Vitendo kama hivi ndiyo vinawafanya investors wa calibre ya TCC kusita kuwekeza nchini na kutubakizia hao wa Millenium Hotel!

..unafahamu faida wanayoipata kwenye cement?unafikiri wataacha ku-invest?

..kesi kama hii ya kudaiwa na chombo cha umma/serikali si ya kwanza! tra zipo nyingi!na wapuuzi wanalipa hizo kodi walizokwepa/kopa pamoja na faini!

..btw,siwahukumu tcc,lakini sioni haja ya kuwa na mtazamo wa "hear no evil,see no evil"
 
Unajua kodi kubwa kabisa zinalipwa serikalini na Sigara, TBL, Tanga Cement, Twiga Cement, Mbeya Cement? Na ambazo zinatumika kukujengea bara bara wewe mwananchi?

..bila kusahau watu kama metl et al!

Tanesco wamechemsha, na Dr Idris kapigiwa simu na Finance manager wa Tanga Cement over 50 times hajawahi kupokea hata moja, ni biashara ya namna gani wanafanya hawa? wanauza sura?

..you sound like mganga wa kienyeji![no pun!]au unafahamu kwa kina nini kinachoendelea!

Wakati Idris anaamrisha Tanesco wakate umeme Tanga Cement 20.10.2007, kulikuwa na kikao cha majadiliano kinaendelea btwn the two, na huku wanakata umeme ebo!

..ugomvi huu ni kama mambo ya ndani ya nyumba,una chanzo chake na mambo mengine kadhaa yaliyojificha!let's not jump into conclusions !


..swali la mada bado halijafumbuka vizuri!
 
JK amtoe Dr. Idrisa kwenye uongozi wa TANESCO. HAFAI. Period. Kama MD hawezi hata kujua nani ni mteja mashuhuri kwake, basi ni kipofu kuliko hata jongoo.

..kama hufahamu hao wateja mashuhuri ndio wabaya kwa kwenda mbele!waulize wafanyabiashara!
 
Hivi hatujiulizi kwa nini tunapotangaza kuuza mashirika yetu kama ya Simu, Maji,Reli n.k hakuna invetor wa maana anayejitokeza isipokuwa fake kama Richmonds, City Water n.k? Hakuna serious investor atawekezeza kwenye mazingira kama haya tunayoyaona!M.D wa utility company anakataa kupokea simu kutoka kwa strategic investor wake? Mangapi yangeokolewa kama angepokea hiyo simu!

..interesting indeed!yes!

..jibu ni kuwa kama alivyo mwanamke au dada anayechumbiwa,tunababaika na maneno mengi mazuri yaliyo matupu ndani yake!na vijisenti vya hongo ndogondogo!. a suitable suitor haji na longolongo na hajibaraguzi kwa kutoa vijihongo!.sasa,hapo ndio walafi[wapokea mahari na wakati mwingine mchumbiwa]wanapofanya maamuzi bila kujali lengo la kuchumbiwa!.wanamkubali mchumba tapeli!

..vivyo hivyo wa bwana anayetafuta mke!hupumbazwa na marembo ya nje,mikogo,maringo,kujisebua,nk na asijali nini maana ya mke!hivyo hu-end up na balaa ndani ya nyumba badala ya rafiki na msimamizi wa familia!

..it's that simple!.knowing what you need instead of what you want!
 
Dar si Lamu,

Una uhakika na hili? Mimi umeme Dar kwenye nyumba yangu nalipia pesa nyingi zaidi kwa mwezi kuliko ninazolipa hapa UK, why? Wakati gharama za uendeshaji kwa vyovyote UK ziko juu mno hasa kwenye mishahara na pia matumizi yangu ya umeme hapa ni makubwa zaidi ya nikiwa Dar.

..ni kweli!je,wajua kwamba mfumo wa umeme kwa sasa ni hoi kiasi kwamba investment kubwa inahitajika?unafikiri hii italipiwa na nini ili mikopo irejeshwe kwa waliokopesha investors?

..halafu,kuna wizi mkubwa sana wa umeme!nadhani unalifahamu hili!au kama waulize washikaji wako wa sinza,kinondoni,mikocheni,ilala,msasani,masaki,nk!

..wizi huu ukipungua utasaidia kupunguza gharama na kutoa nafuu katika bei!baada ya muda!kumbuka massive investment inahitajika katika infrustructure ya umeme!

