Amavubi
JF-Expert Member
- Dec 9, 2010
- 30,142
- 13,216
Pamoja na mazuri ninayohisi yamefanywa na CAG, najiuliza ni nani anayemkagua katika utendaji wake?
-------- Michango-------
SubiriJibu anasema,
Mleta mada,
Ukiachilia mbali wanaokubeza kwa mada yako inabidi nikupongeze kwani umeleta kitu kikubwa kilichojificha kutokana na wengi wetu nikiwemo mimi tuko wavivu wa kusoma.
Katiba yetu iko wazi kabisa kuhusu CAG. Ibara ya 143 (i) inasema: {Kutakuwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali wa Jamhuri ya Muungano.}
Hapo hakuna matatizo. Jibu la swali lako linaweza kupatikana kwenye ibara ya 143(6) isemayo hivi: {Katika kutekeleza madaraka yake kwa mujibu wa masharti ya ibara ndogo ya (2), (3) na (4) ya ibara hii, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu hatalazimika kufuata amri au maagizo ya mtu mwingine yeyote au idara yoyote ya Serikali, lakini maelezo hayo ya ibara hii ndogo hayataizuia Mahakama nayo kutumia madaraka yake kwa ajili ya kuchunguza kama Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu ametekeleza madaraka yake kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii au sivyo.}
Hapo kwenye blue ni kwamba CAG si mwisho he/she is subject to court. Hivyo, CAG anaweza kushitakiwa mahakamani kama ameboronga.
Kikubwa kingine ambacho hukukileta lakini nakiona potential kwenye post yako ni kwenye ibara ya 143(4) isemayo hivi: { Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu atawasilisha kwa Rais kila taarifa atakayotoa kwa mujibu wa masharti ya ibara ndogo ya (2) ya ibara hii. Baada ya kupokea taarifa hiyo Rais atawaagiza watu anaohusika wawasilishe taarifa hiyo kwenye kikao cha kwanza cha Bunge kitakachofanyika baada ya Rais kupokea taarifa hiyo na itabidi iwasilishwe katika kikao hicho kabla ya kupita siku saba tangu siku ile kilipoanza kikao hicho. Iwapo Rais hatachukua hatua za kuwasilisha taarifa hiyo kwa Spika wa Bunge (au Naibu wa Spika ikiwa kiti cha Spika ki wazi wakati huo au ikiwa kwa sababu yoyote Spika hawezi Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania}
Hapa ndipo penye sakata ambalo inawezekana hujui lakini umelianzisha. Maana yake ni nini? Maana yake ni kwamba Rais ndiye anayepewa report ya madudu aliyogundua CAG wakati wa ukaguzi wake. Mara tu Rais anapoipata report hiyo anaipeleka kopi Bungeni.
Hivyo, mtiririko wa safari ya report ni kwamba inaanza kwa CAG, inaenda kwa Rais, kisha inaenda Bungeni. Hakuna mahala panapoonyesha kuwa Makamu wa Rais, au Waziri Mkuu au Waziri yoyote anapitia mlolongo wa kuipokea au kuigusa report ya CAG.
Kumbe, Waziri Mkuu na mawaziri wenzake, wanashtukia kuyasoma madudu yale report inaposomwa Bungeni. Hivyo, kwa utaratibu huu mtu pekee anayejua madudu ya report kabla haijaenda Bungeni ni Rais na CAG tu.
Kwa utaratibu huu, huwezi kusema Waziri Mkuu hakumshauri Rais kuhusu madudu yaliyomo kwenye report ya CAG wakati Waziri Mkuu hakupata nafasi ya kuiona kwani utaratibu uko wazi kabisa yeye anaijua report inaposomwa Bungeni.
Nakubali kwamba Pinda anaweza kuwa aliiona mapema, lakini kikatiba anapoiona Pinda ni kwamba ime-leak kwani hakutakiwa hadi aisikie ikisomwa Bungeni.
Hivyo, kikatiba huwezi kusema Pinda anapaswa kuwajibika kwa lolote lililotajwa na CAG. Eti hakumshauri Rais. Angemshauri vipi kwa jambo ambalo katiba yenyewe inasema kuwa hakutakiwa kulijua kabla report haijasomwa Bungeni na kuisikia kama tunavyoisikia sisi.
Hivyo, aliyeshindwa kuwawajibisha mawaziri kabla hata repirt haijaenda Bungeni ni Rais mwenye kikatiba na tuache ngonjera zingine za kisiasa ambazo hazitasaidia kuubadilisha ukweli huu wa kikatiba.
Someni ibara mbili za katiba yaani 143 na 144 ambapo ukweli ninaosema umeanikwa wazi hata primary school pupil anaweza kuusoma.
Namalizia tena, hongera mleta mada, na kama magazeti yatapitia thread hii, hii ni habari mpya ya kubadilisha upepa wa suala zima ambalo sasa eti linachukua sura ya kisiasa wakati ni suala la kikatiba.
