Hivi Rais Magufuli kuruhusu Polisi kuua majambazi bila kuchukuliwa hatua zozote za kisheria, je hiyo siyo kuingilia mhimili wa mahakama?

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,479
30,144
Tumemsikia wenyewe kwa masikio yetu wenyewe, Rais Magufuli katika shughuli ya kufunga mafinzo ya Polisi Kurasini, akiwaambia Polisi kuwa yeye anawaruhusu kuua majambazi na Polisi hao hawapaswi kukamatwa na kupelekwa mahakamani kujibu tuhuma hizo!

Nimeshangazwa sana na kauli hiyo ya Rais ya "kuruhusu" askari wetu kuua na wasipelekwe mahakamani, kwa kuwa nijuavyo kwa mujibu wa Katiba ya nchi, ni mhimili wa mahakama pekee ndiyo unaoweza kuthibitisha tuhuma za mwananchi yeyote na kutoa adhabu, ambayo itakuwa kwa mujibu wa "penal code" kwa mtuhumiwa huyo iwapo itathibitika kuwa yeye ni jambazi

Hivi Rais Magufuli anapowapa kiburi cha aina hii Polisi, anategemea hali itakuwaje nchini??

Natabiri kuwa raia wema wengi watauliwa, kwa "kisingizio" kuwa wao ni majambazi!

Hivi Rais Magufuli anaweza kutwambia Jeshi letu la Polisi lina "credibility" gani hadi kuaminiwa kuua na wasiulizwe chochote??

Hivi kwa Jeshi hili la Polisi, ambalo kuna watanzania wenzetu wengi wamepotea katika mazingira ya kutatanisha na hadi Leo hatujui waliko na Jeshi letu la Polisi lipo na linadai linaendelea na uchunguzi

Jeshi letu la Polisi limeshindwa kutuambia yuko wapi Ben.Saanane, ambaye tokea kupotea kwake ni zaidi ya miaka 2 sasa

Jeshi letu la Polisi limeshindwa kutuambia yuko wapi, Azory Gwanda, ambaye tokea kupotea kwake ni zaidi ya mwaka mmoja sasa

Jeshi letu la Polisi limeshindwa kumkamata hata mtuhiwa mmoja, kati ya wale waliojaribu kumwua kwa kumpiga risasi Mbunge wa Singida Madhariki, Mheshimiwa Tundu Lissu, zaidi ya mwaka mmoja tokea tukio hilo litokee

Vile vile nimkumbishe tu kidogo Rais Magufuli, kuhusu principle kubwa sana ya sheria inayosema kuwa A MAN CAN NOT BE A JUDGE IN HIS OWN CASE

Kwa kuwaruhusu Polisi waue kwa "kisingizio" cha kuwamaliza majambazi, maana yake ni kuwa keshawaruhisu mapolisi wawe ni mahakimu katika kesi imayowakabili wao wenyewe!

Hivi atajuaje kama Polisi ameua jambazi au amemwua raia mwema asiye na hatia kwa sababu zake binafsi??

  • Ni muhimu kila mhimili wa dola ufanye kazi zake kwa mujibu wa Katiba ya nchi unavyoelekeza

Mungu ibariki Tanzania
 
Kwa kweli INAOGOPESHA sana! Yaana TANZANIA yetu ILEEEEEEEEEEEE! Kama MUNGU acpotupigania CJUI ITAKUWAJE! Kwani WASHAURI, WASTAAFU, WAZEE nk cjui kama WANAWAJIBIKA kwa mheshimiwa wetu! Au labda HAWASIKILIZWI
 
Sasa hivi tunainyoosha nchi kwanza.
Inabidi tuinyooshe nchi huku tukizingatia Katiba ya nchi......

Hatuwezi tukatoa kisingizio cha kuinyoosha nchi huku tukiisigina waziwazi Katiba ya nchi!
 
Tumemsikia wenyewe kwa masikio yetu wenyewe, Rais Magufuli katika shughuli ya kufunga mafinzo ya Polisi Kurasini, akiwaambia Polisi kuwa yeye anawaruhusu kuua majambazi na Polisi hao hawapaswi kukamatwa na kupelekwa mahakamani kujibu tuhuma hizo!

