Luteni
JF-Expert Member
- Jan 9, 2010
- 2,274
- 301
Ndugu wana jamvi nimejitahidi kutega sikio nisikie angalau salamu za rambirambi kutoka serikalini lakini hadi msiba unakwisha sikusikia chochote, ina maana serikali imesusia raia wake?
Ninavyofahamu mimi waliokufa ni watanzania regardless wanatoka chama gani, ingependeza sana na serikali ingeonekana ungwana kama ingewakilishwa na kiongozi yeyote msibani na kujitambulisha rasmi hata kutoa mkono wa pole.
Naomba kama kuna mwana JF aliyekuwepo kwenye msiba au hata kasikia ni kiongozi fulani anisaidie. Tuelewe kwamba sisi sote ni watanzania tunajenga nchi moja mazuri na mabaya yakitokea ni yetu sote. Siku Tanzania ikibarikiwa neema tutakaofaidi ni watanzania na si Chadema, CCM wala CUF pekee.
Nitasikitika sana endapo serikali yangu itakuwa haijawakilishwa.
Naomba kutoa hoja.
Ninavyofahamu mimi waliokufa ni watanzania regardless wanatoka chama gani, ingependeza sana na serikali ingeonekana ungwana kama ingewakilishwa na kiongozi yeyote msibani na kujitambulisha rasmi hata kutoa mkono wa pole.
Naomba kama kuna mwana JF aliyekuwepo kwenye msiba au hata kasikia ni kiongozi fulani anisaidie. Tuelewe kwamba sisi sote ni watanzania tunajenga nchi moja mazuri na mabaya yakitokea ni yetu sote. Siku Tanzania ikibarikiwa neema tutakaofaidi ni watanzania na si Chadema, CCM wala CUF pekee.
Nitasikitika sana endapo serikali yangu itakuwa haijawakilishwa.
Naomba kutoa hoja.