Hivi ni mimi sijui Hesabu au Mabeberu Wana Hela? Apple Pekee ina Thamani Sawa na Bajeti ya Tanzania ya Miaka 200?

Hivi ni mimi sijui Hesabu au Mabeberu Wana Hela? Apple Pekee ina Thamani Sawa na Bajeti ya Tanzania ya Miaka 200?

Mad Max

JF-Expert Member
Joined
Oct 21, 2010
Posts
33,538
Reaction score
96,686
Ni either mimi hesabu za Kihasibu sijui au Hawa jamaa waheshimiwe!

Makala inaniambia kampuni la Marekani Apple, wenye iPhone, Mac, na iPads zao, wana net-worthy ya zaidi ya US$4.5 trillion tunavyoongea.
IMG_8841.jpeg

Hapo hapo budget yetu kwa mwaka ni US$24 billion.
IMG_8842.jpeg

Kwahiyo ukigawa hapo si kwamba Apple wanathamani mara 200 zaidi ya budget yetu?

Na hapo sio kwamba Apple ndio kampuni lenye thamani kubwa Marekani, wapo wababe juu yake.

Au mi nirudi shule?
 
Tajiri; hapo hapo kwenye bajeti. Makadirio yao ya mmapatokwa mwaka husika waga hayatimii kuleta matumizi halisi "actual eexpenditure" sababu ni kwamba huwa tunaipigia bajeti pesa sio yetu (wahisani/mikopo na ruzuku); na serikali haisemi hilo popote, isipokuwa ni kwamba yale ambayo hayakutekelezwa mwaka husika, hasa miradi, inapelekwa mbele kuja kumaliziwa na bajeti ijayo. Kwa iyo huwa tuna bajeti kiporo/viporo. 😊

Kwa hiyo hapo; unatakiwa upige % flani ambayo ni hewa kila mwaka kutoka kwenye hiyo TZS 62.3 Trillion. Actual expenditure inaweza kuwa TZS 40 Trillion. Hivyo tunawez kuwa tunaingia hata mara 30 kwenye thamani ya Apple Inc.
Ni sawa unakwenda kutoa mahali ukitegemea kubakiza kiasi flani uje ulipe ukipata, ila mke wakupe, mahali kiasi wakudai. 😊
 
Mkuu, hapa kuna tatizo la kuchanganya dhana mbili tofauti kabisa za uchumi.

Apple market cap na GDP ya Tanzania si vitu vinavyopimwa kwa kipimo kimoja. Market cap ni thamani ambayo wawekezaji wanaipa kampuni kwenye soko la hisa, wakati GDP ni thamani ya bidhaa na huduma zote zinazozalishwa nchini ndani ya mwaka mmoja.

Ni sawa na kusema nyumba yangu ina thamani ya milioni 500 halafu nikajilinganisha na mtu anayepata mshahara wa milioni 50 kwa mwaka. Namba zinaweza kulinganishwa, lakini kiuchumi ni vipimo viwili tofauti.

Kitu kingine ambacho watu wengi hawakielewi ni kwamba Apple haina fedha zote zinazolingana na market cap yake. Market cap ni makadirio ya thamani ya kampuni kutokana na bei ya hisa zake. Kesho hisa zikishuka kwa 20%, mamia ya mabilioni ya dola yanaweza "kutoweka" kwenye market cap bila hata iPhone moja kupotea.

GDP ya Tanzania kwa upande mwingine ni shughuli halisi za kiuchumi: kilimo, madini, viwanda, biashara, usafirishaji, utalii, huduma n.k.

Kwa hiyo kusema "Apple ina thamani sawa na bajeti ya Tanzania ya miaka 200" kunavutia kusoma lakini si uchambuzi sahihi wa kiuchumi. Comparison yenye maana zaidi ingekuwa Apple revenue dhidi ya GDP ya Tanzania, au market cap ya Apple dhidi ya market cap ya makampuni yote yaliyosajiliwa kwenye soko la hisa la Tanzania.

Tusipende namba kubwa zikatushangaza mpaka tukaanza kulinganisha maembe na pikipiki.
 
Mkuu, hapa kuna tatizo la kuchanganya dhana mbili tofauti kabisa za uchumi.

Apple market cap na GDP ya Tanzania si vitu vinavyopimwa kwa kipimo kimoja. Market cap ni thamani ambayo wawekezaji wanaipa kampuni kwenye soko la hisa, wakati GDP ni thamani ya bidhaa na huduma zote zinazozalishwa nchini ndani ya mwaka mmoja.

