Hivi sheria za nchi hii zina macho??

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,480
30,152
Moja ya sifa kuu ya sheria huwa inakuwa haina macho, sheria ni kama msumeno unakata huku na kule.

Lakini cha ajabu ni kwamba katika serikali ya awamu ya 5 sheria imekuwa na macho, inaangalia nani amefanya kosa hilo kama ni mteule wa Rais basi sheria hiyo haitamgusa na kama ni mtu mwingine, sheria hiyo itamgusa, tena kwa nguvu zote!

Lilianzishwa hapa zoezi la kuhakiki vyeti, maelfu ya watu wameathirika na zoezi lile, wemgi wamepoteza kazi zao na wamekosa kulipwa hata angalau stahiki zao za kutumikia serikali hii kwa kipindi kirefu.

Lakini lilipokuja kumgusa Mkuu wa mkoa wa Dar, watu wamesema sana kuhusu huyo mtu kutumia jina la mtu mwingine, jambo ambalo ni kinyume cha sheria, kama ambavyo wale maelfu ya waathirika wengine wa serikali, lakini tumeshuhudia mtu huyo akiambiwa na mteule wake kuwa kijana piga kazi!

Tumeshuhudia pia huyo "dogo" huyo akivamia studio za Clouds akiwa na maaskari wenye silaha, za moto lakini tumeshuhudia mtu ambaye ameunda tume kuchunguza tukio lile la kinyama akifukizwa kazi ya uwaziri, huku akimwacha yule "dogo" akiendelea kuchapa kazi!

Tumeshuhudia pia Mkuu wa mkoa wa Arusha akitumia vibaya madaraka yake, mathalani akitumia vibaya rambirambi za wafiwa wa Lucky Vincent, tumeshuhudia pia mteule wake akisema kijana chapa kazi, usisikilize maneno ya mitaani!

Tumeshuhidia pia Mkuu wa wilaya ya Arumeru akifanya vituko vingi, miongoni mwake ni hii skandali inayotrend hivi sasa kwenye social media nyingi kuhusu hiki kituko cha mwaka inayohusu "ununuzi" wa madiwani wa Arumeru, lakini kama ilivyo kawaida ya aliyemteua hatutarajii lolote limtokee huyo jamaa zaidi ya kuambiwa kijana chapa kazi usisikiize maneno ya wapiga debe wa mitaani!

Sass ndiyo nauliza hivi kwenye utawala bora na utawala unaozingatia sheria, hivi makosa yaliyofanywa na wakuu wilaya na mikoa ambao hawako juu ya sheria, hivi si walipaswa kwanza kukaa pembeni na kupisha uchumguzi ili ikithibitika kuwa madudu wanayosemwa ni kweli basi watupishe??

Mimi nimejaribu kueleza kanuni za utawala bora na utawala unaozingatia sheria unavyopaswa kuwa ni hao jamaa wasingestahili kuwepo kwenye nafasi zao za sasa ili kupisha uchunguzi, lakini as usual tutajibiwa na mteule wao kuwa vijana chapeni kazi na msisikilize maneno ya mitaani!

Nchi hii inahitaji maombi makubwa kabisa kwa Mungu wetu ili atuongoze na tuvuke salama safari yetu.
 
Tumeshuhidia pia Mkuu wa wilaya ya Arumeru akifanya vituko vingi, miongoni mwake ni hii skandali inayotrend hivi sasa kwenye social media nyingi kuhusu hiki kituko cha mwaka inayohusu ununuzi wa madiwani wa Arumeru, lakini kama ilivyo kawaida ya aliyemteua hatutarajii lolote limtokee huyo jamaa zaidi ya kuambiwa kijana chapa kazi usisikiize maneno ya wapiga debe wa mitaani!
.
Nitakutahadharisha jambo kuhusu hicho kitu kimoja. Vipi sana kama chama cha madiwani waliopewa rushwa kama mnavyodai kinatoa nadharia gani? Niseme tu chama chenyewe ni CHADEMA. Sasa tukiwaambia kuwa CHADEMA ni chama cha wala rushwa mtasemaje? Madiwani wamekula rushwa wakiwa wanachama wa CHADEMA. Baada ya kuchukua chao wakaamua wasepe na kukitelekeza chama. kwa hiyo CHADEMA ni chama cha wala rushwa na wasaliti.
 
Katiba imeshamezwa, sasa tutarajie nini!?
Hata hayo niliyoyaeleza hapo juu yapo kwenye Katiba ya hivi sasa ya nchi yetu, lakini kwa kiburi kikubwa cha mtawala wetu mambo hayo yanatiwa kapuni, ndiyo maana nimesema nchi hii inahitji maombi makubwa kwa Mungu wetu ili atunusuru na na hali hii.........
 
Hata hayo niliyoyaeleza hapo juu yapo kwenye Katiba ya hivi sasa ya nchi yetu, lakini kwa kiburi kikubwa cha mtawala wetu mambo hayo yanatiwa kapuni, ndiyo maana nimesema nchi hii inahitji maombi makubwa kwa Mungu wetu ili atunusuru na na hali hii.........
Hujui unachokiogea au bado unausingizi. Ibara ipi ya Katiba imekiukwa kulingana na ulichokizungumza?
 
