Return Of Undertaker
JF-Expert Member
- Jun 12, 2012
- 4,572
- 26,867
Anaandika Thadei Ole Mushi (mmoja ya wanaCCM wachache wenye akili nyingi).!
______________________________________
POLIS WANAKIMBIZANA NA MADUMU YA PETROLI SASA HIVI.
Na Thadei Ole Mushi
Hakuna Nchi ambayo haipatagi majanga, hata Marekani na ubora wake hupata majanga ila kwa nia ya kuimarisha Jeshi langu la polisi tuzungumze kidogo.
Si Mara moja tunewahi kusikia mikutano ya wapinzani ikizuiwa kwa kile kinachoitwa taarifa za Kiitelejensia kuwafikia kuwa kutakuwa na kiashiria cha uvunjifu wa amani.
Si Mara Moja kwa Jeshi letu la polisi kufika kwa mbwembwe kuwakata waandamani kwenye mabango muda mchache tu baada ya naandamano kuanza huku wakiwa na mabomu, manati na mitutu ya Bunduki.
Twende sawa hapa
Siwalaumu polisi moja kwa moja ila tuangalie mazingira ya utokeaji wa tukio hili. Rafiki yangu mmoja kaniambia kuwa kuna haja ya kutafakari namna ya kunyambulisha majanga. Matanker ya mafuta na kemikali zenye sumu ni majanga yanayotembea.
Nilitegemea baada ya tanker kuanguka
1.Polisi wangefika mara moja na kuweka riboni kuzuia mtu yetote kuingia eneo hilo.
2.Yale magari ya washawasha yangekuwa stand by kufanya ile kazi yake maarufu ya kutawanya mikusanyiko haramu kama huu wa wizi wa mafuta.
3.Wakati huo huo fire brigade wangekuwa alerted wasogee karibu.
Ni kwa nini?hata bila kuchomoa betri bado kulikuwa na possibility kubwa kutokea moto .
kwamba gari lenye lita 36,000 linaunguka maeneo yenye mkusanyiko wa Watu kama Msamvu, Kilomita chache kutoka iliko fire brigade na makao makuu ya Polisi na hakuna kilichofanyika ni bahati mbaya sana.
Wakati tunakazana kulaumu wananchi kwa kutokuwa na elimu stahiki janga hili ni vema tuanze pia na wale wanaotumia kodi zetu na kutotaka kuzuia hali kama hii isitokee.
Siwalaumu Polisi.
Nimetoa hii kwa lengo la kujifunza, ila wanaotakiwa kujifunza zaidi ni Jeshi letu la polisi lenye jukumu la kulinda RAIA na Mali zao. Wa pili kujifunza ni wananchi wangelipaswa kutoa taarifa Polisi badala ya kufakamia petroli kwenye madumu yao.
Ukiangalia video nyingi za tukio hili ni kwamba kabla ya kulipuka watu walijichotea mafuta kwa takribani dakika 45 hadi lisaa kabla ya wanayemtumu kuwa teja kuja kutaka kuchomoka na Betri iliyosababisha mafuta kulipuka. Muda huo ni mkubwa sana kwa watu kufanya uhalifu.
Je tumejuandaaje kukabiliana na majanga kama haya? Je tupo tayari kiasi gani?
TUJIFUNZE.
OLE MUSHI
0712702602.
______________________________________
POLIS WANAKIMBIZANA NA MADUMU YA PETROLI SASA HIVI.
Na Thadei Ole Mushi
Hakuna Nchi ambayo haipatagi majanga, hata Marekani na ubora wake hupata majanga ila kwa nia ya kuimarisha Jeshi langu la polisi tuzungumze kidogo.
Si Mara moja tunewahi kusikia mikutano ya wapinzani ikizuiwa kwa kile kinachoitwa taarifa za Kiitelejensia kuwafikia kuwa kutakuwa na kiashiria cha uvunjifu wa amani.
Si Mara Moja kwa Jeshi letu la polisi kufika kwa mbwembwe kuwakata waandamani kwenye mabango muda mchache tu baada ya naandamano kuanza huku wakiwa na mabomu, manati na mitutu ya Bunduki.
Twende sawa hapa
Siwalaumu polisi moja kwa moja ila tuangalie mazingira ya utokeaji wa tukio hili. Rafiki yangu mmoja kaniambia kuwa kuna haja ya kutafakari namna ya kunyambulisha majanga. Matanker ya mafuta na kemikali zenye sumu ni majanga yanayotembea.
Nilitegemea baada ya tanker kuanguka
1.Polisi wangefika mara moja na kuweka riboni kuzuia mtu yetote kuingia eneo hilo.
2.Yale magari ya washawasha yangekuwa stand by kufanya ile kazi yake maarufu ya kutawanya mikusanyiko haramu kama huu wa wizi wa mafuta.
3.Wakati huo huo fire brigade wangekuwa alerted wasogee karibu.
Ni kwa nini?hata bila kuchomoa betri bado kulikuwa na possibility kubwa kutokea moto .
kwamba gari lenye lita 36,000 linaunguka maeneo yenye mkusanyiko wa Watu kama Msamvu, Kilomita chache kutoka iliko fire brigade na makao makuu ya Polisi na hakuna kilichofanyika ni bahati mbaya sana.
Wakati tunakazana kulaumu wananchi kwa kutokuwa na elimu stahiki janga hili ni vema tuanze pia na wale wanaotumia kodi zetu na kutotaka kuzuia hali kama hii isitokee.
Siwalaumu Polisi.
Nimetoa hii kwa lengo la kujifunza, ila wanaotakiwa kujifunza zaidi ni Jeshi letu la polisi lenye jukumu la kulinda RAIA na Mali zao. Wa pili kujifunza ni wananchi wangelipaswa kutoa taarifa Polisi badala ya kufakamia petroli kwenye madumu yao.
Ukiangalia video nyingi za tukio hili ni kwamba kabla ya kulipuka watu walijichotea mafuta kwa takribani dakika 45 hadi lisaa kabla ya wanayemtumu kuwa teja kuja kutaka kuchomoka na Betri iliyosababisha mafuta kulipuka. Muda huo ni mkubwa sana kwa watu kufanya uhalifu.
Je tumejuandaaje kukabiliana na majanga kama haya? Je tupo tayari kiasi gani?
TUJIFUNZE.
OLE MUSHI
0712702602.