Ni sawa na kusema nyumba yangu ina thamani ya milioni 500 halafu nikajilinganisha na mtu anayepata mshahara wa milioni 50 kwa mwaka. Namba zinaweza kulinganishwa, lakini kiuchumi ni vipimo viwili tofauti.

Kitu kingine ambacho watu wengi hawakielewi ni kwamba Apple haina fedha zote zinazolingana na market cap yake. Market cap ni makadirio ya thamani ya kampuni kutokana na bei ya hisa zake. Kesho hisa zikishuka kwa 20%, mamia ya mabilioni ya dola yanaweza "kutoweka" kwenye market cap bila hata iPhone moja kupotea.

GDP ya Tanzania kwa upande mwingine ni shughuli halisi za kiuchumi: kilimo, madini, viwanda, biashara, usafirishaji, utalii, huduma n.k.

Kwa hiyo kusema "Apple ina thamani sawa na bajeti ya Tanzania ya miaka 200" kunavutia kusoma lakini si uchambuzi sahihi wa kiuchumi. Comparison yenye maana zaidi ingekuwa Apple revenue dhidi ya GDP ya Tanzania, au market cap ya Apple dhidi ya market cap ya makampuni yote yaliyosajiliwa kwenye soko la hisa la Tanzania.

Tusipende namba kubwa zikatushangaza mpaka tukaanza kulinganisha maembe na pikipiki.
Maelezo mazuri Ila amelinganisha BAJETI na thamani sio GDP na thamani.
 
Ni either mimi hesabu za Kihasibu sijui au Hawa jamaa waheshimiwe!

Makala inaniambia kampuni la Marekani Apple, wenye iPhone, Mac, na iPads zao, wana net-worthy ya zaidi ya US$4.5 trillion tunavyoongea.
View attachment 3597923
Hapo hapo budget yetu kwa mwaka ni US$24 billion.
View attachment 3597924
Kwahiyo ukigawa hapo si kwamba Apple wanathamani mara 200 zaidi ya budget yetu?

Na hapo sio kwamba Apple ndio kampuni lenye thamani kubwa Marekani, wapo wababe juu yake.

Au mi nirudi shule?
ikiwa ni hivyo,
fikiri na waza kitajiri sasa gentleman na sio kinyonge na kimaskini hivyo,

ni muhimu sana kuifanya hali hiyo kua fursa kwako na kuacha uvivu bali kuzidisha juuhudi zaidi katika kufanya kazi kwa bidii na maarifa, ili kufikia malengo yako kiuchumi na sio malengo ya mwingine,

mafanikio ya wengine yasikutie kiwewe na kukuduwaza bali ya kusisimue na kukufanya uwe na malengo mahususi zaidi kiuchumi 🐒
 
Ni either mimi hesabu za Kihasibu sijui au Hawa jamaa waheshimiwe!

Makala inaniambia kampuni la Marekani Apple, wenye iPhone, Mac, na iPads zao, wana net-worthy ya zaidi ya US$4.5 trillion tunavyoongea.
View attachment 3597923
Hapo hapo budget yetu kwa mwaka ni US$24 billion.
View attachment 3597924
Kwahiyo ukigawa hapo si kwamba Apple wanathamani mara 200 zaidi ya budget yetu?

Na hapo sio kwamba Apple ndio kampuni lenye thamani kubwa Marekani, wapo wababe juu yake.

Au mi nirudi shule?
You aren’t serious! Unawezaje kuilinganisha Apple na Tanzania? Sisi size yetu ni individual billionaires, sio heavyweight corporations!

Kuna nchi nne tu duniani ambazo zina GDP inayozidi utajiri wa Apple. Hizo nchi ni USA, China, Germany na Japan!
 
Maelezo mazuri Ila amelinganisha BAJETI na thamani sio GDP na thamani.
Mkuu, Hata hivyo hoja yangu kuu bado ipo.

Bajeti ya serikali ni kiasi kinachopangwa kutumiwa ndani ya mwaka mmoja, wakati market cap ya Apple ni makadirio ya thamani ya kampuni kwenye soko la hisa. Hivyo bado tunalinganisha vipimo viwili vyenye maana tofauti.

