Napenda nielemishwe kwa hili. Sheria zetu zinazuia mtu kujichukulia sheria mkononi. Lakini mara nyingi nimekuwa nikisikia polisi kujichukulia sheria mkononi hasa kuua raia kwa kuwadhania kuwa ni wahalifu. Mfano, huko Arusha kuna taksi dreva ameripotiwa na vyombo vya habari kuwa aliuawa na polisi katika mazingira ya kutatanisha (hakuwa na silaha).
Huko Mbeya polisi anadaiwa kumwua kichaa kwa kumpiga risasi kichwani. Hapa Dar es Salaam (huko Kimara) dreva teksi anadaiwa kuawa na polisi kwa kupigwa risasi akiwa ndani ya gari baada ya kuamriwa kusimama.
Hivi karibuni waandishi wa habari walitishiwa kwa bastola na polisi walipokuwa wakifuatilia tukio fulani huko Morogoro.
Je, hii sheria ya kujichukulia sheria mkononi haiwahusu polisi na je, polisi akishamhisi mtu kuwa ni mhalifu tayari anaruhusiwa kuua? Huu ndo utawala bora?
Nimeona niyaseme haya kwa sababu naogopa mauaji ya namna hii yatakuwa yakiendelea na raia tutakuwa tunaendelea kukosa ulinzi wa polisi kwani badala ya kulinda maisha yetu na mali zetu wanaanza kutumaliza mmojammoja kwa kuhisi tu kuwa fulani anahusika kwenye uhalifu.
Pia ni lini polisi anaruhusiwa kuua na lini anaruhusiwa kujeruhi tu ili kufanikisha kumkamata mtu anahehisiwa kuwa mhalifu na anayekimbia au kukataa kukamatwa lakini hana silaha yoyote? Huu ugonjwa wa kuua watu kwa risasi utaendelea hadi lini?
Pili kuna kitu kingine kina kera. Kuna baadhi eti ni askari wastaafu na wana bastola. Sasa wakiwa baa na wakibishana kidogo (kwa maneno) na wanywaji wengine wanatoa bastola na kutishia kuua. Na wengine hata kabla ya kuulizwa wanajitangaza kuwa ni moto wa kuotea mbali na ukibisha kidogo kinatolewa cha moto. Sasa hii tabia inatoka wapi jamani Watz wenzangu? Hivi tumechokana kiasi hicho hata hatuthamini tena uhai wa wenzetu?
Huko Mbeya polisi anadaiwa kumwua kichaa kwa kumpiga risasi kichwani. Hapa Dar es Salaam (huko Kimara) dreva teksi anadaiwa kuawa na polisi kwa kupigwa risasi akiwa ndani ya gari baada ya kuamriwa kusimama.
Hivi karibuni waandishi wa habari walitishiwa kwa bastola na polisi walipokuwa wakifuatilia tukio fulani huko Morogoro.
Je, hii sheria ya kujichukulia sheria mkononi haiwahusu polisi na je, polisi akishamhisi mtu kuwa ni mhalifu tayari anaruhusiwa kuua? Huu ndo utawala bora?
Nimeona niyaseme haya kwa sababu naogopa mauaji ya namna hii yatakuwa yakiendelea na raia tutakuwa tunaendelea kukosa ulinzi wa polisi kwani badala ya kulinda maisha yetu na mali zetu wanaanza kutumaliza mmojammoja kwa kuhisi tu kuwa fulani anahusika kwenye uhalifu.
Pia ni lini polisi anaruhusiwa kuua na lini anaruhusiwa kujeruhi tu ili kufanikisha kumkamata mtu anahehisiwa kuwa mhalifu na anayekimbia au kukataa kukamatwa lakini hana silaha yoyote? Huu ugonjwa wa kuua watu kwa risasi utaendelea hadi lini?
Pili kuna kitu kingine kina kera. Kuna baadhi eti ni askari wastaafu na wana bastola. Sasa wakiwa baa na wakibishana kidogo (kwa maneno) na wanywaji wengine wanatoa bastola na kutishia kuua. Na wengine hata kabla ya kuulizwa wanajitangaza kuwa ni moto wa kuotea mbali na ukibisha kidogo kinatolewa cha moto. Sasa hii tabia inatoka wapi jamani Watz wenzangu? Hivi tumechokana kiasi hicho hata hatuthamini tena uhai wa wenzetu?