Wakiondoa monopoly ya Tanesco huenda bei zikashuka. Wasiwasi wangu tu ni kwamba wakiondoa monopoly basi hao wawekezaji wapya wata concentrate mijini na kuacha sehemu kubwa ya nchi bila umeme. Lakini Tanesco inabidi wabadilike na waache ujinga huu wanaofanya wa kujifanya wao ndio miamba.

..long term,yes!

Kwasasa tungeweka nguvu kubwa kutumia makaa ya mawe kwenye kuzalisha umeme, hii litaleta ajira kwa watu wetu na pia linaweza kupunguza gharama za kuzalisha umeme, japo kutakuwa na madhara kwenye mazingira.

..with you 100%!hayo madhara tuwaache wazungu wahangaike nayo!we don't pollute!we deplete!kama ukifuatilia vizuri!so,what we need is to preserve!and plant!


Pia solar power bado ni aghali sana Tanzania. Jua tunalo la kutosha, tunge encourage matumizi ya solar na pia kuwapa incentives watengenezaji ambao wangetengeneza hizo panel kwa wingi hapo TZ hapo TZ, matokeo yake bei yake ingeshuka sana, mahitaji ya umeme wa Tanesco yangepungua, mambo yaliyotokea 2006 tusingeyaona tena.

..solar ni aghali everywhere!si ndio maana bado wanaendelea ku-develop efficient ones!
 
Ndugu Mtz na Dar,

so far Tanesco hawana ukiritimba tena wa kuzalisha umeme. Kuna players ktk power generation wengine kama IPTL, ambao umfumo huu unaitwa Public Private Partnership. Tatizo bado ku liberalize power supply.

..ofcourse!yuko pia songas,dowans,aggreko na artumas!

..tatizo haliko na halitokuwa kwenye uzalishaji kwa kuwa ni mradi ulio straight forward!

..deal lipo kwenye usambazaji!na hapo ndipo kwenye matatizo na siasa nyingi!a very crazy business indeed!

Tusisahau pia kuwa u ghali wa kuendesha Tanesco unatokana na kulipa wazalishaji binafsi pesa nyingi sana, na hii ni matokeo ya mikataba mibovu.

..very right!

Kuna tatizo la ki ufundi pia, kwamba umeme mwingi unaibiwa kuliko ule unaolipiwa na wateja.

..nadhani tukiliita la kitaifa tutakuwa sahihi zaidi!mkuu, masuala ya kiufundi mengi yako straight forward!

Taasisi nyingi za serikali ni wadaiwa wakubwa. Siasa zinatumika ku neutralize hii.

..yes!
 
..unafahamu faida wanayoipata kwenye cement?unafikiri wataacha ku-invest?

..kesi kama hii ya kudaiwa na chombo cha umma/serikali si ya kwanza! tra zipo nyingi!na wapuuzi wanalipa hizo kodi walizokwepa/kopa pamoja na faini!

..btw,siwahukumu tcc,lakini sioni haja ya kuwa na mtazamo wa "hear no evil,see no evil"

Imani kama hizi ndiyo zimetufikisha hapa tulipo. Tanga Cement ni public traded company ambamo shareholders wake ni Holcim South Africa(62.5%), watanzania wa kawaida(35.4%) na wafanyakazi wa TCC(2.1%). Hii kampuni ni ya kwetu na tukiiiangamiza tunajikata kiganja wenyewe. Management ya TCC iko answerable kwa hawa shareholders na wajibu wake ni mmoja tuu, kuhakikisha kuwa hawa wanapata faida kutokana na investment yao. Hiyo hali ikibadilika,wenye shares wanauwezo wa kuziuza na kujitoa. Kabla ya hayo Management itatoswa. Management watakapotoa ripoti ya mwaka ya utendaji watahojiwa kuhusu kila senti. wenye kiwanda, tukiwemo sisi wenyewe, tutataka kujua hayo malipo ya 49 milioni yalisababishwa na nini na nje ya hapa vibarua chake vitaota nyasi. Kwa hali hiyo hawatakubali kubambikiwa kama tulivyozoea wengine.

