TUJITEGEMEE
JF-Expert Member
- Nov 6, 2010
- 23,810
- 22,927
Ongeza sauti, Mkuu, Lasco Kaunda
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hahaha! Siyo Lasco mkuu, ni Racso...Ongeza sauti, Mkuu, Lasco Kaunda
Lazima tufike sehemu sasa tukubaliane na hali, kanda ya ziwa, mbeya kote, kanda ya kati na sehemu mbalimbali hizi herufi zimeshaashindikana. Tukubali tu kama vile mjerumani hawezi kusema roho anasema hoho au mtu wa india kusema wewe hawezi hata umshikie bunduki atasema veve. Au kama kiingereza cha kimarekani kilivyo tofauti kimatamshi na kiingereza cha uingereza. Kuna sehemu mpaka bbadhi ya majina yameathirika KAROLI...KALOLI,nk
Kwa kawaida, ningeweza kusema kwamba kiwango cha elimu aliyopata mtu kama huyu inawezekana kuwa elimu ya msingi.
Lakini kama mtu wa aina hiyo ni mtu aliyemaliza kidato cha nne au sita, hicho kitakuwa ni kielelezo tosha cha ubovu wa elimu yetu.
Pia kuna "ha" na "a"...... Mtu anaandika " jamaa hanakula"dah
WahandishiTatizo hili sio hapa jf tuu.yaani Wahandishi na watangazaji karibu wote kwenye tv za mitandaoni .wana tatizo hili R na L
Ninakubaliana nawe moja kwa moja...matatizo hayo yalitakiwa yashughulikiwe wakati watoto wako shule za msingi wanapoanza kujifunza kusoma na kuandika.
..wakati mwingine tuna tatizo la kutoku-aim for perfection. Mtoto akijua kuandika hata kama kwenye "r" anaandika "l" waalimu hawachukui muda kumrekebisha.
..matokeo ya utamaduni wa kulipua-lipua kazi ndiyo haya tunayoyashuhudia sasa kwamba tuna taifa la watu wasiojua kuzungumza na kuandika kwa ufasaha lugha yao ya taifa.
Mkuu tafadhali, mimi sio mshabiki wa Magufuli, lakini haimaanishi nitamponda kwenye tatizo la kibinadamu. Magufuli anakijua kiswahili vizuri hata kama sio kwa kiwango cha kupata A+, lakini anakijua. Isipokuwa anapata tatizo ya kutamka herufi fulani fulani, kutokana na herufi hizo kutokuwepo kwenye lugha aliyozungumza hasa wakati wa utotoni. Hilo ni tatizo ambalo hata awe rais wa dunia hakuna atakayemshangaa kutokuweza kuzitamka. Ingekuwa wakati wa kuandika pia anafanya kosa hilo ungekuwa na hoja lakini sio kwenye kutamka boss.
Sio r na l tu, ni kwamba Watanzania wengi hawawezi kuandika kiswahili. Huko Facebook ndio balaa kabisa, najiuliza hawa watu walimaliza vipi shule za msingi.
Mbona watu tunajifunza Kifaransa na Kihispania lugha ambazo si tu si za mama zetu, bali pia hata hazizungumzwi kwetu tulikozaliwa, na tunajitahidi kupata matamshi yanayokubalika.Kiranga kimsingi naona hapa ni kama unasaka kuibuka mshindi kwenye hili jambo. Nina maeneo mengi naweza kusaka ushindi ila sio kwenye hili. Naomba nikubali unalosema kwani sioni mtu anajifunza vipi kutamka herufi inayokataa kwenye ulimi wake. Sio kwake tu bali ni kwa walio wengi sioni wakitoboa kwenye hilo.
..kwa maoni yangu Jpm amebeba ajenda ambayo hakupaswa kuibeba.
..ajenda ya kukisambaza Kiswahili ilitakiwa ibebwe na Raisi ambaye anazungumza Kiswahili kilichonyooka.
..Na kwa attitude zetu hapa Tz, za kuendekeza uzembe-uzembe, tunaweza kufika mahali wenzetu huko nje wakawa wanatubeza kuwa tunazungumza Kiswahili kibovu.