Hivi Rais analindwa na vikosi vingapi vya askari?

1. Kwanza Kuna yule amevaa Sare ya JWTZ = Mpambe wa Raisi, kawaida kutoka JWTZ

2. Kuna hawa wanavaaga SUTI huwa hawana silaha zinazoonekana = TISS kikosi cha ulinzi wa Raisi (bodyguards)

3. Kuna hawa wengine wana silaha kubwa sana sijawahi ona silaha ya vile uniforms zao zina mabaka madogo madogo = with love from Rwanda

4. Kuna hawa wengine wamevaa uniforms za kama polisi FFU = Polisi kikosi cha ulinzi wa Raisi na kudhibiti umati

5 Wa mwisho ni hawa askari wa kawaida tunakimbizana nao kila siku mtaani wanavaa kofia nyekundu kichwani = FFU Kikosi cha ulinzi wa Raisi na kudhibiti umati
Hapo vipi mzee? Kuna Warwanda bado?
 
Bonjour wana JF,

Sijui kuna mtu ameshawahi kua na swali kama langu ila akakosa majibu ya kitaalamu.

Kila nikiangalia ziara za Rais JPM huwa naona walinzi mwenye sare tofauti tofauti nikapata wazo la kufuatilia layers za walinzi wale ila sijui kazi za kila mmoja naomba nipate kujuzwa za mimi nielewe leo.

1. Kwanza kuna yule amevaa sare ya JWTZ huwa yupo na Rais bega kwa bega na hata gari huwa wanakaa moja huwa ni nani na kazi zake exactly ni zipi?

2. Kuna hawa wanavaaga SUTI huwa wanana silaha zinazoonekana sijui kama wana silaha ila huwa wamevaa vifaa vya mawasiliano katika sikio moja na wapo hadi wanawake hawa ni kina nani na wajibu wao ni upi?

3. Kuna hawa wengine wana silaha kubwa sana sijawahi ona silaha ya vile uniforms zao zina mabaka madogo madogo rangi yake kama uniform za US Army tunazoonaga kwenye movies huwa wamejaa sana weusi tii na wanaogopesha.

4. Kuna hawa wengine wamevaa uniforms za kama polisi FFU ila kofia zao ni ngumu nyeusi sio nyekundu kama zilivyo za FFU na zina mifumo ya mawasiliano direct, huwa wana machine Guns za kisasa hatari kama tunazoonaga kwenye movie nyingi za Hollywood kufuani huwa wamevalia Bullet proof vest nyeusi ikiwa na gears nyingi sana kama kamba, mabomu ya mkono, visu, Vidude vya risasi vile na vitu vingine hata sielewi ni vitu gani, vest zao kwa nyuma zimeandikwa SWAT sijui maana yake ila huwa naonaga kwenye movie pia hilo neno kwa askari wa vikosi maalum. Hawa kazi yao ni nini?

5. Wa mwisho ni hawa askari wa kawaida tunakimbizana nao kila siku mtaani wanavaa kofia nyekundu kichwani FFU na hawa wengine wanaovaa kofia za kawaida pamoja na Traffic hawa najua wajibu wao ni nini.

Kwa yeyote mwenye uelewa mzuri wa layers za kijeshi naomba kupata elimu.

Nawasiliaha

UH-60 Black Hawk


Sent from my iPhone using JamiiForums
Mambo mengine kuyaelezea humu unahitaji umakini wa hali ya juu. Hii mitandao ya kwetu huku si salama.
 
Ngoja nami nichangie machache

1,huyo mwanajeshi ambae muda wote unamuona na raisi anaitwa ADC Aide de camp,kazi yake kubwa ni kuhakikisha anamsaidia raisi kwenye shughuli zote,kama kumbebea simu na baadhi ya vitu vyake na kingine kikubwa yeye ndo mtu wa kwanza kuwa responsible pale inapotokea ambush ya haraka na yeye ndo huhusika haraka kwenye kumtorosha raisi au kumkinga na lolote mfano pale bush alipo rushiwa kiatu basi angekuwa rais wetu basi yule ADC angekidaka na kumuondoa chap mkuu eneo la tukio.

2.namba mbili ni hao wavaa suti,hao ni kikosi cha raisi ambao kazi yao kubwa ni kuhakikisha usalama wa raisi katika nyinja mbali mbali hasa kuhakikisha kuna radius(duara)ambalo watalitengeneza kuhakikisha kuwa hakuna adui anaingia ndani ya meter hizo,hvyo chunguza raisi kila atembeapo huwa kuna duara linatengenezwa na hwa jamaa kuhakikisha kuwa adui hasogei karbu na raisi na kila wanapopiga hatua ndio hapo hapo raisi nae atakanyaga.
Hawa jamaa hubeba silaha aina ya pistol ndogo kiunoni but kama utakuwa makini kila raisi akiwa ameshuka kwenye gari anatembea huwa kuna magari yanatembea yakiwa karibu nae mno,likiwemo gari lake basi yale magari mengne huwa ni maalum yamebeba silaha nzito incase limetokea tatizo basi ni kitendo cha dakika tu wanaume walishazibeba na kukinukisha.