Mfano, mtu akiwa na nyumba ya bilioni 1 na matumizi yake ya mwaka ni milioni 20, huwezi kusema nyumba yake ni sawa na matumizi yake ya miaka 50 halafu ukahitimisha moja kwa moja kuwa ana fedha hizo mkononi.

Kuna jambo lingine ambalo watu wengi hulisahau. Tuchukulie kwa mawazo ya kinadharia kuna tajiri mmoja akaamua kununua Apple yote kwa thamani yake ya soko. Je, atatoa fedha zote zinazolingana na market cap iliyokuwa inaonekana jana?

Si lazima. Mara tu anapoanza kununua hisa kwa kiwango kikubwa, bei ya hisa itaanza kubadilika kutokana na mahitaji ya soko, matarajio ya wawekezaji, na upatikanaji wa hisa zinazouzwa. Vivyo hivyo, kama wanahisa wote wa Apple wangejaribu kuuza kwa wakati mmoja, market cap ingeanguka haraka sana.

Ndiyo maana market cap si fedha zilizowekwa benki kusubiri kuchukuliwa. Ni makadirio ya thamani yanayotegemea bei ya hisa katika muda fulani.

Kwa hiyo comparison inaweza kutumika kuonesha ukubwa wa Apple, lakini si ushahidi kwamba Apple ina fedha taslimu sawa na bajeti ya Tanzania ya miaka 200.
 
Bajeti sio real money hasa kwa nchi kama Tanzania. Kila mwaka hela nyingi zilizoahidiwa kwenye bajeti hazifiki kunakohusika na sehemu ya bajeti ni hela ya msaada.
Bado hujaiweka kwenye uzito watu watalichukulia poa hili.

Kwenye bajeti hii ya mwaka huu tumechangia 75% yake na fedha zingine ni mikopo, grants na donor funds. Hata hivyo Tanzania haijawahi kuwa na surplus budget, huwa siku zote ina deficit.

Lakini hapo hapo bado kwenye bajeti hii inayoelekea kuisha, 25.2% ya bajeti ilipangwa kulipia mikopo na riba ya mikopo iliyopita.

Kwahiyo kwenye 100% ya bajeti, 25% ya fedha sio zetu ni mikopo yenye riba na misaada michache wakati huo 25% ni kulipa madeni. Tunabaki na bajeti halisi kama 50% ambayo nayo huwa haifikiwi kabisa.

Kwenye bajeti nzima 68% yake ni recurrent expenditure ambapo kinachobaki ndio fedha za maendeleo kama barabara na shule. Mwisho wa siku sisi bado tu ni mbumbumbu mbele ya Apple Inc. sababu wao wana bajeti kubwa ya research and development kwahiyo wako more likely kuuza zaidi kuliko sisi ambao hela nyingi ni za kulipa walimu na kujenga vyoo shuleni kila mwaka maana nchi inazaliana kama vile hakuna shughuli nyingine ya kufanya.

Ingawa kiustahimilivu nchi yoyote ile inasimama vizuri kuliko kampuni. Tunaweza kunywa uji na matikiti kwa miaka hata 30 na nchi isipotee completely. Ila Apple ni tech company haiwezi stahimili kufanya upuuzi kwa miaka hata mitano, inapotea kabisa kabisa.
 
Ni either mimi hesabu za Kihasibu sijui au Hawa jamaa waheshimiwe!

Makala inaniambia kampuni la Marekani Apple, wenye iPhone, Mac, na iPads zao, wana net-worthy ya zaidi ya US$4.5 trillion tunavyoongea.
View attachment 3597923
Hapo hapo budget yetu kwa mwaka ni US$24 billion.
View attachment 3597924
Kwahiyo ukigawa hapo si kwamba Apple wanathamani mara 200 zaidi ya budget yetu?

Na hapo sio kwamba Apple ndio kampuni lenye thamani kubwa Marekani, wapo wababe juu yake.

Au mi nirudi shule?
Hiyo ni thamani ya kampuni (market capitalization) sio net worth. Market capitalization ya kampuni ni jumla ya thamani ya hisa zote za hiyo kampuni. Kwa kifupi hayo ni mahesabu ya kwenye makaratasi tu. Thamani ya hisa hupanda na kushuka kutokana na perfomance ya kibiashara ya kampuni husika. Hizo hisa za apple zinaweza kushuka na kushusha thamani ya kampuni muda wowote kutokana na mazingira mbalimbali.
 
Back
Top Bottom