GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,545
- 108,873
Yaani hadi najuta sijui ni kwanini nimekuwa Mpayapaya/ Masikini/ Mbayuwayu hivi kiasi kwamba miaka yangu nenda rudi nashindwa kupata Kipato cha hata Kununua tu ‘ Simenti ‘ mfuko Mmoja ili name nianze Ujenzi wa Kujenga ‘ Kakibanda ‘ Kangu niondokane na ‘ manyanyaso ‘ ya ‘ Kimakusudi ‘ kabisa kutoka kwa wenye Nyumba wangu.
Kisa kilichofanya nihame Nyumba ya Kwanza ambapo Kodi ilikuwa ni Tsh 30,000/= tu (ila Panya utaishi nao humo) niliyopanga ni Sharti la ‘ Kimanyanyaso ‘ kutoka kwa Mama mwenye Nyumba wangu ambapo aliniambia kuwa hapo Nyumbani Kwake hataki Kuona Mgeni wa Kike ila wa Kiume muda wowote ule akaribie na hata akitaka Kulala alale nikamuuliza kwanini jibu alilonipa nikitaka nipange kama siwezi niondoke ‘ Kidume ‘ nikavumilia.
Baadae tena nikahama pale na kwenda Kupanga Kwingine ambapo Kodi yake ilikuwa ni Tsh 35,000/= ( ila Mende ni Marafiki zangu ) ambapo huko napo nilikumbana na Sharti kutoka kwa mwenye Nyumba wangu kuwa Siku Yanga SC ikishinda tu basi kutakuwa na Mchango wa Lazima wa Kusheherekea ushindi nje ya Nyumba yake na kwamba hata ukiwa Mshabiki wa Simba SC utachangia tu. Nilipohoji Kwanini nikajibiwa nikajenge Kwangu.
Sasa nina kama Wiki ya Pili hivi nimehama na nimepanga Kwingine ambapo Kodi yake ni Tsh 40,000/= (ila Paka Usiku lazima waje Kulala jirani na Dirisha langu) ambapo kiukweli ni Nyumba nzuri na ina Mazingira mazuri tu ila Sharti nililokumbana nalo hadi hivi leo nalitafakari bado sijalipatia Jibu lake. Mwenye Nyumba wangu huyu mpya kaniambia nipike niwezavyo humo ndani ila hataki Kusikia ninakaanga Mayai na Siku akisikia basi ‘ Notisi ‘ ya Kuhama nitaikuta chini ya Mlango pale nikishatoka katika Mizunguko yangu ya Kubeba Zege. Nilipomhoji Kwanini nae akaniuliza kuna Mfuko wowote wa ‘ Simenti ‘ nilimchangia wakati anaanza Ujenzi wa hiyo Nyumba?
Najua hapa Jamvini (JamiiForums) Watu wa Serikali wapo (na hasa hasa Waziri husika Lukuvi na Wasaidizi wake) hebu tafadhalini Serikali jitahidi mtunge Sheria Kali ya ‘ Kuwabana ‘ hawa Wamiliki wa Nyumba ambazo Sisi ‘ Walalahoi ‘ akina GENTAMYCINE tunapanga kwani kiukweli ‘ wanatunyanyasa ‘ na ‘ tunanyanyasika ‘ mno tu. Kuna Rafiki yangu Mmoja yupo Kinzudi huko amepanga na Kilichomkuta anajuta hata kwanini hajarudi tu Kijijini Kwao Kuishi kwani Sharti pekee alilopewa na Mwenye Nyumba wake ni kwamba awe ‘ anakunya ‘ mara moja tu Siku nzima ili Choo Kisijae hali inayomlazimu Jamaa yangu huyo nae awe na Ratiba yake ‘ mbadala ‘ ya Kujisaidia Haja Kubwa hiyo (Kunya) katika Nyumba za ‘ Masela ‘ wake kwani Yeye ameshajizoesha ‘ Kunya ‘ angalau mara mbili au tatu kwa Siku kutokana na ‘ Ulaji ‘ wake.
Tunajua kuwa Nyumba ni zao ila na Wao basi angalau ‘ Watuthamini ‘ na Sisi Wapangaji Wao (Choka Mbaya) akina GENTAMYCINE kwani siyo Siri hapa duniani tunaishi kwa Kutegemeana hivyo hakuna haja ya ‘ Kunyanyasana ‘ kwa Masharti ya ‘ Kikatili / Kishalubela ‘ kama haya. Hela yenu ya Kodi tuitafute kwa shida na huku Majumbani mwenu tena mnatupa Masharti haya magumu hivi mnataka tuwe Wageni wa nani? Inauma sana Serikali iingilie kati katika hili na nitawashukuru.
