Hivi ni nani anatakiwa kuwa mfano kwa kulipa kodi?

kandawe

JF-Expert Member
Jun 24, 2013
1,137
809
Jana tukiwa na furaha na bashasha za kusubilia KIFAA chetu brand new AIR BUS 220-300, Mh mkuu wa mkoa wa Dar Es Salaam ndugu Paul makonda alipewa nafasi ya kuwakaribisha na kuwatambulisha wananchi wa mkoa wake maana yeye ndiye alikuwa mwenyeji wa hafla hiyo.

Katika hotuba yake fupi ya ukaribisho alimuahidi Mh Rais kuwa wanampango mkakati wa kujifungia ndani yeye pamoja na watendaji wake ili kufanyia kazi suala la ukusanyaji wa kodi. Na alienda mbali zaidi kwa kumhakikishia Mh Rais kuwa jiji la Dar Es Salaam litakuwa namba moja kwa ukusanyaji wa kodi.

Nilisikiliza na baadae nikaanza kujiuliza na kutopata majibu mimi mwenyewe,

kuwa Mh Makonda, asimamie ukusanyaji wa ushuru na mpka jiji la Dar es Salaam liwe kinara wa ukusanyaji mapato wakati sio miezi mingi ilopita Mh Makonda alikuwa na mgogoro na TRA pamoja na waziri wa fedha juu ya kutolkulipa kodi.

Huyu alietaka asilipe kodi leo anakuwa kinara wa ukusanyaji wa kodi?

Au ni watu gani ambao ni walengwa wa kulipa kodi ili jiji letu liwe kinara wa ukusanyaji wa mapato/kodi?
 
Unapaswa tuu kuelewa kwa serikali hii huyu kijana ni "maalumu" hata akikosea atavumiliwa!!
 
Ameokoka na kuacha hy dhambi, umebaki Ww na yule, nendeni mkatubu mumpe kaisali kodi yake.
 
Kuna wakati unalazimika kuamini kwamba uchawi upo na DAB amebobea kama sio kiongozi wao.
 
Ukusanyaji wa kodi unataka mikakati mikubwa na akili
Lakini kwa ukusanyaji wetu wataumia wafanyabiashara tu kwa sana
Wangekuwa wanaangalia wengine wanakusanya kwa njia zipi
Halafu Mayor huko huwa ana kazi gani?
 
Ukusanyaji wa kodi unataka mikakati mikubwa na akili
Lakini kwa ukusanyaji wetu wataumia wafanyabiashara tu kwa sana
Wangekuwa wanaangalia wengine wanakusanya kwa njia zipi
Halafu Mayor huko huwa ana kazi gani?
Sure,
Shida ni pale mkwepa kodi anageuka kutuhubilia ulipaji wa kodi
 
Back
Top Bottom