3.Hao wanaovaa nguo za mabaka mabaka na silaha nzito hao wanaitwa energence response team hao kazi yao ni ku act haraka na kupambana na adui as soon ameact au kuonyesha dalili za kutaka ku attact na ndio wakwanza kumzunguka rais na viongozi ndani ya tukio(kumcover) wakati huo wale wengine wasuti wanachukua silaha kwenye magari ili kuunganisha nguvu,then kumtoa mkuu eneo la tukia as soon as possible huku msala mkibaki nao na hawa wa mabaka mabaka

4,ni hao unao waona kama field force hicho ni presidential force ambayo inahusika na kuweka mazingira sawa,wakati raisi akiwa bado hajafika eneo la tukio na wangine wanakuja nae,kazi yao ni kutengeneza njia ya raisi kupita na kuzuia mtu yoyote au chochote kisiwe karibu na raisi kwa umbali wa meter 10.nao pia wana act ina case kumetokea tatizo na wako vizuri sana kwenye combat kwa maana ukitaka kumkarbia raisi alafu wakakuonya ukajifanya mbishi utachezea ngumi ndani ya sekunde na watu wasijue but watashangaa tu pua znatoka dam

Pia kuna hao trafiki ambao unawaona hapo kwenye msafara,hao k
Ote ni usalama wa taifa wanakuwa wanakink moja kwa moja na kitengo,na kabla mheshimiwa hajapita eneo la tukio ni lazima lipite gari au piki piki ya ikulu kwanza kuangalia njia na waongozaji kama ndo wenyewe au kuna tofauti then ndo anatoa permission kwa msafara kusogea ikiwa other wise msafara unaweza kugeuza hata hapo hapo.

Pia mwisho tambua kuwa raisi si mtu bali raisi ni taasisi inayojitegemea na ya kipekee kushinda zote, hivyo usishangae umaambiwa kuwa kuna magufuli watatu (doubles)

I hope nmejibu tunachotakiwa kujua mengine yaache yawe classified

Sent using Jamii Forums mobile app
Point
 
1. Kwanza Kuna yule amevaa Sare ya JWTZ = Mpambe wa Raisi, kawaida kutoka JWTZ

2. Kuna hawa wanavaaga SUTI huwa hawana silaha zinazoonekana = TISS kikosi cha ulinzi wa Raisi (bodyguards)

3. Kuna hawa wengine wana silaha kubwa sana sijawahi ona silaha ya vile uniforms zao zina mabaka madogo madogo = with love from Rwanda

4. Kuna hawa wengine wamevaa uniforms za kama polisi FFU = Polisi kikosi cha ulinzi wa Raisi na kudhibiti umati

5 Wa mwisho ni hawa askari wa kawaida tunakimbizana nao kila siku mtaani wanavaa kofia nyekundu kichwani = FFU Kikosi cha ulinzi wa Raisi na kudhibiti umati
Acha uongo wewe! Watanzania hawawezi kulindwa na wanyarwanda hata siku moja. Peleka ujinga wako kule
 
Nakujibu kama ifuatavyo.

Anayevalia sare ya JWTZ ni mpambe wake kazi yake ni kumsaidia Rais kazi ndogo ndogo kama kumbebea begi, simu n.k mara nyingi utamwona akiwa nyuma ya Rais.

Wanaovalia suti ni watu wa usalama, kazi yao kubwa ni kuhakikisha Rais anakuwa salama muda wote.

Wenye silaha kubwa wanaovalia combat kama za US Army ni walinzi, kazi yao kubwa ni kuhakikisha ulinzi kwenye eneo la tukio

Askari wa FFU kazi yao kubwa ni kutuliza ghasia na Askari wanaovalia kawaida kazi yao ni kukamata waleta fujo na ghasia

Nadhani mpaka hapo nimek

Nakujibu kama ifuatavyo.

Anayevalia sare ya JWTZ ni mpambe wake kazi yake ni kumsaidia Rais kazi ndogo ndogo kama kumbebea begi, simu n.k mara nyingi utamwona akiwa nyuma ya Rais.

Wanaovalia suti ni watu wa usalama, kazi yao kubwa ni kuhakikisha Rais anakuwa salama muda wote.

Wenye silaha kubwa wanaovalia combat kama za US Army ni walinzi, kazi yao kubwa ni kuhakikisha ulinzi kwenye eneo la tukio

Askari wa FFU kazi yao kubwa ni kutuliza ghasia na Askari wanaovalia kawaida kazi yao ni kukamata waleta fujo na ghasia

Nadhani mpaka hapo nimekujibu.
Hao wenye suti kazi yao ni kumtoa raisi kwenye eneo la hatari na kumpeleka eneo salama.... Hao wenye combat kazi yao ni kujibu mapigo kwa adui anapotaka kushambulia
 
19 Reactions
Reply
Back
Top Bottom