Kisa kilichofanya nihame Nyumba ya Kwanza ambapo Kodi ilikuwa ni Tsh 30,000/= tu (ila Panya utaishi nao humo) niliyopanga ni Sharti la ‘ Kimanyanyaso ‘ kutoka kwa Mama mwenye Nyumba wangu ambapo aliniambia kuwa hapo Nyumbani Kwake hataki Kuona Mgeni wa Kike ila wa Kiume muda wowote ule akaribie na hata akitaka Kulala alale nikamuuliza kwanini jibu alilonipa nikitaka nipange kama siwezi niondoke ‘ Kidume ‘ nikavumilia.
Baadae tena nikahama pale na kwenda Kupanga Kwingine ambapo Kodi yake ilikuwa ni Tsh 35,000/= ( ila Mende ni Marafiki zangu ) ambapo huko napo nilikumbana na Sharti kutoka kwa mwenye Nyumba wangu kuwa Siku Yanga SC ikishinda tu basi kutakuwa na Mchango wa Lazima wa Kusheherekea ushindi nje ya Nyumba yake na kwamba hata ukiwa Mshabiki wa Simba SC utachangia tu. Nilipohoji Kwanini nikajibiwa nikajenge Kwangu.
Sasa nina kama Wiki ya Pili hivi nimehama na nimepanga Kwingine ambapo Kodi yake ni Tsh 40,000/= (ila Paka Usiku lazima waje Kulala jirani na Dirisha langu) ambapo kiukweli ni Nyumba nzuri na ina Mazingira mazuri tu ila Sharti nililokumbana nalo hadi hivi leo nalitafakari bado sijalipatia Jibu lake. Mwenye Nyumba wangu huyu mpya kaniambia nipike niwezavyo humo ndani ila hataki Kusikia ninakaanga Mayai na Siku akisikia basi ‘ Notisi ‘ ya Kuhama nitaikuta chini ya Mlango pale nikishatoka katika Mizunguko yangu ya Kubeba Zege. Nilipomhoji Kwanini nae akaniuliza kuna Mfuko wowote wa ‘ Simenti ‘ nilimchangia wakati anaanza Ujenzi wa hiyo Nyumba?
Najua hapa Jamvini (JamiiForums) Watu wa Serikali wapo (na hasa hasa Waziri husika Lukuvi na Wasaidizi wake) hebu tafadhalini Serikali jitahidi mtunge Sheria Kali ya ‘ Kuwabana ‘ hawa Wamiliki wa Nyumba ambazo Sisi ‘ Walalahoi ‘ akina GENTAMYCINE tunapanga kwani kiukweli ‘ wanatunyanyasa ‘ na ‘ tunanyanyasika ‘ mno tu. Kuna Rafiki yangu Mmoja yupo Kinzudi huko amepanga na Kilichomkuta anajuta hata kwanini hajarudi tu Kijijini Kwao Kuishi kwani Sharti pekee alilopewa na Mwenye Nyumba wake ni kwamba awe ‘ anakunya ‘ mara moja tu Siku nzima ili Choo Kisijae hali inayomlazimu Jamaa yangu huyo nae awe na Ratiba yake ‘ mbadala ‘ ya Kujisaidia Haja Kubwa hiyo (Kunya) katika Nyumba za ‘ Masela ‘ wake kwani Yeye ameshajizoesha ‘ Kunya ‘ angalau mara mbili au tatu kwa Siku kutokana na ‘ Ulaji ‘ wake.
Tunajua kuwa Nyumba ni zao ila na Wao basi angalau ‘ Watuthamini ‘ na Sisi Wapangaji Wao (Choka Mbaya) akina GENTAMYCINE kwani siyo Siri hapa duniani tunaishi kwa Kutegemeana hivyo hakuna haja ya ‘ Kunyanyasana ‘ kwa Masharti ya ‘ Kikatili / Kishalubela ‘ kama haya. Hela yenu ya Kodi tuitafute kwa shida na huku Majumbani mwenu tena mnatupa Masharti haya magumu hivi mnataka tuwe Wageni wa nani? Inauma sana Serikali iingilie kati katika hili na nitawashukuru.