Hivi ni nchi gani nyingine duniani ambayo kila Mei mosi (siku ya wafanyakazi duniani) huongeza mishahara ya watumishi wake wa umma?

Tunamuomba RAIS Mama Samia na Serikali yetu sikivu wasikie kilio Chetu Sisi wastaafu tuliostaafu wakati mfumo wa mishahara Serikalini Ikiwa kidogo.Maana pension inalipwa kulingana na size ya mshahara WAKO wakati unastaafu.Mfano Mimi nilikuwa Officer wa Serikali Mwenye first degree niliyekuwa nimefanya kazi kwa zaidi ya miaka 15 baada ya ku-graduate.Wakati nastaafu,mshahara wangu ulikuwa sh 25,000 kwa mwezi(kwa wakati HUO mshahara huu ulikuwa unanitosha mahitaji muhimu kwa mwezi(ambayo siyo ya anasa).Pension yangu kwa mwezi kwa Sasa nalipwa sh 100,000.Ni kidogo Sana jamani kwa Khali ya MAISHA ilivyo kwa Sasa.Equivalent officer (kwa cheo nilichostaafu nacho Mimi) aliyestaafu miaka ya karibuni analipwa pension ya shs 1,000,000 kwa mwezi.Tunaomba Serikali ituongezee angalao pension yetu Sisi tuliostaafu zamani pension angalao tulipwe sh 300,000 kwa mwezi badala ya hii sh 100,000 tunayolipwa KILA mwezi kwa Sasa.
 
Hayo mambo ya ongezeko la mshahara mara nyingi ilikuwa ni kuongeza kima cha chini, wenye mishahara mikubwa walikuwa wanaguswa kidogo sana or hawaguswi kabisa.
Nyongeza za Mei mosi zilikuwa zinagusa ngazi zote za mishahara ikiwamo zile zenye mishahara fixed (K to Z). Kitarakimu wale wa mishahara ya juu ndiyo walipata nyingi ukilinganisha na wale wa chini ila kwa ongezeko kwa percentage (asilimia ya mshahara) wale wa chini ongezeko kwa asilimia ilikuwa ni kubwa kuliko wale wa juu.

Nadhani unajua kuwa kwa watumishi wa serikali kuna ngazi (madaraja) 24 za mishahara ambazo zimepewa herudi za alfabeti - yaani A hadi Z. Zile ngazi za juu sana (O hadi Z) ni za mtu (cheo) mmoja mmoja. Kwa mfano ngazi ya Z ni ya rais pekee., Spika wa Bunge ana ngazi yake peke na vivo hivyo kwa Jaji Mkuu, Waziri Mkuu na kadhalika. Ngazi ya mshahara ndiyo heshima kwa mtumishi wa serikali na kila mmoja anastahiki yake inayokuwa reflected na ngazi aliyonayo. Hivyo kucheleweshwa au kutokupandishwa ngazi ni kukunyima heshima yako unayostahili baada ya utumishi wako wa miaka uliyolitumikia taifa!
 
Ngoja nikuulize swali jepesi tu

Hivi nchi gani duniani, ambayo imewahi shuhudia watumishi wake wa Umma, hawajaongezewa mishahara yao, ambayo ni kwa mujibu wa sheria, kwa miaka 5 mfululizo??
Nchi zote duniani isipokuwa Tanzania miaka ya 2005 hadi 2015. Nadhani nimekujibu sahihi, nipe vyema yangu ikiambatana na very good au excellent!
 
Back
Top Bottom