Hivi R, L na H, ni Ugonjwa wa Taifa?

Mkuu Lugha inazungumzwa na kuandikwa pia. Tena ya kuandika ndiyo ya muhimu zaidi kwa sababu inakuwa documented (sijui Kiswahili cha hili neno, kama wajua nijuze) na hivyo kuwafia wengi zaidi wakati huo mwandishi haupo nao, japo kwa upande wa wana-habari kama radio, tv, nk hata hiyo ya kuongea, lugha fasaha ni muhimu pia.

Nilichokusudia mimi kukuambia, kupasi mtihani wa darasani sio hoja kabisa ya kuwa wewe ndio mwenye lugha, Hata mtoto wa kizungu akiingia tuition miaka miwili anaweza faulu pia.
 
Nilichokusudia mimi kukuambia, kupasi mtihani wa darasani sio hoja kabisa ya kuwa wewe ndio mwenye lugha, Hata mtoto wa kizungu akiingia tuition miaka miwili anaweza faulu pia.
Nimekuelewa sana tu mkuu. Sasa ni nini maana ya kuwa na mtihani? Nijuavyo mtihani ufanyika ili kutenganisha anayejua na asiyejua kitu fulani mfano lugha. Hivyo ikiwa mwenye lugha akafundishwa lugha yake hiyohiyo na kisha akapewa mtihani na akashindwa na mtu asiye mwenye lugha bali amefundishwa kwa muda tu ujue kuna tatizo kwa mwenye lugha.

Kwa maana nyingine ni kuwa aliyejifunza ame-jua/elewa hiyo lugha zaidi na mwenye lugha ajui lugha yake!! Ni sawa na wanaomiliki mfano magari wakati wanaogopa kuyaendesha hata baada ya kufundishwa udereva kisha wanatafuta dereva awaendeshe. Unamiliki lugha lakini ujui kuitumia kifasaha na mwisho una-fail mtihani wa lugha yako!!!, unapata wapi jeuri ya kutamba eti wewe ndiyo mwenye lugha?
 
profftobe,

Hata wewe waweza faulu mtihani wa kiengereza kuliko waengereza wenyewe, Bado Haitojaalisha kuwa wewe ndie mwenye kiengereza.
 
Hata wewe waweza faulu mtihani wa kiengereza kuliko waengereza wenyewe, Bado Haitojaalisha kuwa wewe ndie mwenye kiengereza.
Screenshot_2019-11-21-22-01-06-1.png
 
Habari Wanandugu,

Katika kitu ambacho huwa kinanishangaza katika nyakati hizi ni maandishi na matamshi ya baadhi ya herufi na silabi. Huwa najiuliza kuwa Watanzania tunakwama wapi kwenye herufi "R" na "L" kuanzia kuyaandika mpaka kutamka?

Miaka ya nyuma kulikuwa na kichaka cha kujificha kuwa kuna Makabila ambayo hayana herufi "R" kwenye lugha zao za nyumbani, hasa mikoa ya kusini (Lindi & Mtwara).

Lakini siku hizi siyo kushindwa kutamka bali yanabadilishwa kabisa. Utakuta mtu na elimu yake anakuandikia "RAKINI" badala ya "LAKINI", Eti " KALILI" badala "KARIRI", kuna muda unamsikiliza mtu mpaka unashindwa kumwelewa kama anaongea kiswahili au anatumia lugha nyingine.

Tena kuna hawa Wachungaji na Manabii ukiwaskia wakiongea ndiyo wanazikazia " L" badala ya "R". Halafu hapo bado haujahamia kwenye vyombo vya habari.

Sasa cha ajabu siwani wakiwa wanabadili matumizi ya R na L wakiwa wanazungumza Kiingereza. Kwa hiyo huu ugonjwa ni ulimbukeni uliotujaa au ni wa makusudi?


MAONI KUTOKA KWA WADAU


------------
Naenda kura nikishiba ndio nitaenda kupiga kula 🤣🤣
 
Ngoja tuache wabara wagombane hamna wanachojua hapo kweny lugha kazi kuweka ukabila mbele

Kuna moja ana masters ila meseji kama mtoto anavyoandika
 
Haiwezekani matamshi ya maneno jamii zote zikafanana

Mjerumani hata umshikie bunduki hawezi kutamka ROHO badala yake atatamka HOHO

Mhindi hata umlipue kwa bomu hawezi kusema WEWE atasema VEVE
 
Watu wanajifunza na kunyoosha lugha. Hajataka tu.

