Hivi Polisi wa Morogoro ingekuwa CHADEMA wanataka kuandamana Itigi ingetumika intelejensia, lori la mafuta dk 45 mmelala tu

Return Of Undertaker

JF-Expert Member
Jun 12, 2012
4,572
26,867
Anaandika Thadei Ole Mushi (mmoja ya wanaCCM wachache wenye akili nyingi).!
______________________________________
POLIS WANAKIMBIZANA NA MADUMU YA PETROLI SASA HIVI.

Na Thadei Ole Mushi

Hakuna Nchi ambayo haipatagi majanga, hata Marekani na ubora wake hupata majanga ila kwa nia ya kuimarisha Jeshi langu la polisi tuzungumze kidogo.

Si Mara moja tunewahi kusikia mikutano ya wapinzani ikizuiwa kwa kile kinachoitwa taarifa za Kiitelejensia kuwafikia kuwa kutakuwa na kiashiria cha uvunjifu wa amani.

Si Mara Moja kwa Jeshi letu la polisi kufika kwa mbwembwe kuwakata waandamani kwenye mabango muda mchache tu baada ya naandamano kuanza huku wakiwa na mabomu, manati na mitutu ya Bunduki.

Twende sawa hapa

Siwalaumu polisi moja kwa moja ila tuangalie mazingira ya utokeaji wa tukio hili. Rafiki yangu mmoja kaniambia kuwa kuna haja ya kutafakari namna ya kunyambulisha majanga. Matanker ya mafuta na kemikali zenye sumu ni majanga yanayotembea.

Nilitegemea baada ya tanker kuanguka
1.Polisi wangefika mara moja na kuweka riboni kuzuia mtu yetote kuingia eneo hilo.

2.Yale magari ya washawasha yangekuwa stand by kufanya ile kazi yake maarufu ya kutawanya mikusanyiko haramu kama huu wa wizi wa mafuta.

3.Wakati huo huo fire brigade wangekuwa alerted wasogee karibu.

Ni kwa nini?hata bila kuchomoa betri bado kulikuwa na possibility kubwa kutokea moto .
kwamba gari lenye lita 36,000 linaunguka maeneo yenye mkusanyiko wa Watu kama Msamvu, Kilomita chache kutoka iliko fire brigade na makao makuu ya Polisi na hakuna kilichofanyika ni bahati mbaya sana.

Wakati tunakazana kulaumu wananchi kwa kutokuwa na elimu stahiki janga hili ni vema tuanze pia na wale wanaotumia kodi zetu na kutotaka kuzuia hali kama hii isitokee.

Siwalaumu Polisi.

Nimetoa hii kwa lengo la kujifunza, ila wanaotakiwa kujifunza zaidi ni Jeshi letu la polisi lenye jukumu la kulinda RAIA na Mali zao. Wa pili kujifunza ni wananchi wangelipaswa kutoa taarifa Polisi badala ya kufakamia petroli kwenye madumu yao.

Ukiangalia video nyingi za tukio hili ni kwamba kabla ya kulipuka watu walijichotea mafuta kwa takribani dakika 45 hadi lisaa kabla ya wanayemtumu kuwa teja kuja kutaka kuchomoka na Betri iliyosababisha mafuta kulipuka. Muda huo ni mkubwa sana kwa watu kufanya uhalifu.

Je tumejuandaaje kukabiliana na majanga kama haya? Je tupo tayari kiasi gani?

TUJIFUNZE.

OLE MUSHI
0712702602.
 
Ukiwaza sana unaweza ukawapiga polisi mawe..washenzi sana.

Siamini kama polisi walizidiwa nguvu labda na wananchi, nachoamini ni uzembe mkubwa sana ulifanywa na polisi waliokuwepo eneo hilo,maana hapo msanvu tu geti la kutokea huwa wapo.

Anyway, hebu ngoja tusitiri kwanza hawa wapendwa wetu kisha tuanze kuulizana vizuri.
 