Nimeshangazwa sana na kauli hiyo ya Rais ya "kuruhusu" askari wetu kuua na wasipelekwe mahakamani, kwa kuwa nijuavyo kwa mujibu wa Katiba ya nchi, ni mhimili wa mahakama pekee ndiyo unaoweza kuthibitisha tuhuma za mwananchi yeyote na kutoa adhabu, ambayo itakuwa kwa mujibu wa "penal code" kwa mtuhumiwa huyo iwapo itathibitika kuwa yeye ni jambazi

Hivi Rais Magufuli anapowapa kiburi cha aina hii Polisi, anategemea hali itakuwaje nchini??

Natabiri kuwa raia wema wengi watauliwa, kwa "kisingizio" kuwa wao ni majambazi!

Hivi Rais Magufuli anaweza kutwambia Jeshi letu la Polisi lina "credibility" gani hadi kuaminiwa kuua na wasiulizwe chochote??

Hivi kwa Jeshi hili la Polisi, ambalo kuna watanzania wenzetu wengi wamepotea katika mazingira ya kutatanisha na hadi Leo hatujui waliko na Jeshi letu la Polisi lipo na linadai linaendelea na uchunguzi

Jeshi letu la Polisi limeshindwa kutuambia yuko wapi Ben.Saanane, ambaye tokea kupotea kwake ni zaidi ya miaka 2 sasa

Jeshi letu la Polisi limeshindwa kutuambia yuko wapi, Azory Gwanda, ambaye tokea kupotea kwake ni zaidi ya mwaka mmoja sasa

Jeshi letu la Polisi limeshindwa kumkamata hata mtuhiwa mmoja, kati ya wale waliojaribu kumwua kwa kumpiga risasi Mbunge wa Singida Madhariki, Mheshimiwa Tundu Lissu, zaidi ya mwaka mmoja tokea tukio hilo litokee

Vile vile nimkumbishe tu kidogo Rais Magufuli, kuhusu principle kubwa sana ya sheria inayosema kuwa A MAN CAN NOT BE A JUDGE IN HIS OWN CASE

Kwa kuwaruhusu Polisi waue kwa "kisingizio" cha kuwamaliza majambazi, maana yake ni kuwa keshawaruhisu mapolisi wawe ni mahakimu katika kesi imayowakabili wao wenyewe!

Hivi atajuaje kama Polisi ameua jambazi au amemwua raia mwema asiye na hatia kwa sababu zake binafsi??

  • Ni muhimu kila mhimili wa dola ufanye kazi zake kwa mujibu wa Katiba ya nchi unavyoelekeza

Mungu ibariki Tanzania
Unaunga mkono majambazi?
 
Sasa hivi tumeahirisha matumizi ya sheria zote kwa propaganda ya kujenga nchi. Huyu mtu anaharibu
Inabidi tuinyooshe nchi huku tukizingatia Katiba ya nchi......

Hatuwezi tukatoa kisingizio cha kuinyoosha nchi huku tukiisigina waziwazi Katiba ya nchi!
 
Siungi mkono majambazi, la hasha, ila ninachotaka uachiwe mhimili wa mahakama utoe adhabu baada ya kusikiliza ushahidi
Good,je lkn kwa nn baadhi ya watu wanapinga yanayotokea kwa Mbowe na kusingizia Serikali kuwa imeingilia Mhimili wa mahakama,je kuna ukweli wowote Mkuu?
 
Kuna nchi zina maraisi wa hovyo sana duniani.
Wanadhani kuongoza nchi ni kama kuongoza familia zao.
 
Sasa hivi tumeahirisha matumizi ya sheria zote kwa propaganda ya kujenga nchi. Huyu mtu anaharibu
Kabisa.....

Hivi unadhani kwa tukio la kutekwa mfanyibiashara maarufu kabisa nchini kwetu, Mohammed Dewji, huu sasa ni zaidi ya mwezi mmoja, hakuna mtu yeyote aliyekamatwa.......

Hivi unadhani kwa Jeshi la Polisi linalofanya "maigizo" katika shughuli zake, ndiyo liwe na "credibility" ya kusimamia kuua majambazi??
 
Time will tell
Kabisa.....

Hivi unadhani kwa tukio la kutekwa mfanyibiashara maarufu kabisa nchini kwetu, Mohammed Dewji, huu sasa ni zaidi ya mwezi mmoja, hakuna mtu yeyote aliyekamatwa.......

