Wakuu mimi nina mke na nina watoto na mke wangu. Pia nina mwanamke mwingine nilizaa naye. Mkipitia nyuzi zangu za nyuma nilishalileta kwenu hili swala, na mlinishauri vizuri tu.
Kwa kukumbushia kwa wale ambao hawakusoma uzi wangu, ni kwamba huyu sijui nimuite mchepuko, japo huwa sijisikii vizuri kumwita mchepuko maana ni mama wa mwanangu, nimedumu naye kwa miaka minne. Mwaka jana niligundua anatoka na mwanaume mwingine nikaamua kuachana naye.
Nikahamishia mapenzi yote kwa wife. Furaha ndani ya ndoa ikarudi. Wife akawa ni mtu mwenye furaha sana. Miezi minne baada ya kumwacha huyu mzazi mwenzangu alinitafuta. Aliniomba msamaha na kuniomba turudiane. Alinielezea jinsi alivyotendwa na jamaa. Japo nilikuwa mzito kukubali kumrudia nikikumbuka maumivu aliyonisababishia, ila baada ya kufikiria vizuri, na kukumbuka tulikotoka nikaona acha tu nipashe kiporo, isitoshe pia nina mke hivyo haina haja ya kumuonea wivu mwanamke ambaye sio mke wangu.
Tumeendelea kuwa pamoja kwa muda wa miezi saba hivi tokea turudiane japo migogoro ya hapa na pale imekuwa ikijitokeza. Hivi karibuni huyu mwanamke ameanza tabia ya kukataa kufanya mapenzi. Mnaweza kupanga siku flani mkutane mfanye yenu lakini siku ikifika analeta visingizio.
Hali hii imepelekea niamue kuachana naye japo kiuhalisia naona yeye ndio ameamua kuniacha, maana kama hataki kufanya mapenzi anategemea nini. Kwa hiyo nimekata shauri nimwache tu maana naona kama nimekuwa mtumwa wa mapenzi, nimekuwa mtu wa kumbembeleza kila mara ili tufanye mapenzi ila yeye hata hajali. Tatizo roho inaniuma kweli, akili haifanyi kazi kabisa, najihisi nimepata msongo wa mawazo. Hamu ya kula sina na kila kitu naona hakiendi kabisa.
Najitahidi kuchangamka humu ndani ili wife asihisi kama kuna kitu kinanisumbua. Wanaume wenzangu, hivi hali hii ya kuzama kwenye penzi la mzazi mwenzako inakuwaje? Naomba mnishauri namna nzuri ya kusonga na maisha, mwenzenu napata tabu.
Kwa kukumbushia kwa wale ambao hawakusoma uzi wangu, ni kwamba huyu sijui nimuite mchepuko, japo huwa sijisikii vizuri kumwita mchepuko maana ni mama wa mwanangu, nimedumu naye kwa miaka minne. Mwaka jana niligundua anatoka na mwanaume mwingine nikaamua kuachana naye.
Nikahamishia mapenzi yote kwa wife. Furaha ndani ya ndoa ikarudi. Wife akawa ni mtu mwenye furaha sana. Miezi minne baada ya kumwacha huyu mzazi mwenzangu alinitafuta. Aliniomba msamaha na kuniomba turudiane. Alinielezea jinsi alivyotendwa na jamaa. Japo nilikuwa mzito kukubali kumrudia nikikumbuka maumivu aliyonisababishia, ila baada ya kufikiria vizuri, na kukumbuka tulikotoka nikaona acha tu nipashe kiporo, isitoshe pia nina mke hivyo haina haja ya kumuonea wivu mwanamke ambaye sio mke wangu.
Tumeendelea kuwa pamoja kwa muda wa miezi saba hivi tokea turudiane japo migogoro ya hapa na pale imekuwa ikijitokeza. Hivi karibuni huyu mwanamke ameanza tabia ya kukataa kufanya mapenzi. Mnaweza kupanga siku flani mkutane mfanye yenu lakini siku ikifika analeta visingizio.
Hali hii imepelekea niamue kuachana naye japo kiuhalisia naona yeye ndio ameamua kuniacha, maana kama hataki kufanya mapenzi anategemea nini. Kwa hiyo nimekata shauri nimwache tu maana naona kama nimekuwa mtumwa wa mapenzi, nimekuwa mtu wa kumbembeleza kila mara ili tufanye mapenzi ila yeye hata hajali. Tatizo roho inaniuma kweli, akili haifanyi kazi kabisa, najihisi nimepata msongo wa mawazo. Hamu ya kula sina na kila kitu naona hakiendi kabisa.
Najitahidi kuchangamka humu ndani ili wife asihisi kama kuna kitu kinanisumbua. Wanaume wenzangu, hivi hali hii ya kuzama kwenye penzi la mzazi mwenzako inakuwaje? Naomba mnishauri namna nzuri ya kusonga na maisha, mwenzenu napata tabu.