Hivi serikali ipi inayotoa mchano na serikali ya mapinduzi ya zanzibar katika mfuko wa pamoja

BUMIJA MOSSES

Member
Dec 5, 2012
67
23
NDG, WANAJF
Naomba tujadili kuhusu Mchango na Mgawanyo wa Mapato ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania:

1. Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977 (TOLEO LA MWAKA 2005), ibara ya 133 inasema " Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itatunza akaunti ya Fedha ya pamoja na ambayo itakuwa ni sehemu ya Mfuko Mkuu wa Hazina ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambamo kutawekwa fedha yote itakayochangwa na Serikali mbili kwa kiasi kitakachoamuliwa na tume ya pamoja ya fedha kwa mujibu wa sheria iyotungwa na Bunge, kwa madhumuni ya shughuli za Jamhuri ya Muungano kwa mambo ya Muungano"

2.Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 (TOLEO LA MWAKA 2010), ibara ya 114 inasema "fedha zote ambazo ni sehemu ya mchango wa muungano ambazo Serikali ya Mapinduzi Zanzibar inawajibika kulipa zitakuwa ni gharama inayotoka Mfuko Mkuu wa Hazina.

Maswali muhimu ya Mjadala:

1. Je Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ndio inayochangia kama moja ya Serikali, baada ya kungoja kuchangiwa na Serikali mbili

2. Je, kama Serikali ya Muungano si moja ya Serikali zinazochangia, Serikali ipi inachangia Mfuko Mkuu wa Hazina ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

WANAJF naomba ufafanuzi.
 
Nafikiri kabla ya kuangalia mgawanyo tuangalie kwanza kila sehemu ya Muungano inachangia kiasi gani kwenye mfuko huo!
 
NDG, WANAJF
Naomba tujadili kuhusu Mchango na Mgawanyo wa Mapato ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania:

1. Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977 (TOLEO LA MWAKA 2005), ibara ya 133 inasema " Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itatunza akaunti ya Fedha ya pamoja na ambayo itakuwa ni sehemu ya Mfuko Mkuu wa Hazina ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambamo kutawekwa fedha yote itakayochangwa na Serikali mbili kwa kiasi kitakachoamuliwa na tume ya pamoja ya fedha kwa mujibu wa sheria iyotungwa na Bunge, kwa madhumuni ya shughuli za Jamhuri ya Muungano kwa mambo ya Muungano"

2.Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 (TOLEO LA MWAKA 2010), ibara ya 114 inasema "fedha zote ambazo ni sehemu ya mchango wa muungano ambazo Serikali ya Mapinduzi Zanzibar inawajibika kulipa zitakuwa ni gharama inayotoka Mfuko Mkuu wa Hazina.

Maswali muhimu ya Mjadala:

1. Je Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ndio inayochangia kama moja ya Serikali, baada ya kungoja kuchangiwa na Serikali mbili

2. Je, kama Serikali ya Muungano si moja ya Serikali zinazochangia, Serikali ipi inachangia Mfuko Mkuu wa Hazina ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

WANAJF naomba ufafanuzi.
 
Hakuna atakaeweza kujibu maswali hayo,mhusika mmoja kwenye muungano amefariki na maiti yake haijulikani ilipo.
 
Back
Top Bottom