Tusijidanganye kuwa sisi watanzania tumebarikiwa sana kiasi cha kwamba hawa mabwana wanalazimika kubaki kwetu. Wanauwezo wa kujitoa na kununua hisa kwenye viwanda kama hivi Kenya, Msumbiji n.k. na kutuachia hiyo mitambo. Na wakiwa huko wakashindaniana na TCC kwenye soko hili hili la kwetu na wote tunajua atakaeshinda nani. Sasa hivi msumbiji ni mshindani mkubwa kwetu katika uwekezaji na nishati anayo kibao. Tusijidanganye kwa uzalendo wa kijinga. Hivi mnaamini kuwa mwekezaji wa maana atavutiwa na maneno ambayo Mheshimiwa Rais wetu atakayowaambia kwenye chakula cha jioni huko kwao bila kuulizia jinsi wawekezaji wengine wanavyomudu? Yale yale ya kuwaambia wasomi walio nje warudi wakati walio nyumbani hauwathamini!

Hizo kesi za TRA dhidi ya mteja wa maana, wameshinda ngapi? Ikiwa hata kwenye mkataba ambao wote tunakubali kuwa ulikuwa mbovu, bado tunashindwa itakuwa kwenye kesi kama hii? Na kwa nini tutafute kesi zisizo na maana ati kwa sababu ziko nyingi kama hizi?

Hakuna mahali ambapo tanesco wamedai kuwa huyu mteja amekuwa halipi kama anavyodai, sh 500 milioni kwa mwezi. Dispute ni juu ya haya madai ya sh 49 milioni. Na wengi wetu, tukiondoa uzalendo, tunajua jinsi tanesco walivyokuwa na kawaida ya kutoa inflated bills, kwa hiyo hili si ajabu. Haiingii kichwani kwetu kwa nini Tanesco hawakuendelea na mazungumzo na huyu mteja wakati wanavuta hizo sh 500 milioni kwa mwezi ambao wao wenyewe wamekiri wanazihitaji sana. Hasira za mkizi!

Maoni yote tunayoyatoa humu ni kutokana na habari ambazo Tanesco wenyewe wanazitoa, sasa hiyo " see no evil...." imetoka wapi? Wenzetu ndiyo mnashindwa kukubali ukweli kuwa huyu mzalendo mwenzenu amechemsha pamoja na maPh.D yake!
 
..nimepitia post kadhaa sijaliona hilo!

..nadhani kuna a lot of misinforming going around!

..with a lot of nice innocent wishes too![/
B]


Ni zipi hizi? Tanesco lini wametoa jipya nje ya kudai kuongeza bei kufidia gharama za uzalishaji. Badala ya kung'ang'ania kumkamua yule anayelipa, lini wametoa mpango kabambe wa kupanua wigo la watumiaji?
 
Mkuu Dar Si Lamu, soma hii hapa chini niliyoitoa kwenye thread nyingine ( samahani Bubu atakae kusema), na utajua kuwa dawa si kuongeza bei maana wateja wameishafikia kikomo cha uwezo wao! Bado wenzangu wanakazania kukamua jiwe.

Lema akisoma tamko hilo, alitaja takwimu za kushuka kwa makusanyo kwamba, mwaka 2004 makusanyo yalifikia asilimia 108, 2005 asilimia 97, 2006 asilimia 87 na kuongeza kwamba mwelekeo huo unakinzana na matarajio ya Tanesco ya kufikia makusanyo ya asilimia 96 kwa miaka mitano ijayo (2007-2011).

"Kwa mfano wizi wa umeme wa watumiaji wakubwa wakishirikiana na wafanyakazi wa Tanesco, hili linanyima uwezo shirika kufikia malengo yaliyokusudiwa na wakati huo huo gharama za uzalishaji na usambazaji ziko pale pale," inasisitiza sehemu ya tamko.
 
..
..you sound like mganga wa kienyeji![no pun!]au unafahamu kwa kina nini kinachoendelea!

..ugomvi huu ni kama mambo ya ndani ya nyumba,una chanzo chake na mambo mengine kadhaa yaliyojificha!let's not jump into conclusions !

Mkuu,so i sound like (mganga!!)

Haya yanasemwa na wahusika kwenye vyombo vya habari. Huwa ninasoma na kuwasikiliza, nikijaribu kupima maelezo yao. Inawezekana chumvi pia wanaweka, lakini Tanesco nao wanauwezo wa kukanusha...lakini hawafanyi hivyo. Kumbuka kuwa free flow of info kwenye taasisi za serikali ni ugonjwa usiotibika hadi sasa.

Private sector hutoa sana info, hasa makampuni yaliyo list kwenye DSE. Hivi kujua mambo kama haya ni interest tu, ya jinsi tunavyoendesha mambo yetu bongo.
 
