mama D
JF-Expert Member
- Nov 22, 2010
- 19,760
- 35,205
Nilisikitishwa sana na hili tukio lililomkuta kaka Sindato kwa kweli!
Na hii sio kwa Sindato tuu. Inatokea kwa watu wengi wanaume kwa wanawake. Unakuta watu wameshashindwana na kuamua kuachana lakini mmoja wao anapoamua kuingia kwenye mahusiano mengine inakua vita.
Tena wengine wanafikia hatua ya kuuana ili mradi mtu asiwe na mwenza mwingine.
Binafsi naamini ndoa ni maisha mazuri yenye kumpendeza Mungu na watu wanaotuzunguka; na zaidi naamini ndoa ni upendo Kati wa mwanaume na mwanamke. Naamini kabisa kama hakuna upendo basi hakuna ndoa, zaidi kutakua na uadui Kati marafiki waliogeuka kuwa maadui. Na hii ndio inapelekea kwenye Ile hatari ya watu kuuana na kuumizana.
Ifike mahala waoaji na waolewaji watambue kwamba kuoana na mtu haimaanishi kwamba hata upendo unapokua umeisha wewe utaendelea kummiliki, kumnyima haki yake ya kuishi na kumiliki vitu vingine na maisha mengine.
Yaani hawa watu wametengana nikiwa mdogo sana, hapo wanasema 18 years lakini kiuhalisia ni zaidi ya hiyo miaka. Sema hiyo 18 ndio yenye ushahidi wa utengano wao.
Wote ni waelewa, sheria ya ndoa ya dini yao wanaijua, sheria ya ndoa ya nchi wanaijua, wanajua kabisa hadi hiyo miaka ndoa ilishakua batili. Sasa sijui nia yao sasa ni kukomoana au kutaabishana tu.
Na hii sio kwa Sindato tuu. Inatokea kwa watu wengi wanaume kwa wanawake. Unakuta watu wameshashindwana na kuamua kuachana lakini mmoja wao anapoamua kuingia kwenye mahusiano mengine inakua vita.
Tena wengine wanafikia hatua ya kuuana ili mradi mtu asiwe na mwenza mwingine.
Binafsi naamini ndoa ni maisha mazuri yenye kumpendeza Mungu na watu wanaotuzunguka; na zaidi naamini ndoa ni upendo Kati wa mwanaume na mwanamke. Naamini kabisa kama hakuna upendo basi hakuna ndoa, zaidi kutakua na uadui Kati marafiki waliogeuka kuwa maadui. Na hii ndio inapelekea kwenye Ile hatari ya watu kuuana na kuumizana.
Ifike mahala waoaji na waolewaji watambue kwamba kuoana na mtu haimaanishi kwamba hata upendo unapokua umeisha wewe utaendelea kummiliki, kumnyima haki yake ya kuishi na kumiliki vitu vingine na maisha mengine.
Yaani hawa watu wametengana nikiwa mdogo sana, hapo wanasema 18 years lakini kiuhalisia ni zaidi ya hiyo miaka. Sema hiyo 18 ndio yenye ushahidi wa utengano wao.
Wote ni waelewa, sheria ya ndoa ya dini yao wanaijua, sheria ya ndoa ya nchi wanaijua, wanajua kabisa hadi hiyo miaka ndoa ilishakua batili. Sasa sijui nia yao sasa ni kukomoana au kutaabishana tu.