Nani anayekagua na kudhibiti ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali(CAG)?

Amavubi

JF-Expert Member
Dec 9, 2010
30,142
13,216
Pamoja na mazuri ninayohisi yamefanywa na CAG, najiuliza ni nani anayemkagua katika utendaji wake?

-------- Michango-------

SubiriJibu anasema,

Mleta mada,

Ukiachilia mbali wanaokubeza kwa mada yako inabidi nikupongeze kwani umeleta kitu kikubwa kilichojificha kutokana na wengi wetu nikiwemo mimi tuko wavivu wa kusoma.

Katiba yetu iko wazi kabisa kuhusu CAG. Ibara ya 143 (i) inasema: {Kutakuwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali wa Jamhuri ya Muungano.}

Hapo hakuna matatizo. Jibu la swali lako linaweza kupatikana kwenye ibara ya 143(6) isemayo hivi: {Katika kutekeleza madaraka yake kwa mujibu wa masharti ya ibara ndogo ya (2), (3) na (4) ya ibara hii, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu hatalazimika kufuata amri au maagizo ya mtu mwingine yeyote au idara yoyote ya Serikali, lakini maelezo hayo ya ibara hii ndogo hayataizuia Mahakama nayo kutumia madaraka yake kwa ajili ya kuchunguza kama Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu ametekeleza madaraka yake kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii au sivyo.}

Hapo kwenye blue ni kwamba CAG si mwisho he/she is subject to court. Hivyo, CAG anaweza kushitakiwa mahakamani kama ameboronga.

Kikubwa kingine ambacho hukukileta lakini nakiona potential kwenye post yako ni kwenye ibara ya 143(4) isemayo hivi: { Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu atawasilisha kwa Rais kila taarifa atakayotoa kwa mujibu wa masharti ya ibara ndogo ya (2) ya ibara hii. Baada ya kupokea taarifa hiyo Rais atawaagiza watu anaohusika wawasilishe taarifa hiyo kwenye kikao cha kwanza cha Bunge kitakachofanyika baada ya Rais kupokea taarifa hiyo na itabidi iwasilishwe katika kikao hicho kabla ya kupita siku saba tangu siku ile kilipoanza kikao hicho. Iwapo Rais hatachukua hatua za kuwasilisha taarifa hiyo kwa Spika wa Bunge (au Naibu wa Spika ikiwa kiti cha Spika ki wazi wakati huo au ikiwa kwa sababu yoyote Spika hawezi Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania}

Hapa ndipo penye sakata ambalo inawezekana hujui lakini umelianzisha. Maana yake ni nini? Maana yake ni kwamba Rais ndiye anayepewa report ya madudu aliyogundua CAG wakati wa ukaguzi wake. Mara tu Rais anapoipata report hiyo anaipeleka kopi Bungeni.

Hivyo, mtiririko wa safari ya report ni kwamba inaanza kwa CAG, inaenda kwa Rais, kisha inaenda Bungeni. Hakuna mahala panapoonyesha kuwa Makamu wa Rais, au Waziri Mkuu au Waziri yoyote anapitia mlolongo wa kuipokea au kuigusa report ya CAG.

Kumbe, Waziri Mkuu na mawaziri wenzake, wanashtukia kuyasoma madudu yale report inaposomwa Bungeni. Hivyo, kwa utaratibu huu mtu pekee anayejua madudu ya report kabla haijaenda Bungeni ni Rais na CAG tu.

Kwa utaratibu huu, huwezi kusema Waziri Mkuu hakumshauri Rais kuhusu madudu yaliyomo kwenye report ya CAG wakati Waziri Mkuu hakupata nafasi ya kuiona kwani utaratibu uko wazi kabisa yeye anaijua report inaposomwa Bungeni.

Nakubali kwamba Pinda anaweza kuwa aliiona mapema, lakini kikatiba anapoiona Pinda ni kwamba ime-leak kwani hakutakiwa hadi aisikie ikisomwa Bungeni.

Hivyo, kikatiba huwezi kusema Pinda anapaswa kuwajibika kwa lolote lililotajwa na CAG. Eti hakumshauri Rais. Angemshauri vipi kwa jambo ambalo katiba yenyewe inasema kuwa hakutakiwa kulijua kabla report haijasomwa Bungeni na kuisikia kama tunavyoisikia sisi.

Hivyo, aliyeshindwa kuwawajibisha mawaziri kabla hata repirt haijaenda Bungeni ni Rais mwenye kikatiba na tuache ngonjera zingine za kisiasa ambazo hazitasaidia kuubadilisha ukweli huu wa kikatiba.

Someni ibara mbili za katiba yaani 143 na 144 ambapo ukweli ninaosema umeanikwa wazi hata primary school pupil anaweza kuusoma.

Namalizia tena, hongera mleta mada, na kama magazeti yatapitia thread hii, hii ni habari mpya ya kubadilisha upepa wa suala zima ambalo sasa eti linachukua sura ya kisiasa wakati ni suala la kikatiba.
 
