Uchaguzi 2020 Hivi Rais Magufuli kuwaahidi nafasi za uteuzi akina Andrew Chenge, siyo kutonesha kidonda kwa mamilioni ya vijana wasiokuwa na Ajira?

Si ndio ahadi za wagombea za watatufanyia nini tukiwapa uongozi? Na baada ya miaka mitano tutawauliza kama wametimiza ahadi zao? Ndio ujue ahadi zozote zinazotolewa ni HONGO takatifu ili tupate mchecheto tuwachague. Hongo mbaya haiahidiwi, inatolewa papo kwa papo unapoitoa kama mgombea😂😂

Hongereni sana wanaChadema kwa kuwa na msimamo huo wa ki-Mandela!

Pamoja na kupitia mateso makubwa sana, chini ya utawala huu wa awamu ya 5, lakini mmetoa msimamo wenu kuwa iwapo wananchi watawapa ridhaa ya kuongoza nchi hii kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka huu, hamtalipiza kisasi kabisa!
 
Katambi amemuaminisha Jiwe kuwa Tundu Lissu ni level yake na anauwezo wa kumpa makavu hadharani. Kwa muda huu Jiwe Akimpata mtu mwenye uwezo huo anaweza kulabidhiwa hata Bombardier iwe mali yake yeye mkewe na watoto wake.
Huyo Magufuli kama anajiamini kweli, ni kitu gani kinamfanya aogope, kuandaliwa mdahalo na mgombea mwenzake wa kiti cha urais Tundu Lissu?

Kwa yeye Tundu Lissu yupo tayari kuingia katika mdahalo huo, hata kama utakuwa umeandaliwa kesho!
 
Hongereni sana wanaChadema kwa kuwa na msimamo huo wa ki-Mandela!

Pamoja na kupitia mateso makubwa sana, chini ya utawala huu wa awamu ya 5, lakini mmetoa msimamo wenu kuwa iwapo wananchi watawapa ridhaa ya kuongoza nchi hii kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka huu, hamtalipiza kisasi kabisa!
Umekosea, tuko kwenye mada ya hongo!! Sema "Hongera Chadema kwa kutoa Hongo takatifu"😂😂
 
Huyo Magufuli kama anajiamini kweli, ni kitu gani kinamfanya aogope, kuandaliwa mdahalo na mgombea mwenzake wa kiti cha urais Tundu Lissu?

Kwa yeye Tundu Lissu yupo tayari kuingia katika mdahalo huo, hata kama utakuwa umeandaliwa kesho!
Mengi aliyofanya Magufuli katika hii miaka mitano yana maswali ambayo hata yeye mwenyewe binafsi hana majibu.
 
kwa akili yako unaweza kutoka chuo tu ukateuliwa kuwa balozi au katibu mkuu nishati na madini?
vijana someni lakini msitegemee kuajiriwa na serikali
Salim Ahmed Salim aliteuliwa kuwa Balozi akiwa na umri wa miaka 26? na akapaa mpaka kugombea Ukatibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa akishindwa kwa kura ya turufu akiishia kuwa Katibu Mkuu wa AU. Vijana wanaweza kufanya maajabu wakipewa nafasi!
 
Salim Ahmed Salim aliteuliwa kuwa Balozi akiwa na umri wa miaka 26? na akapaa mpaka kugombea Ukatibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa akishindwa kwa kura ya turufu akiishia kuwa Katibu Mkuu wa AU. Vijana wanaweza kufanya maajabu wakipewa nafasi!
acha kukariri maisha.mambo ya 1962 unalinganisha na sasa?wakati huo wasomi walikua wachache sana
 
Yaani huwa najaribu kuweza, hivi huyu Magufuli anaelewa kweli kuwa yupo katika kampeni?

Utawezaje kuwaahidi vyeo watu, wakati huelewi kama utashinda uchaguzi huo au laa?

Kwanza huo mchakamchaka, anaoendeshwa na Lissu, siyo wa kawaida!

Mathalani tuchukulie, ameshindwa kwenye uchaguzi huu, hivi hivyo vyeo anavyowaahidi kina Chenge, atawapa akina Chenge, atakapokuwa Chato, akiwa Rais mstaafu?

Hii ni sawasawa na ule msemo wa wahenga, unaosema USIMTUKANE MAMBA KABLA HUJAVUKA MTO
Anaanzaje kushinwa ameshapita tokea 2015 mwezi ujao kukamilisha ratiba tu
 
acha kukariri maisha.mambo ya 1962 unalinganisha na sasa?wakati huo wasomi walikua wachache sana
Wewe kada kwanini huukubali ukweli unaoambiwa?

Hivi huyu Mzee Chenge, unategemea afanye muujiza gani, katika nafasi hizo za uteuzi?

Acha kukariri kwa kufikiria kuwa hao wazee peke yao ndiyo wanaofaa kwa nafasi hizo za uteuzi
 
Acha kukariri kwa kufikiria kuwa hao wazee peke yao ndiyo wanaofaa kwa nafasi hizo za uteuzi
uzee dawa
ina maana baba yako mzazi si lolote si chochote kisa ni mzee?
umetoka tu university huna expurience exposure,unataka uteuliwe kuwa DG TBS??Inabidi uwe karibu sana na Mungu
 
Kunaushenzi wahali juu sana ajira tumeambiwa mara nyingi tujiajiri wenyewe lakini kwa wakina.change.masele.nk hawawezi kujiari tumuondoe mtu huyu niadui wa watanzania mbaguzi hawataki wanyonge lakini hujifanya yeye niwawanyonge
Ndiyo vijana mjue mna Rais wa aina gani.............

Yeye ni bingwa wa kufanya maigizo, akiwa kwenye majukwaa ya kisiasa, ana-pretend kuwa yeye ni Rais wa wanyonge.........

Lakini katika hali halisi, hao wanyonge "anawanyonga" taratibu!
 
Back
Top Bottom