-------- Michango-------
SubiriJibu anasema,
Mleta mada,
Ukiachilia mbali wanaokubeza kwa mada yako inabidi nikupongeze kwani umeleta kitu kikubwa kilichojificha kutokana na wengi wetu nikiwemo mimi tuko wavivu wa kusoma.
Katiba yetu iko wazi kabisa kuhusu CAG. Ibara ya 143 (i) inasema: {Kutakuwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali wa Jamhuri ya Muungano.}
Hapo hakuna matatizo. Jibu la swali lako linaweza kupatikana kwenye ibara ya 143(6) isemayo hivi: {Katika kutekeleza madaraka yake kwa mujibu wa masharti ya ibara ndogo ya (2), (3) na (4) ya ibara hii, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu hatalazimika kufuata amri au maagizo ya mtu mwingine yeyote au idara yoyote ya Serikali, lakini maelezo hayo ya ibara hii ndogo hayataizuia Mahakama nayo kutumia madaraka yake kwa ajili ya kuchunguza kama Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu ametekeleza madaraka yake kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii au sivyo.}
Hapo kwenye blue ni kwamba CAG si mwisho he/she is subject to court. Hivyo, CAG anaweza kushitakiwa mahakamani kama ameboronga.
Kikubwa kingine ambacho hukukileta lakini nakiona potential kwenye post yako ni kwenye ibara ya 143(4) isemayo hivi: { Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu atawasilisha kwa Rais kila taarifa atakayotoa kwa mujibu wa masharti ya ibara ndogo ya (2) ya ibara hii. Baada ya kupokea taarifa hiyo Rais atawaagiza watu anaohusika wawasilishe taarifa hiyo kwenye kikao cha kwanza cha Bunge kitakachofanyika baada ya Rais kupokea taarifa hiyo na itabidi iwasilishwe katika kikao hicho kabla ya kupita siku saba tangu siku ile kilipoanza kikao hicho. Iwapo Rais hatachukua hatua za kuwasilisha taarifa hiyo kwa Spika wa Bunge (au Naibu wa Spika ikiwa kiti cha Spika ki wazi wakati huo au ikiwa kwa sababu yoyote Spika hawezi Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania}
Hapa ndipo penye sakata ambalo inawezekana hujui lakini umelianzisha. Maana yake ni nini? Maana yake ni kwamba Rais ndiye anayepewa report ya madudu aliyogundua CAG wakati wa ukaguzi wake. Mara tu Rais anapoipata report hiyo anaipeleka kopi Bungeni.
Hivyo, mtiririko wa safari ya report ni kwamba inaanza kwa CAG, inaenda kwa Rais, kisha inaenda Bungeni. Hakuna mahala panapoonyesha kuwa Makamu wa Rais, au Waziri Mkuu au Waziri yoyote anapitia mlolongo wa kuipokea au kuigusa report ya CAG.
Kumbe, Waziri Mkuu na mawaziri wenzake, wanashtukia kuyasoma madudu yale report inaposomwa Bungeni. Hivyo, kwa utaratibu huu mtu pekee anayejua madudu ya report kabla haijaenda Bungeni ni Rais na CAG tu.
Kwa utaratibu huu, huwezi kusema Waziri Mkuu hakumshauri Rais kuhusu madudu yaliyomo kwenye report ya CAG wakati Waziri Mkuu hakupata nafasi ya kuiona kwani utaratibu uko wazi kabisa yeye anaijua report inaposomwa Bungeni.
Nakubali kwamba Pinda anaweza kuwa aliiona mapema, lakini kikatiba anapoiona Pinda ni kwamba ime-leak kwani hakutakiwa hadi aisikie ikisomwa Bungeni.
Hivyo, kikatiba huwezi kusema Pinda anapaswa kuwajibika kwa lolote lililotajwa na CAG. Eti hakumshauri Rais. Angemshauri vipi kwa jambo ambalo katiba yenyewe inasema kuwa hakutakiwa kulijua kabla report haijasomwa Bungeni na kuisikia kama tunavyoisikia sisi.
Hivyo, aliyeshindwa kuwawajibisha mawaziri kabla hata repirt haijaenda Bungeni ni Rais mwenye kikatiba na tuache ngonjera zingine za kisiasa ambazo hazitasaidia kuubadilisha ukweli huu wa kikatiba.
Someni ibara mbili za katiba yaani 143 na 144 ambapo ukweli ninaosema umeanikwa wazi hata primary school pupil anaweza kuusoma.
Namalizia tena, hongera mleta mada, na kama magazeti yatapitia thread hii, hii ni habari mpya ya kubadilisha upepa wa suala zima ambalo sasa eti linachukua sura ya kisiasa wakati ni suala la kikatiba.