CAG anakaguliwa na wakaguzi wenzake wa nje. Katika taaluma ya kikaguzi kuna kitu inaitwa peer review ama Engagement Quality Review ambapo kunakuwa na wakaguzi wenzi ambao hukagua utendaji wa wakaguzi wengine ili kuangalia kama wanatenda kazi zao kulingana na weledi. Ila kitu nilichogundua ni kwamba hii taaluma imejilinda sana hivyo hata hizo report huwa si za hadhara.
 
CAG anakaguliwa na wakaguzi wenzake wa nje. Katika taaluma ya kikaguzi kuna kitu inaitwa peer review ama Engagement Quality Review ambapo kunakuwa na wakaguzi wenzi ambao hukagua utendaji wa wakaguzi wengine ili kuangalia kama wanatenda kazi zao kulingana na weledi. Ila kitu nilichogundua ni kwamba hii taaluma imejilinda sana hivyo hata hizo report huwa si za hadhara.
Maana yake ni wao kwa wao....nataka kujua anatumia kiasi gani mpaka anahitimisha kazi yake na kuna usafi kiasi gani katika matumizi hayo
 
Maana yake ni wao kwa wao....nataka kujua anatumia kiasi gani mpaka anahitimisha kazi yake na kuna usafi kiasi gani katika matumizi hayo

Mkuu nilijua tu kwamba mwisho wa siku ni matumizi ya utendaji kazi. Kusema kweli jinsi ninavyojua hawa wanaofanya ukaguzi kwa wakaguzi huwa wanaangalia budget na matumizi ya CAG (sijui kama CAG wa TZ) amewahi kufanyiwa ukaguzi huu. Lakini lengo lao kuu huwa ni kuangalia kama CAG anakagua kulingana na standards walizojiwekea. Huenda kwa CAG nako kuna madudu.
 
nakuelewa,AU NDO MANA J.K ALISEMA RIPOTI YA CAG IENF BUNGENI?

Mkuu Report ya CAG kwenda bungeni ni matakwa ya Kikatiba. Imekuwa ikienda bungeni miaka yote. Tatizo ni kwamba miaka ya nyuma ilikuwa report zinachelewa sana. Kwa mfano ungweza kukuta report ya 2007/2008 inasomwa bungeni mwaka 2012 kwa hiyo zikawa zinakosa impact. Ila miaka ya hivi karibuni ukaguzi umekuwa ukifanywa kwa wakati na repott kwenda bado ya motomoto kama hii ya juzi.
 
Naona wote mnajikanyaga na kuna baadhi yetu hawajaelewa hoja ya mleta hoja. Someni[SUP]1 [/SUP]hapa:-


46. Audit of accounts
(1) The accounts of the National Audit Office shall be audited, at least once in every financial year, by a person appointed by the Public Accounts Committee from amongst persons who are registered as auditors under the Auditors and Accountants (Registration) Act or possessing such other qualifications as the Public Accounts Committee may determine, at such remuneration and, on such other terms and, conditions as the Public Accounts Committee may determine.

(2) The remuneration of the auditor appointed under subsection (1) shall be defrayed from the funds of the National Audit Office.

(3) In the performance of his functions the auditor shall have the same powers as the Controller and Auditor-General has in respect of the audit of public authorities and other bodies.

(4) Upon completion of examination of the accounts of the National Audit Office, the auditor shall express a professional opinion on the accounts and submit the report to the Public Accounts Committee.

(5) The Public Accounts Committee shall consider the report and submit the same to the Minister with or without comment.

(6) Upon receipt of the report, the Minister shall submit the report in the next session of the National Assembly together with the responses of the Management.


[SUP]1[/SUP]
http://www.nao.go.tz/files/PUBLIC%20AUDIT%20ACT.pdf
 
Ngoja tuulize. Nani anamkagua jaji??
Jaji akishatoa hukumu, nani anatoa hukumu ya kumuhukumu Jaji aliyetoa hukumu ya kwanza.

Ukishatoa majibu hapa. Utajijibu swali lako la kwanza.
 
Ngoja tuulize. Nani anamkagua jaji??
Jaji akishatoa hukumu, nani anatoa hukumu ya kumuhukumu Jaji aliyetoa hukumu ya kwanza.

Ukishatoa majibu hapa. Utajijibu swali lako la kwanza.

Ana report kwa Goverment Audit Committee sijui ipo? Au Bunge Audit Commitee na anateuliwa nayo, Sijui ipo kwenye katiba, anateuliwa na GAC au BAU sijui analipwa na nani mshahara-na nani anampangia mshahara-widhara ya fedha-''Wadau wa katiba hii ni changamoto""
 
Hii nchi bwana. Juzi kati wakati wa issue ya Jairo, huyu CAG alionekana mbaya sana, lakini leo anaonekana wa maana sana!
 
CAG inaonekana kakata mirija za baadhi ya watu hapa,zengwe limeanza kuandaliwa kuwa nae ni fisadi,kweli ufisadi ukikuingia huwezi acha.
 
Mleta mada,

Ukiachilia mbali wanaokubeza kwa mada yako inabidi nikupongeze kwani umeleta kitu kikubwa kilichojificha kutokana na wengi wetu nikiwemo mimi tuko wavivu wa kusoma.

