Hivi Tanesco mnafanya ukarabati saa tisa ya usiku au? Mbona mmekata umeme mara tatu saa tisa usiku?

notifeki

JF-Expert Member
Jan 4, 2013
402
281
Sijui ni umeme umejizima wenyewe au mmekata makusudi au mnafanya ukarabati, ila umeme umekatika na kurudi mara ya tano kuanzia saa nane usiku hadi sasa saa kumi usiku. Jamani mtasababisha watu wafeli mitihani mtu ameamsha anapiga msuli wake usiku mnamkatia umeme ovyo ovyo. Na hapa ninapoongea ni giza balaa. Huu ni uzembe usio na mfano.

Haiwezekani umeme mnatumia vifaa kutoka Ulaya, Marekani, Japan nk, power stations mnazotumia, sub stations, grid lines, transformers ni zilezile zinazotumika Ulaya na Marekani inakuwaje wao umeme wao haukatiki ila nyinyi kila saa unakatika au mnashindwa kuvitumia vifaa mlivyouziwa? Wenzetu wakikata umeme ujue kuna janga maalum kama vile California juzi walikata baadhi ya maeneo kwa sababu kulikuwa na bush fires, ila wao suala la umeme kukatika kizembezembe haiwezekani, nyie wenzetu mkijiskia tu mnakata bila kujua athari mnazotupa sisi watumiaji ambao tunaathirika kiuchumi na kisaikolojia kutokana na kukaa gizani. Imagine nimekaa macho usiku huu wa manane naandika hapa niko gizani nimezungukwa na wachawi athari ninazo pata kisaikolojia mngejua tu.

Kuna haja Rais kuliangalia hili shirika upya. Alafu unakuta mtu eti kasoma Marekani alafu viswitch vidogo vinamshinda ku operate. Mmejazana mandugu humo kwa kujuana shirika hamliwezi kuliendesha. Haiwezekani vifaa vile vile mnavyoagiza Ulaya kwetu viwe vibovu kila siku wakati wao huko kwao hawajui umeme kukatika. Tatizo lenu ni utaalamu mdogo wa ku operate hivyo vifaa hamna excuses.
 
shukuru hukusoma kipindi cha mgao
tanesco wamejitahidi kwakweli yaani now day's umeme unakatika nusu saa tu watu wanapata wanahoji
 
Tena saa tisa usiku,sijui ni konda wa dala dala huyu,saa tisa upo yupo macho
Huko kijijini kwenu mnadanganywa kuwa daresalamu daladala zinatumia umeme wa Tanesco kumbe. Yaani kondakta wa daladala alalamike Tanesco wamekata umeme gari haliendi si ndiyo?
 
Sijui ni umeme umejizima wenyewe au mmekata makusudi au mnafanya ukarabati, ila umeme umekatika na kurudi mara ya tano kuanzia saa nane usiku hadi sasa saa kumi usiku. Jamani mtasababisha watu wafeli mitihani mtu ameamsha anapiga msuli wake usiku mnamkatia umeme ovyo ovyo. Na hapa ninapoongea ni giza balaa. Huu ni uzembe usio na mfano.

Haiwezekani umeme mnatumia vifaa kutoka Ulaya, Marekani, Japan nk, power stations mnazotumia, sub stations, grid lines, transformers ni zilezile zinazotumika Ulaya na Marekani inakuwaje wao umeme wao haukatiki ila nyinyi kila saa unakatika au mnashindwa kuvitumia vifaa mlivyouziwa? Wenzetu wakikata umeme ujue kuna janga maalum kama vile California juzi walikata baadhi ya maeneo kwa sababu kulikuwa na bush fires, ila wao suala la umeme kukatika kizembezembe haiwezekani, nyie wenzetu mkijiskia tu mnakata bila kujua athari mnazotupa sisi watumiaji ambao tunaathirika kiuchumi na kisaikolojia kutokana na kukaa gizani. Imagine nimekaa macho usiku huu wa manane naandika hapa niko gizani nimezungukwa na wachawi athari ninazo pata kisaikolojia mngejua tu.

Kuna haja Rais kuliangalia hili shirika upya. Alafu unakuta mtu eti kasoma Marekani alafu viswitch vidogo vinamshinda ku operate. Mmejazana mandugu humo kwa kujuana shirika hamliwezi kuliendesha. Haiwezekani vifaa vile vile mnavyoagiza Ulaya kwetu viwe vibovu kila siku wakati wao huko kwao hawajui umeme kukatika. Tatizo lenu ni utaalamu mdogo wa ku operate hivyo vifaa hamna excuses.
Katika mashirika yaliyojaza vilaza kwenye taasisi nyeti ni TANESCO!. Sishangai kabisa kuona na kusikia kiongozi mkuu wa nchi akiwachamba watendaji hadharani kwa maneno yasiyo na staha kwani wanayastahili. Juzi usiku wa manane mchezo wa washa zima mara kadhaa ulifanyika maeneo Chanika na hakuna sababu iliyotolewa na wahusika!. Cha kushangaza kila ifikapo saa 12 jioni wao wanakata... Ajabu gani hii?.

Pale Kisarawe kuna mpuuzi mmoja anaitwa Nyanda, nimefahamishwa kuwa ndiye Meneja wa Tanesco pale. Nilimpelekea malalamiko kuwa natumia LUKU lakini nalipia ankara zangu kwa mwezi kabla ya kuhudumiwa, lakini TANESCO hawana huduma ya uhakika kwani mara nyingi tu huwa sina umeme......Jibu alilonipa ni kuwa ninapopata "UNITS" za mwezi mzima umeme unapokatika hazitumiki kwa hiyo hakuna hasara maana ukiwepo nitatumia tu "UNITS" zangu!.

Hivi mtu kama huyu kuwepo TANESCO na mambo hayaendi inavyopaswa, akitumbuliwa atalalamika? Je akiambiwa anafanya kazi kipumbavu hadharani atasema ameonewa? anadhalilishwa?... Wakati umefika sasa wa kuwahukumu wale wote wasiotosha kwenye nafasi zenye maslahi kwa umma, wakafanye kile wanachokiweza zaidi.
 
Back
Top Bottom