Polisi wana makosa zaidi.raia wana makosa ila sio kama ya polisi.Dk 45 bado hawajaja.Lakin Tanzania sijui shida iko wapi maana kila mwaka matukio kama haya yanatokea na.polisi+zimamoto wanachelewa.Yani kila mwaka.sasa nidhamu ya jeshi iko wapi?je,ukitokea ugaidi na watu wakatekwa ndani mfano m city pale polisi itawachukua masaa mangapi kusogeza pua?au mpaka wazee wa mabaka ndo wafanye mambo sensitive?

MI nashauri kiundwe kikosi kazi cha kupambana na maafa kama vile ugaidi,moto,ajali za majini,ajali za ndege nk.na wapewe helicopter ambazo zitakuwa standby muda wote na magali ya kisasa ambayo yatakuwa standby.Na cha zaidi ni kwamba kikosi maalum hicho kiwe chini ya JWTZ kisiwe chini ya JKT.
 
Maandamano yana taarifa kuwa siku fulani yatatokea ndio maana ni rahisi polisi kujiandaa ila ni lini na wapi uliwahi kuona ajali ina taarifa kuwa itatokea? Acheni kutafuta wa kumtupia lawama huku mkijiua kabisa walioathirika na tukio ndio walikuwa wazembe na wajinga kama sio wapumbavu. Unafanya mchezo na maisha yako mwenyewe kwa kutegemea polisi atakuja kukuokoa. Ni upuuzi wa hali ya juu.
 
Anaandika Thadei Ole Mushi (mmoja ya wanaCCM wachache wenye akili nyingi).!
______________________________________
POLIS WANAKIMBIZANA NA MADUMU YA PETROLI SASA HIVI.

Na Thadei Ole Mushi

Hakuna Nchi ambayo haipatagi majanga, hata Marekani na ubora wake hupata majanga ila kwa nia ya kuimarisha Jeshi langu la polisi tuzungumze kidogo.

Si Mara moja tunewahi kusikia mikutano ya wapinzani ikizuiwa kwa kile kinachoitwa taarifa za Kiitelejensia kuwafikia kuwa kutakuwa na kiashiria cha uvunjifu wa amani.

Si Mara Moja kwa Jeshi letu la polisi kufika kwa mbwembwe kuwakata waandamani kwenye mabango muda mchache tu baada ya naandamano kuanza huku wakiwa na mabomu, manati na mitutu ya Bunduki.

Twende sawa hapa

Siwalaumu polisi moja kwa moja ila tuangalie mazingira ya utokeaji wa tukio hili. Rafiki yangu mmoja kaniambia kuwa kuna haja ya kutafakari namna ya kunyambulisha majanga. Matanker ya mafuta na kemikali zenye sumu ni majanga yanayotembea.

Nilitegemea baada ya tanker kuanguka
1.Polisi wangefika mara moja na kuweka riboni kuzuia mtu yetote kuingia eneo hilo.

2.Yale magari ya washawasha yangekuwa stand by kufanya ile kazi yake maarufu ya kutawanya mikusanyiko haramu kama huu wa wizi wa mafuta.

3.Wakati huo huo fire brigade wangekuwa alerted wasogee karibu.

Ni kwa nini?hata bila kuchomoa betri bado kulikuwa na possibility kubwa kutokea moto .
kwamba gari lenye lita 36,000 linaunguka maeneo yenye mkusanyiko wa Watu kama Msamvu, Kilomita chache kutoka iliko fire brigade na makao makuu ya Polisi na hakuna kilichofanyika ni bahati mbaya sana.

Wakati tunakazana kulaumu wananchi kwa kutokuwa na elimu stahiki janga hili ni vema tuanze pia na wale wanaotumia kodi zetu na kutotaka kuzuia hali kama hii isitokee.

Siwalaumu Polisi.

Nimetoa hii kwa lengo la kujifunza, ila wanaotakiwa kujifunza zaidi ni Jeshi letu la polisi lenye jukumu la kulinda RAIA na Mali zao. Wa pili kujifunza ni wananchi wangelipaswa kutoa taarifa Polisi badala ya kufakamia petroli kwenye madumu yao.

