Kiraka
JF-Expert Member
- Feb 1, 2010
- 3,834
- 3,076
Nimekuwa nikiangalia taarifa za habari na magazeti na ni mara chache sana utaona watu waliokamatwa kwa makosa mbali mbali kuonyeshwa picha zao kwenye runinga, au picha kwenye magazeti.
Je kuna sheria yoyote inazuia hili, hatusemi kuwa wamehukumiwa na makosa lakini kwani si ni kweli wamekamatwa kuna tatizo gani kuonyesha picha zao?
Nikilinganisha na nchi za Ulaya au hata Kenya wao huwa wanaonyesha habari kama ilivyo, lakini sisi utakuta mara nyingi Wakuu wa polisi wakiwa na marundo ya risasi au vitu vya wizi wakionyesha kuthibitisha kutokea kwa tukio, lakini kamwe hawata onyesha picha za waliokamatwa. Je kwa kufanya hivi hawaoni kuwa hata wanaongeza bure muda wa kufanya upelelezi , kwani pengine wangeonyesha hao waharifu labda wangepata watu kuwasaidia katika upelelezi au kupata taarifa zaidi za matukio mengine.
Naoma ufafanuzi wa kisheria kama kuna sheria inazuia hili maana mimi sioni sababu ya kuficha sura za watu waliokamatwa na makosa mbali mbali kwani wangesaidia sana sisi raia kuweza kujilinda, inawezekana kabisa tunaishi na majambazi yanakamatwa katika matukio lakini kwakuwa hawaonyeshwi basi hatujui na tunaendelea kuishi nao bila kuchukua tahadhari yoyote.
Je kuna sheria yoyote inazuia hili, hatusemi kuwa wamehukumiwa na makosa lakini kwani si ni kweli wamekamatwa kuna tatizo gani kuonyesha picha zao?
Nikilinganisha na nchi za Ulaya au hata Kenya wao huwa wanaonyesha habari kama ilivyo, lakini sisi utakuta mara nyingi Wakuu wa polisi wakiwa na marundo ya risasi au vitu vya wizi wakionyesha kuthibitisha kutokea kwa tukio, lakini kamwe hawata onyesha picha za waliokamatwa. Je kwa kufanya hivi hawaoni kuwa hata wanaongeza bure muda wa kufanya upelelezi , kwani pengine wangeonyesha hao waharifu labda wangepata watu kuwasaidia katika upelelezi au kupata taarifa zaidi za matukio mengine.
Naoma ufafanuzi wa kisheria kama kuna sheria inazuia hili maana mimi sioni sababu ya kuficha sura za watu waliokamatwa na makosa mbali mbali kwani wangesaidia sana sisi raia kuweza kujilinda, inawezekana kabisa tunaishi na majambazi yanakamatwa katika matukio lakini kwakuwa hawaonyeshwi basi hatujui na tunaendelea kuishi nao bila kuchukua tahadhari yoyote.