Hivi unadhani kwa Jeshi la Polisi linalofanya "maigizo" katika shughuli zake, ndiyo Lowe na "credibility" ya kusimamia kuua majambazi??
 
dictactors ndo wako hvo ...wanaanza kuotesha mizizi ya mauji polepole siku siyo nyingi watu wasio na hatia watauwawa kwa maelezo ya kuwa alikuwa jambazi!
 
KWA WALE AMBAO TUPO MTAANI TUNAANGAIKA NA SHIDA ZA DUNIA KATIKA HILI HATUNA CHA KUCHANGIA

ILA TUNAWAKUMBUSHA MLIOPO MAKAZINI KUNA MAISHA BAADA YA KAZI HIVYO ISHINI VIZULI NA JAMIII INAYOWAZUNGUKA KABLA YA MUDA WA KUSTAAFU HAUJAFIKA
 
Mleta mada unaleta siasa katika mambo ya msingi ya maisha ya watu. Yakikukuta utaandika uzi wenye ujumbe tofauti na huu wa sasa.
 
Kauli hiyo sio nzuri lakini sanasana inamdhalilisha yeye kama yeye mwenyewe zaidi na kuwapa sababu hao wanaoitwa wanafiki, wadhungu wafadhili wa maendeleo kwamba hana uwezo wa kusimamia utawala wa sheria au ni mtu asiyeheshimu haki za binadamu na uhuru wa mihimili mingine ya serikali anayoiongoza mwenyewe.
Mimi nina imani Jeshi la polisi haliwezi kuitekeleza kauli hiyo "wholesale" au "jumla jumla" kama anavyosema Aggrey Mwanri! kwa sababu wanajua mwisho wa siku watakaolaumiwa na watakaoadhibiwa na wananchi in their own small way; au kuwajibishwa kisheria huko mbele ya safari ni wao kama Jeshi la polisi na wala sio Magufuli.

Hili nina uhakika nalo kwa sababu hata ile siku nyingine aliwaambia maafisa wa magereza kwamba "wafungwa wafanye kazi mpaka usiku na kupigwa viboko ikibidi" hakuna gereza hata moja lililowahi kutekeleza kauli hiyo tata; I stand to be corrected! tukizingatia nguvu ya social media ingeshajulikana au kusikika, wafumgwa si ndugu zetu, tunaongea nao na wengine wanafunguliwa wanarudi kitaa!
Kwa hiyo ukiondoa polisi wachache, wachacche sana wasiojitambua, hilo halitatekelezwa kama agizo au sera labda kwa bahati mbaya au kwa mihemuko kama yule polisi wa Tarime aliyempiga kisu mdogo wake Heche! huwezi kusema ile ni sera au agizo la polisi, ni mihemuko ya muhusika kama yeye binafsi.
Polisi wetu wana mapungufu yao kama taasisi nyigine zilivyo; lakini wao sio matumbili wakutekeleza kila wanachoambiwa hovyohovyo tu!, usisahau wale ni ndugu zetu, rafiki zetu na jamaa zetu tunawajua, tunaishi nao; sio mapimbi kiasi hicho, tupunguze hof! maneno mengine Magufuli huwa anayatamka kufurahisha baraza tu, deep down siamini kama anakusudia yatekelezwe kama alivyoyasema; wholesome, na ndio maana huwa hafuatilii kama anavyofanya kwa mambo mengine! kwa sababu hata yeye anajua kwamba japo kauli ya Rais ni agizo halali lakini halina mashiko sana kisheria, linaweza kupingwa mahakamani hata kama ni the Hague kisha nchi au rais mwenyewe akaingia matatani hata baada ya kutoka madarakani.
Makaburi hufukuliwa mazee!, angalia Fredrick Chiluba wa Zambia alifia kizuizini, rais wa zamani wa Brazil Lula da Silva yuko lupango, Netanyahu wa Israel atapandishwa kizimbani soon, Mubarak wa Misri amesota lupango kwa miaka sita, Charles Taylor wa Liberia anaozea jela hadi leo, Christina de Kirchner wa Argentina anarengetwa kizimbani januari hii!
Relax mkuu.
 
Back
Top Bottom