Wakuu,

Check out the following:

A Lot of misinformation going around

Hapana, tumejitahidi kuleta tunachosikia toka pande zote mbili, Tanga na Tanesco. Kama kuna yeyote anayemisinform public, nadhani upande mwingine ungelalamika juu ya hili, maana wanajuana hawa. Siyo sisi.

What happened to the meter?

Original reasons as given by TCC ni kuwa kuna fuse iliungua kwenye eneo au kwenye mita..(japo kuna wengine humu JF walisema inside info zilisema TCC "ni kawaida yao kutemper nazo".

Lakini Tanesco hawajaelezea hasa ki undani juu ya hili, na ama kuwachukulia hatua TCC kwa kuharibu mita. Hii inaonyesha kuwa pengine si kweli?
 
Tanga Cement ni public traded company ambamo shareholders wake ni Holcim South Africa(62.5%), watanzania wa kawaida(35.4%) na wafanyakazi wa TCC(2.1%). Hii kampuni ni ya kwetu na tukiiiangamiza tunajikata kiganja wenyewe.

Management ya TCC iko answerable kwa hawa shareholders na wajibu wake ni mmoja tuu, kuhakikisha kuwa hawa wanapata faida kutokana na investment yao. Hiyo hali ikibadilika,wenye shares wanauwezo wa kuziuza na kujitoa. Kabla ya hayo Management itatoswa. Management watakapotoa ripoti ya mwaka ya utendaji watahojiwa kuhusu kila senti.

wenye kiwanda, tukiwemo sisi wenyewe, tutataka kujua hayo malipo ya 49 milioni yalisababishwa na nini na nje ya hapa vibarua chake vitaota nyasi. Kwa hali hiyo hawatakubali kubambikiwa kama tulivyozoea wengine.

Kwa namna hoja nyingine zinavyotolewa humu wakuu, ni wazi kuwa hii info haifahamiki kwa wengi. Na si kwa sababu ni classified info, no, ni kwa kuwa tu namna yetu ya kutaka kujua mambo ki undani haikutuwezesha kupekua na kujua hili...ndo maana tunasema kiwanda hiki ni cha Wageni...tunawalinganisha na Millennium Hotel, ooohh wanahamisha faida zote kwao...Really?
 
..fundi,nimekusoma!

..mbalamwezi,nimekusoma pia!

..nadhani majibu ya mada hii yapo kwenye posts hizi!

..kilichobaki ni kuchambua ipi chenga upi mchele mzima!

..shukrani!
 
Dar Si Lamu,

Mwambieni huyo Rashid, watu wamelipia meter miezi na miezi mpaka
sasa wanasota bila umeme, kisa hakuna 3 phase meters, why?

Watengenezaji wa hizo mete wamekufa? Si watoe tender tu na kununua hizo meter?

Mambo mengine hayahitaji hata kuwa mchumi au kusomea management kujua namna ya kuya handle.

kabla ya kufikiria kupandisha umeme, watatue kwanza matatizo ya customers wao.

Wanachukua pesa za watu na miezi sita hakuna huduma, wao mteja hajalipia umeme wiki, wanakata huduma, usawa uko wapi hapo?
 
Dar Si Lamu,

Mwambieni huyo Rashid, watu wamelipia meter miezi na miezi mpaka
sasa wanasota bila umeme, kisa hakuna 3 phase meters, why?

Watengenezaji wa hizo mete wamekufa? Si watoe tender tu na kununua hizo meter?

Mambo mengine hayahitaji hata kuwa mchumi au kusomea management kujua namna ya kuya handle.

kabla ya kufikiria kupandisha umeme, watatue kwanza matatizo ya customers wao.

Wanachukua pesa za watu na miezi sita hakuna huduma, wao mteja hajalipia umeme wiki, wanakata huduma, usawa uko wapi hapo?

Na zikipatikana, utaambiwa bei imebadilika! Sasa badala ya kufanya juu chini ili kila mtu anaetaka umeme anaupata wao wanakazania kupandisha bei! Hii inanikumbusha hao wanaotuuzia maji na flat rate. Mabomba yameota kutu kwa kutokutoa maji lakini kila mwezi wanakudai! Tumeonewa sana na hizi utility companies. Na kwa wenzangu, umeme na maji nchi NYINGI ni huduma kwanza halafu biashara! Ni haki ya kila mwananchi kupata huduma hii kwa malipo yanayoeleweka. Ndiyo maana serikali zote na bunge zao ziko makini juu ya sekta hii!
 
Back
Top Bottom