Ndikwega
R I P
- Feb 1, 2012
- 5,979
- 5,524
Kuna Jamo ambalo tangia nilipoanza kujiatambua nilianza kujiuliza. Na swali lenyewe ndiyo hili "Hivi Waafrika (Black People) tumelaaniwa au kuna Tatizo gani katika Vichwa Vyetu"?
1. Kwanini Waafrika ndiyo tuwe na Matatizo saana kwenye maswala ya siasa, hususani katika kuachia madaraka katika uongozi wa Nchi? DRC Sasa hivi watu wanauana kisa, Kabila hataki Kuachia Madaraka, Mseveni Kajimilikisha nchi wapinzani wanakiona cha moto, Kagame kajipa nchi mali ya familia yake, Mukurunzinza ndiyo kabisa mpaka sasa hataki hata kusafiri kwa Kuhofia Kupinduliwa, Mughabe daah sijui alizaliwa na Urais mimi sijui.
Katika woote hao wako radhi mufe wote na vyombo ya dola wabakie wao na wale wanaowaunga mkono. NAOMBA lisitokee Tanzania, japo nao wamejimilikisha Nchi kupitia chama chao.
2.Umasikini kupindukia, Waafrika bila shaka ndiyo Bara lenye Watu wengi mafukara kuliko Bara lingine. Ajabu zaidi ndilo Bara lenye Utajiri wa Rasilimali nyingi kuliko Nchi yoyote.
3. Ndiyo watu wasiyojielewa wengi, yaani Wanaacha kuendeleza Bara lao bali Wakiibia Serikalini wanaenda kuweka fedha Ng'ambo ili na huku wanaishi Afrika.
4. Viongozi Wakiumwa wanaenda Kutibiwa Ulaya na India huku wakisifiwa kuwa Hospitali zimeboreshwa.
5.Viongozi wa Afrika hawataki Kukosolewa, na wangependa Mitandao ya Kijamii isiwepo kwavile inawakosoa wakisahu kuwa Dunia inaenda Mbele na hairudi nyuma. Wanapenda mitandao itumike kwa yale wanayoyataka hii ni sawa kutokula Samaki lakini Mchuzi wake Unakunywa, ajabu.
Sasa najiuliza, haya yoote kwanini sisi, je tuna LAANA au ni nini haswa?
1. Kwanini Waafrika ndiyo tuwe na Matatizo saana kwenye maswala ya siasa, hususani katika kuachia madaraka katika uongozi wa Nchi? DRC Sasa hivi watu wanauana kisa, Kabila hataki Kuachia Madaraka, Mseveni Kajimilikisha nchi wapinzani wanakiona cha moto, Kagame kajipa nchi mali ya familia yake, Mukurunzinza ndiyo kabisa mpaka sasa hataki hata kusafiri kwa Kuhofia Kupinduliwa, Mughabe daah sijui alizaliwa na Urais mimi sijui.
Katika woote hao wako radhi mufe wote na vyombo ya dola wabakie wao na wale wanaowaunga mkono. NAOMBA lisitokee Tanzania, japo nao wamejimilikisha Nchi kupitia chama chao.
2.Umasikini kupindukia, Waafrika bila shaka ndiyo Bara lenye Watu wengi mafukara kuliko Bara lingine. Ajabu zaidi ndilo Bara lenye Utajiri wa Rasilimali nyingi kuliko Nchi yoyote.
3. Ndiyo watu wasiyojielewa wengi, yaani Wanaacha kuendeleza Bara lao bali Wakiibia Serikalini wanaenda kuweka fedha Ng'ambo ili na huku wanaishi Afrika.
4. Viongozi Wakiumwa wanaenda Kutibiwa Ulaya na India huku wakisifiwa kuwa Hospitali zimeboreshwa.
5.Viongozi wa Afrika hawataki Kukosolewa, na wangependa Mitandao ya Kijamii isiwepo kwavile inawakosoa wakisahu kuwa Dunia inaenda Mbele na hairudi nyuma. Wanapenda mitandao itumike kwa yale wanayoyataka hii ni sawa kutokula Samaki lakini Mchuzi wake Unakunywa, ajabu.
Sasa najiuliza, haya yoote kwanini sisi, je tuna LAANA au ni nini haswa?