Mbona kuna wazee wengi tu wamezaliwa huko na wanaongea vizuri tu.
True story
Lugha mama sio issue

Wazee wengi wa zamani waliosoma are very eloquent actually

Mi naona ni watu hawajui tu kusoma na kuandika
Hawakuzingatia shuleni
Na hawasomi vitabu ili kutajirisha/enrich ufahamu wa maneno na misamiati

Mtu akikosea tu l na r sijui aniambie nini nimuone kama ni mtu serious

Cause how cant you comprehend something so basic; Grade 7 comprehension

Wengi ukifatilia hawana 'attention to details' na ufahamu wao una walakini fulani

Angalia taarifa na makala wanazoandika..utakutana na makosa mengine ambayo mtu makini unatakiwa uyaone
 
Watu wanajifunza na kunyoosha lugha. Hajataka tu.

Mbona kuna wazee wengi tu wamezaliwa huko na wanaongea vizuri tu.
Siku hizi ni tatizo la kuiga/ulimbukeni, zamani waandishi na watangazaji wa vyombo vya habari kutoka sehemu mbalimbali za nchi hii walikuwa hawafanyi makosa hayo, siku hizi wanaiga kama anayeharibu ni maarufu au msomi.
 
Habari Wanandugu,

Katika kitunawasumbiuwa kinanishangaza katika nyakati hizi ni maandishi na matamshi ya baadhi ya herufi na silabi. Huwa najiuliza kuwa Watanzania tunakwama wapi kwenye herufi "R" na "L" kuanzia kuyaandika mpaka kutamka?

Miaka ya nyuma kulikuwa na kichaka cha kujificha kuwa kuna Makabila ambayo hayana herufi "R" kwenye lugha zao za nyumbani, hasa mikoa ya kusini (Lindi & Mtwara).

Lakini siku hizi siyo kushindwa kutamka bali yanabadilishwa kabisa. Utakuta mtu na elimu yake anakuandikia "RAKINI" badala ya "LAKINI", Eti " KALILI" badala "KARIRI", kuna muda unamsikiliza mtu mpaka unashindwa kumwelewa kama anaongea kiswahili au anatumia lugha nyingine.

Tena kuna hawa Wachungaji na Manabii ukiwaskia wakiongea ndiyo wanazikazia " L" badala ya "R". Halafu hapo bado haujahamia kwenye vyombo vya habari.

Sasa cha ajabu siwani wakiwa wanabadili matumizi ya R na L wakiwa wanazungumza Kiingereza. Kwa hiyo huu ugonjwa ni ulimbukeni uliotujaa au ni wa makusudi?


MAONI KUTOKA KWA WADAU


------------
Ni ushamba fulani hivi ambao unawasumbua wengi
 
Habari Wanandugu,

Katika kitu ambacho huwa kinanishangaza katika nyakati hizi ni maandishi na matamshi ya baadhi ya herufi na silabi. Huwa najiuliza kuwa Watanzania tunakwama wapi kwenye herufi "R" na "L" kuanzia kuyaandika mpaka kutamka?

Miaka ya nyuma kulikuwa na kichaka cha kujificha kuwa kuna Makabila ambayo hayana herufi "R" kwenye lugha zao za nyumbani, hasa mikoa ya kusini (Lindi & Mtwara).

Lakini siku hizi siyo kushindwa kutamka bali yanabadilishwa kabisa. Utakuta mtu na elimu yake anakuandikia "RAKINI" badala ya "LAKINI", Eti " KALILI" badala "KARIRI", kuna muda unamsikiliza mtu mpaka unashindwa kumwelewa kama anaongea kiswahili au anatumia lugha nyingine.

Tena kuna hawa Wachungaji na Manabii ukiwaskia wakiongea ndiyo wanazikazia " L" badala ya "R". Halafu hapo bado haujahamia kwenye vyombo vya habari.

Sasa cha ajabu siwani wakiwa wanabadili matumizi ya R na L wakiwa wanazungumza Kiingereza. Kwa hiyo huu ugonjwa ni ulimbukeni uliotujaa au ni wa makusudi?


MAONI KUTOKA KWA WADAU


------------
Kushindwa kutamka baadhi ya herufi za lugha ya Kiswahili kwa usahihi kunasababishwa na athari ya lugha ya kwanza ya mtu. Hilo ni tatizo linaloweza kurekebishwa iwapo mtu husika atapelekwa kwenye maabara ya sauti na kusaidiwa kurekebisha kasoro hiyo chini ya tawi la fonetiki liitwalo fonetiki matamshi.
 
Back
Top Bottom