Hivi Rais Magufuli kumuagiza Waziri wa Fedha atoe pesa shilingi bilioni mbili toka Hazina ni sahihi?

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,477
30,130
Wananchi wote tumemsikia Rais Magufuli akimuagiza waziri wa Fedha, Dkt Philipo Mpango "achote" pesa kiasi cha shilingi bilioni mbili kwenye Hazina ya Taifa, ndani ya saa 24 na awaletee wakandarasi ili zikamilishe ujenzi wa Ikulu wa Chamwino na akaendelea kumpiga mkwara mzito waziri huyo kuwa ole wake asipozileta pesa hizo atakiona!

Swali langu ninaloliuliza, hivi njia hiyo ya kumuagiza waziri wa Fedha tena hadharani mbele ya macamera ya waandishi wa habari na kuendelea kumtisha kuwa ole wake asipotoa pesa hizo hazina ni sahihi kweli?

Ninavyojua mimi ni kuwa pesa zote za hazina ni mali ya Umma na siyo mali binafsi ya Rais na hakuna mtu yeyote mwenye uwezo wa kuagiza zitoke bali Bunge la Jamhuri ya Muungano la Tanzania kwa mujibu wa Katiba ya nchi.

Ninavyojua Mimi ni kuwa Bunge halijaidhinisha pesa hizo zitoke kwa matumizi hayo ya ujenzi wa Ikulu

Hivi huyu Rais Magufuli anapata wapi kiburi cha kumwagiza waziri wa Fedha atoe hizo pesa ambazo hazijaizinishwa na Bunge la Jamhuri, ambalo linaendelea na vikao vyake hapo Dodoma?

Je, kwa kusikia wenyewe Rais Magufuli akimwagiza waziri wa Fedha "azichote" pesa hizo hazina, je ni pesa ngapi zinazotoka kwa aina hiyo ya kumwagiza waziri huyo wa Fedha?

Je, kwa "staili" hiyo ya Rais Magufuli ya kumwagiza waziri wa Fedha azitoe pesa hizo hazina tena akimtissha kuwa ole wake asipozitoa, je wananchi tutakuwa na "doubt" yoyote na ripoti ya CAG aliyepita, Profesa Assad, aliyeibua upotevu wa pesa za Umma, kwa kiasi cha shilingi trillion 1.5?
 
Mystery,

Hii coment inaaksi umri wako kuwa ni mchanga. Budget ya Ujenzi ilikwisha kasmiwa kinachoendelea sasa ni kutumia tu, na kwakuwa Rais ndiye AFISA MASUULI MKUUU alikuwa sahihi kutia saini ya Mdomo ili Hazina watoe pessa. Kikubwa aliyeeelezwa baadae atapeleka nyaraka zinasainiwa na Mhe. Rais mambo yanakuwa sawa kwa mujibu wa Sheria. Hivyo yuko sahihi,
 
Mtoa mada unaongea utafikiria huo mkutano umeangalia mwenyewe tu wakati wengi tu tumeangalia maana nakuona unavyopotosha kuhusu kumlazimisha Waziri wa fedha wakati Mzee baba pale alikuwa anatania tu nasema hivyo sababu Waziri hata siku moja hawezi mpinga bosi wake.

Na kuhusu kutoa Hela Haya mambo bwana tumeshachelewa sana haya sijui ya kusubiri bunge tutafika lini sisi nchi maskini, yani tunafata sheria za nchi ambazo hata wakikaa baada ya miezi baadae hakiaribiki kitu sisi tufanye tu maana pesa sizinaonekana zinafanya kazi ipi.

Afrika tumechelewa haya mambo ya kusubiri bunge likae tusubiri tukishaendelea huko sio sasa.

Hivi zile ajira 1000 za madaktari alizotoa papo kwa hapo Magufuli kwenye mkutano na madaktari angesubiri pia bunge likae??
 
Mystery,
Fedha ni za serikali na Ikulu ni ya serikali wala siyo CCM.So hapo sioni cha ajabu.

sema shida ni kama haikuwa kwenye mpango wa kujengwa na bajeti haikutengwa
 
Katika ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977, ibara ya 135(2) ninainukuu kama ifuatavyo "Fedha ambazo hazitawekwa kwenye mfuko Mkuu wa Hazina ya serikali ni zile zote ambazo zimetajwa na sheria kwamba zitumike kwa shughuli maalum" mwisho wa kunukuu

Sasa swali tunalojiuliza hivi pesa za ujenzi wa Makao makuu ya Chamwino hazijawekwa kwenye fungu hilo la Mfuko mkuu wa hazina ya serikali??
 
Hii coment inaaksi umri wako kuwa ni mchanga. Budget ya Ujenzi ilikwisha kasmiwa kinachoendelea sasa ni kutumia tu, na kwakuwa Rais ndiye AFISA MASUULI MKUUU alikuwa sahihi kutia saini ya Mdomo ili Hazina watoe pessa. Kikubwa aliyeeelezwa baadae atapeleka nyaraka zinasainiwa na Mhe. Rais mambo yanakuwa sawa kwa mujibu wa Sheria. Hivyo yuko sahihi
Ingekuwa vyema Rugemalira na mwenzake mhindi waachwe huru kwa kuwa Afisa Massuli Mkuu Kikwete alisema fedha za Escrow wamelipwa wenye fedha zao. Au sio?
 
35 Reactions
Reply
Back
Top Bottom