Ukiangalia video nyingi za tukio hili ni kwamba kabla ya kulipuka watu walijichotea mafuta kwa takribani dakika 45 hadi lisaa kabla ya wanayemtumu kuwa teja kuja kutaka kuchomoka na Betri iliyosababisha mafuta kulipuka. Muda huo ni mkubwa sana kwa watu kufanya uhalifu.

Je tumejuandaaje kukabiliana na majanga kama haya? Je tupo tayari kiasi gani?

TUJIFUNZE.

OLE MUSHI
0712702602.
Police hawanakosa hao jamaa walisitahili kabisa kufa.
 
Anaandika Thadei Ole Mushi (mmoja ya wanaCCM wachache wenye akili nyingi).!
______________________________________
POLIS WANAKIMBIZANA NA MADUMU YA PETROLI SASA HIVI.

Na Thadei Ole Mushi

Hakuna Nchi ambayo haipatagi majanga, hata Marekani na ubora wake hupata majanga ila kwa nia ya kuimarisha Jeshi langu la polisi tuzungumze kidogo.

Si Mara moja tunewahi kusikia mikutano ya wapinzani ikizuiwa kwa kile kinachoitwa taarifa za Kiitelejensia kuwafikia kuwa kutakuwa na kiashiria cha uvunjifu wa amani.

Si Mara Moja kwa Jeshi letu la polisi kufika kwa mbwembwe kuwakata waandamani kwenye mabango muda mchache tu baada ya naandamano kuanza huku wakiwa na mabomu, manati na mitutu ya Bunduki.

Twende sawa hapa

Siwalaumu polisi moja kwa moja ila tuangalie mazingira ya utokeaji wa tukio hili. Rafiki yangu mmoja kaniambia kuwa kuna haja ya kutafakari namna ya kunyambulisha majanga. Matanker ya mafuta na kemikali zenye sumu ni majanga yanayotembea.

Nilitegemea baada ya tanker kuanguka
1.Polisi wangefika mara moja na kuweka riboni kuzuia mtu yetote kuingia eneo hilo.

2.Yale magari ya washawasha yangekuwa stand by kufanya ile kazi yake maarufu ya kutawanya mikusanyiko haramu kama huu wa wizi wa mafuta.

3.Wakati huo huo fire brigade wangekuwa alerted wasogee karibu.

Ni kwa nini?hata bila kuchomoa betri bado kulikuwa na possibility kubwa kutokea moto .
kwamba gari lenye lita 36,000 linaunguka maeneo yenye mkusanyiko wa Watu kama Msamvu, Kilomita chache kutoka iliko fire brigade na makao makuu ya Polisi na hakuna kilichofanyika ni bahati mbaya sana.

Wakati tunakazana kulaumu wananchi kwa kutokuwa na elimu stahiki janga hili ni vema tuanze pia na wale wanaotumia kodi zetu na kutotaka kuzuia hali kama hii isitokee.

Siwalaumu Polisi.

Nimetoa hii kwa lengo la kujifunza, ila wanaotakiwa kujifunza zaidi ni Jeshi letu la polisi lenye jukumu la kulinda RAIA na Mali zao. Wa pili kujifunza ni wananchi wangelipaswa kutoa taarifa Polisi badala ya kufakamia petroli kwenye madumu yao.

Ukiangalia video nyingi za tukio hili ni kwamba kabla ya kulipuka watu walijichotea mafuta kwa takribani dakika 45 hadi lisaa kabla ya wanayemtumu kuwa teja kuja kutaka kuchomoka na Betri iliyosababisha mafuta kulipuka. Muda huo ni mkubwa sana kwa watu kufanya uhalifu.

Je tumejuandaaje kukabiliana na majanga kama haya? Je tupo tayari kiasi gani?

TUJIFUNZE.

OLE MUSHI
0712702602.
Vipi ameshatoa pole na rambirambi
 
28 Reactions
Reply
Back
Top Bottom