Uchaguzi 2020 Hivi Sheria inaruhusu kuzuia Kampeni na Uchaguzi zisiendelee kwa kuomba Zuio la Mahakama iwapo mmoja wa wagombea Urais anahisi kutotendewa haki?

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,013
144,371
Swali: Iwapo ikatokea Tume ya Uchaguzi ikamuengua mgombea Uraisi wa chama kimojawapo;je, mgombea husika anaweza kwenda mahakamani kupinga uchaguzi huo na kuiomba mahakama isitishe mchakato wte wa uchaguzi mpaka kesi ya msingi iishe mahakamani?

Kuna dalili naziona na bila shaka sio mimi peke yangu, hivyo wanaoweza kutupa ufafanuzi tunawaomba watusaidie kujua kama option hii ipo na kama ipo, inaweza kutumika katika mazingira gani.
 
Huyo Kaijage tunamuonya kwamba mipango yoyote miovu anayopanga kwa kuelekezwa asije akamlilia mtu
Kama haiwezekani kupinga maamuzi ya Tume katika chombo chochote kile zikiwemo hata mahakama zetu,basi sheria inayotoa mwanya huu bila shaka itakuwa ni "bad law" na inayokiuka katiba ya nchi yetu inayotambua mhimili wa mahakama kama chombo pekee chenye mamlaka ya kutafsri sheria/kutoa haki.
 
Mkuu kwani we n mgeni hapa tz hadi uulize swali kama hilo, anyway ngoja nikujibu,,,Inategemeana na mgombea ataeenguliwa atakuwa ni wa chama gani,,,,ila kama ikitokea ni Lissu au Maalim Seif ndo wameenguliwa, basi ata wakienda mahakami haiwezi saidia chochote,

NB: Muhimu tuombe Mungu jambo la aina hiyo lisitokee
 
Nafikiri mgonjwa wa ubelgiji arudishwe hospitalini na kupokea utimamu wa akili kwanza na Kisha alazwe milembe mpaka baada ya miezi sita ndio achekiwe tana Kama anaweza ruhusiwa kutoka wodini🤣😂🤣! Maana siyo kwa uchizi huu I see!
 
Mkuu kwani we n mgeni hapa tz hadi uulize swali kama hilo, anyway ngoja nikujibu,,,Inategemeana na mgombea ataeenguliwa atakuwa ni wa chama gani,,,,ila kama ikitokea ni Lissu au Maalim Seif ndo wameenguliwa, basi ata wakienda mahakami haiwezi saidia chochote,

NB: Muhimu tuombe Mungu jambo la aina hiyo lisitokee
Nakuhakikishi kwamba huu waweza kuwa ndio mwisho wa Tanzania kuwepo duniani
 
Kama haiwezekani kupinga maamuzi ya Tume katika chombo chochote kile zikiwemo hata mahakama zetu,basi sheria inayotoa mwanya huu bila shaka itakuwa ni "bad law" na inayokiuka katiba ya nchi yetu inayotambua mhimili wa mahakama kama chombo pekee chenye mamlaka ya kutafsri sheria/kutoa haki.
Mambo ya katiba mpya ndiyo yalikuwa yaongelewe na upinzani kwa nguvu sana lakini wao wakawa ni wa kupinga serikali kwa mambo ambayo ni trivial tu, kuzusha habari zisizothibitika za trilion 1.5, kuandika barua World bank, kudai maandamano na kufanya fujo magerezani.

Leo miaka mitano inapita, hakuna hata mbunge mmoja wa upinzani aliyewahi kuzungumzia swala la katiba mpya na sasa ndipo wanajua wataingia kwenye uchaguzi kwa katiba na sheria hizo; kumbuka kuwa sheria ni msumeno.
 
mambo ya katiba mpya ndiyo yalikuwa yaongelewe na upinzani kwa nguvu sana lakini wao wakawa ni wa kupinga serikali kwa mambo ambayo ni trivial tu, kuzusha habari zisizothibitika za trilion 1.5, kuandika barua World bank, kudai maandamano na kufanya fujo magerezani. Leo miaka mitano inapita, hakuna hata mbunge mmoja wa upinzani aliyewahi kuzungumzia swala la katiba mpya na sasa ndipo wanajua wataingia kwenye uchaguzi kwa katiba na sheria hizo; kumbuka kuwa sheria ni msumeno.
Mkuu unaishi Nchi gani? Mbona wapinzani wamepiga kelele sana kuhusu kua na katiba mbovu miaka nenda rudi!

Sikio la kufa halisikii dawa, ni mda wa damu kumwagika tu. Mwisho wa uvumilivu umefika.
 
looh! Mpaka aibu kwa mtu mwenye elimu Kama wewe unaongea utumbo shauri ya siasa za ukanda tu.
mambo ya katiba mpya ndiyo yalikuwa yaongelewe na upinzani kwa nguvu sana lakini wao wakawa ni wa kupinga serikali kwa mambo ambayo ni trivial tu, kuzusha habari zisizothibitika za trilion 1.5, kuandika barua World bank, kudai maandamano na kufanya fujo magerezani. Leo miaka mitano inapita, hakuna hata mbunge mmoja wa upinzani aliyewahi kuzungumzia swala la katiba mpya na sasa ndipo wanajua wataingia kwenye uchaguzi kwa katiba na sheria hizo; kumbuka kuwa sheria ni msumeno.
 
Mkuu unaishi Nchi gani? Mbona wapinzani wamepiga kelele sana kuhusu kua na katiba mbovu miaka nenda rudi!

Sikio la kufa halisikii dawa, ni mda wa damu kumwagika tu. Mwisho wa uvumilivu umefika.

Swala la katiba lilipamba moto mwaka 2010 ndipo Kikwete akaunda Tume ya Waryoba; hata hivyo mapenedekezo ya tume yalipozimwa, hakuna aliyewahi kuliongelea tena kwa msukumo. Kuna manung'uniko ya mara kwa mara lakini siyo msukumo wenye nguvu; kila mwaka bajeti ya Wizara ya Sheria na katiba hupita misukosuko yoyote ya kudai katiba mpya. Huwa ni manung'uniko tu.
looh! Mpaka aibu kwa mtu mwenye elimu Kama wewe unaongea utumbo shauri ya siasa za ukanda tu.
Kweli jisikie aibu kwani hujui kujibu mada yaani unakimbili vijambo vya kijiweni tu; kama huna elimu siyo kosa langu na siwezi kukusaidia.
 
Back
Top Bottom