Katiba yetu iko wazi kabisa kuhusu CAG. Ibara ya 143 (i) inasema: {Kutakuwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali wa Jamhuri ya Muungano.}

Hapo hakuna matatizo. Jibu la swali lako linaweza kupatikana kwenye ibara ya 143(6) isemayo hivi: {Katika kutekeleza madaraka yake kwa mujibu wa masharti ya ibara ndogo ya (2), (3) na (4) ya ibara hii, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu hatalazimika kufuata amri au maagizo ya mtu mwingine yeyote au idara yoyote ya Serikali, lakini maelezo hayo ya ibara hii ndogo hayataizuia Mahakama nayo kutumia madaraka yake kwa ajili ya kuchunguza kama Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu ametekeleza madaraka yake kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii au sivyo.}

Hapo kwenye blue ni kwamba CAG si mwisho he/she is subject to court. Hivyo, CAG anaweza kushitakiwa mahakamani kama ameboronga.

Kikubwa kingine ambacho hukukileta lakini nakiona potential kwenye post yako ni kwenye ibara ya 143(4) isemayo hivi: { Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu atawasilisha kwa Rais kila taarifa atakayotoa kwa mujibu wa masharti ya ibara ndogo ya (2) ya ibara hii. Baada ya kupokea taarifa hiyo Rais atawaagiza watu anaohusika wawasilishe taarifa hiyo kwenye kikao cha kwanza cha Bunge kitakachofanyika baada ya Rais kupokea taarifa hiyo na itabidi iwasilishwe katika kikao hicho kabla ya kupita siku saba tangu siku ile kilipoanza kikao hicho. Iwapo Rais hatachukua hatua za kuwasilisha taarifa hiyo kwa Spika wa Bunge (au Naibu wa Spika ikiwa kiti cha Spika ki wazi wakati huo au ikiwa kwa sababu yoyote Spika hawezi Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania}

Hapa ndipo penye sakata ambalo inawezekana hujui lakini umelianzisha. Maana yake ni nini? Maana yake ni kwamba Rais ndiye anayepewa report ya madudu aliyogundua CAG wakati wa ukaguzi wake. Mara tu Rais anapoipata report hiyo anaipeleka kopi Bungeni.

Hivyo, mtiririko wa safari ya report ni kwamba inaanza kwa CAG, inaenda kwa Rais, kisha inaenda Bungeni. Hakuna mahala panapoonyesha kuwa Makamu wa Rais, au Waziri Mkuu au Waziri yoyote anapitia mlolongo wa kuipokea au kuigusa report ya CAG.

Kumbe, Waziri Mkuu na mawaziri wenzake, wanashtukia kuyasoma madudu yale report inaposomwa Bungeni. Hivyo, kwa utaratibu huu mtu pekee anayejua madudu ya report kabla haijaenda Bungeni ni Rais na CAG tu.

Kwa utaratibu huu, huwezi kusema Waziri Mkuu hakumshauri Rais kuhusu madudu yaliyomo kwenye report ya CAG wakati Waziri Mkuu hakupata nafasi ya kuiona kwani utaratibu uko wazi kabisa yeye anaijua report inaposomwa Bungeni.

Nakubali kwamba Pinda anaweza kuwa aliiona mapema, lakini kikatiba anapoiona Pinda ni kwamba ime-leak kwani hakutakiwa hadi aisikie ikisomwa Bungeni.

Hivyo, kikatiba huwezi kusema Pinda anapaswa kuwajibika kwa lolote lililotajwa na CAG. Eti hakumshauri Rais. Angemshauri vipi kwa jambo ambalo katiba yenyewe inasema kuwa hakutakiwa kulijua kabla report haijasomwa Bungeni na kuisikia kama tunavyoisikia sisi.

Hivyo, aliyeshindwa kuwawajibisha mawaziri kabla hata repirt haijaenda Bungeni ni Rais mwenye kikatiba na tuache ngonjera zingine za kisiasa ambazo hazitasaidia kuubadilisha ukweli huu wa kikatiba.

Someni ibara mbili za katiba yaani 143 na 144 ambapo ukweli ninaosema umeanikwa wazi hata primary school pupil anaweza kuusoma.

Namalizia tena, hongera mleta mada, na kama magazeti yatapitia thread hii, hii ni habari mpya ya kubadilisha upepa wa suala zima ambalo sasa eti linachukua sura ya kisiasa wakati ni suala la kikatiba.
 
Mkuu Report ya CAG kwenda bungeni ni matakwa ya Kikatiba. Imekuwa ikienda bungeni miaka yote. Tatizo ni kwamba miaka ya nyuma ilikuwa report zinachelewa sana. Kwa mfano ungweza kukuta report ya 2007/2008 inasomwa bungeni mwaka 2012 kwa hiyo zikawa zinakosa impact. Ila miaka ya hivi karibuni ukaguzi umekuwa ukifanywa kwa wakati na repott kwenda bado ya motomoto kama hii ya juzi.

nadhani ulikuwa unahitaji jibu hili-ofisi yake huwa inakaguliwa na PWC.
 
Back
Top Bottom