.
Nitakutahadharisha jambo kuhusu hicho kitu kimoja. Vipi sana kama chama cha madiwani waliopewa rushwa kama mnavyodai kinatoa nadharia gani? Niseme tu chama chenyewe ni CHADEMA. Sasa tukiwaambia kuwa CHADEMA ni chama cha wala rushwa mtasemaje? Madiwani wamekula rushwa wakiwa wanachama wa CHADEMA. Baada ya kuchukua chao wakaamua wasepe na kukitelekeza chama. kwa hiyo CHADEMA ni chama cha wala rushwa na wasaliti.
Tunachosema ni kuwa mtoa rushwa na mpokea rushwa wote ni wahalifu.

Kwa hiyo tunachosema kwa tukio hili la Arumeru inabidi huyo DC atupishe, ili uchunguzi wa tukio zima la utoaji na upokeaji rushwa ufanyike ili ukweli ufahamike.
 
Tunachosema ni kuwa mtoa rushwa na mpokea rushwa wote ni wahalifu.

Kwa hiyo tunachosema kwa tukio hili la Arumeru inabidi huyo DC atupishe, ili uchunguzi wa tukio zima la utoaji na upokeaji riishwa ufanyike ili ukweli ufahamike.
Awapishe kwa kosa lipi alilofanya? Tuhuma tupu hazimfanyi kiongozi wa kisiasa ajiuzulu nafasi yake. kama ni kujiuzulu ni kwa utashi wake, sio kushinikizwa.
 
Hujui unachokiogea au bado unausingizi. Ibara ipi ya Katiba imekiukwa kulingana na ulichokizungumza?
Wewe unaongea ki- Lumumba Lumumba.

Tunachoongelea hapa maadili ya kiuongozi yamekiukwa, mtu mwenye dhamana ya kuongoza watu hapaswi kuwa na kashfa....

Kwa hiyo tunachomuomba huyo Mkuu wa wilaya akae pembeni ili uchunguzi huru ufanyike
 
Wewe unaongea ki- Lumumba Lumumba.

Tunachoongelea hapa maadili ya kiuongozi yamekiukwa, mtu mwenye dhamana ya kuongoza watu hapaswi kuwa na kashfa....

Kwa hiyo tunachomuomba huyo Mkuu wa wilaya akae pembeni ili uchunguzi huru ufanyike
Sasa kama kashfa ni za kutengenezwa tena kwa misingi ya kisiasi huyu kiongozi ana kosa gani? Acheni kumnyanyasa bwana.
 
Wewe unaongea ki- Lumumba Lumumba.

Tunachoongelea hapa maadili ya kiuongozi yamekiukwa, mtu mwenye dhamana ya kuongoza watu hapaswi kuwa na kashfa....

Kwa hiyo tunachomuomba huyo Mkuu wa wilaya akae pembeni ili uchunguzi huru ufanyike
Kuna watu humu kama maroboti watakusumbua kichwa. Sometime naona shule za kata zime drain akili za vijana
 
.
Nitakutahadharisha jambo kuhusu hicho kitu kimoja. Vipi sana kama chama cha madiwani waliopewa rushwa kama mnavyodai kinatoa nadharia gani? Niseme tu chama chenyewe ni CHADEMA. Sasa tukiwaambia kuwa CHADEMA ni chama cha wala rushwa mtasemaje? Madiwani wamekula rushwa wakiwa wanachama wa CHADEMA. Baada ya kuchukua chao wakaamua wasepe na kukitelekeza chama. kwa hiyo CHADEMA ni chama cha wala rushwa na wasaliti.
Wacha upumbavuu binti,
 
Kuna watu humu kama maroboti watakusumbua kichwa. Sometime naona shule za kata zime drain akili za vijana
Ni kweli kabisa ulichokiongea Mkuu Return of Undertaker....

Hivi wao hawaoni kasoro hapo kati ya kutumbuliwa bila kuchelewa kwa watendaji wengi wa serikali na "kiigugumizi" kinachomkabili Mkulu inapokuja suala la kumtumbua mtu wake aliyemteua!
 
sheria za tanzania ni kama kinyonga(chameleon) zinabalika kutokana na mazingira na matukio kila siku
 
.
Nitakutahadharisha jambo kuhusu hicho kitu kimoja. Vipi sana kama chama cha madiwani waliopewa rushwa kama mnavyodai kinatoa nadharia gani? Niseme tu chama chenyewe ni CHADEMA. Sasa tukiwaambia kuwa CHADEMA ni chama cha wala rushwa mtasemaje? Madiwani wamekula rushwa wakiwa wanachama wa CHADEMA. Baada ya kuchukua chao wakaamua wasepe na kukitelekeza chama. kwa hiyo CHADEMA ni chama cha wala rushwa na wasaliti.
Na ccm vile vile ni chama cha watoa rushwa c ndio
 
Ni kweli kabisa ulichokiongea Mkuu Return of Undertaker....

Hivi wao hawaoni kasoro hapo kati ya kutumbuliwa bila kuchelewa kwa watendaji wengi wa serikali na "kiigugumizi" kinachomkabili Mkulu inapokuja suala la kumtumbua mtu wake aliyemteua!
Nchi haiongozwi na mihemko ya siasa za wapinzani waliokosa sera. Nchi inaongozwa kwa misingi ya sheria na utawala bora.
 
Back
Top Bottom