GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,054
- 107,538
Ifike muda sasa Heshima ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iwepo kama enzi za Awamu ya Kwanza, ya Pili, ya Tatu na kidogo ya Nne. Bunge siyo sehemu ya kuingia Wahuni, Watu wakorofi, Vibaka na Watu wasiotaka kwa Makusudi kuhama eneo Hatarishi la Jangwani ambalo kila Siku tu Serikali inawahimiza wahame ili kuokoa Maisha yao na ya Majengo yao Machafu na yaliyochakaa miaka nenda rudi.
Bunge la Awamu ya Tano lenye muendelezo wa Rais wa Sita naona kama vile Hadhi yake ama inaanza Kupotea au huenda hata linadharaulika kwa sasa ambapo limekuwa linapokea tu Wageni ambao wengine wana Upuuzi Upuuzi mwingi na hawana Thamani yoyote ile ya Kimaendeleo kwa Taifa la Tanzania.
Nijuavyo GENTAMYCINE ni kwamba mpaka ukiona umealikwa Bungeni Dodoma na kuketi kule juu katika Visitors Gallery basi ama ni Mtu Muhimu sana na umefanya Jambo Kubwa, jema na lenye Faida na Mantiki kwa nchi ya Tanzania hivyo Wabunge nao wanataka Kukutambua kama Mhimili Mkuu Kikatiba.
Nimesikitika sana jana nilikiona Kikundi fulani cha Wahuni na Washamba Bungeni kinachotokea katika Kitovu Kikuu cha Mafuriko kwa Jiji la Dar es Salaam katikati ya Kigogo na Muhimbili kikiwa Kimealikwa Bungeni na Nguo zao zenye Rangi Mbovu, Kikitambulishwa na baadhi ya Wabunge wasiojielewa wakaanza Kukishangilia.
Nimejaribu kukifuatilia hicho Kikundi kuona labda kimefanya nini cha maana na Kugundua kuwa ndani ya Miaka Mitatu (3) mfululizo na ukielekea wa Nne (4) huu hakuna cha maana kilichofanya hadi jana Kikaribishwe Bungeni na mpaka Wabunge wasiojielewa nao kuanza Kukishangilia.
Spika wa Bunge Ndugu Job Ndugai tafadhali rejesha Heshima ya Jengo hilo la Bunge kwa kuhakikisha kuwa wanaoalikwa hapo wawe ni Watu wa maana na ambao wameleta Chachu ya Kimaendeleo na Ufanisi mkubwa wa Kiuchumi kwa Tanzania yetu na siyo kualika Watu ambao wakipangiwa Ratiba ya kwenda Vitani Kupambana na Adui wao Wanakimbia na kuanza kuleta Visingizio vya kila aina.
Na sijui kama hiyo Jana baadhi ya Vifaa (Electronic Gadgets) hapo Bungeni hawakuviiba au hata Wabunge nao hawakuchomolewa (hawakuibiwa) Simu na Pochi zao kwani Kikundi hicho kinachotoka Kariakoo Bondeni kinajulikana sana kwa Kuiba, Kupiga, Ubishi na Kulalamika hovyo kikiwa katika Majukumu yake yanayotambulika na Jengo moja hivi Kubwa lililopo Karume.
Bunge la Awamu ya Tano lenye muendelezo wa Rais wa Sita naona kama vile Hadhi yake ama inaanza Kupotea au huenda hata linadharaulika kwa sasa ambapo limekuwa linapokea tu Wageni ambao wengine wana Upuuzi Upuuzi mwingi na hawana Thamani yoyote ile ya Kimaendeleo kwa Taifa la Tanzania.
Nijuavyo GENTAMYCINE ni kwamba mpaka ukiona umealikwa Bungeni Dodoma na kuketi kule juu katika Visitors Gallery basi ama ni Mtu Muhimu sana na umefanya Jambo Kubwa, jema na lenye Faida na Mantiki kwa nchi ya Tanzania hivyo Wabunge nao wanataka Kukutambua kama Mhimili Mkuu Kikatiba.
Nimesikitika sana jana nilikiona Kikundi fulani cha Wahuni na Washamba Bungeni kinachotokea katika Kitovu Kikuu cha Mafuriko kwa Jiji la Dar es Salaam katikati ya Kigogo na Muhimbili kikiwa Kimealikwa Bungeni na Nguo zao zenye Rangi Mbovu, Kikitambulishwa na baadhi ya Wabunge wasiojielewa wakaanza Kukishangilia.
Nimejaribu kukifuatilia hicho Kikundi kuona labda kimefanya nini cha maana na Kugundua kuwa ndani ya Miaka Mitatu (3) mfululizo na ukielekea wa Nne (4) huu hakuna cha maana kilichofanya hadi jana Kikaribishwe Bungeni na mpaka Wabunge wasiojielewa nao kuanza Kukishangilia.
Spika wa Bunge Ndugu Job Ndugai tafadhali rejesha Heshima ya Jengo hilo la Bunge kwa kuhakikisha kuwa wanaoalikwa hapo wawe ni Watu wa maana na ambao wameleta Chachu ya Kimaendeleo na Ufanisi mkubwa wa Kiuchumi kwa Tanzania yetu na siyo kualika Watu ambao wakipangiwa Ratiba ya kwenda Vitani Kupambana na Adui wao Wanakimbia na kuanza kuleta Visingizio vya kila aina.
Na sijui kama hiyo Jana baadhi ya Vifaa (Electronic Gadgets) hapo Bungeni hawakuviiba au hata Wabunge nao hawakuchomolewa (hawakuibiwa) Simu na Pochi zao kwani Kikundi hicho kinachotoka Kariakoo Bondeni kinajulikana sana kwa Kuiba, Kupiga, Ubishi na Kulalamika hovyo kikiwa katika Majukumu yake yanayotambulika na Jengo moja hivi Kubwa lililopo Karume.