Dam55
JF-Expert Member
- Oct 8, 2015
- 5,592
- 11,831
Nimemsikiliza mh Bernard Membe leo ameongea jambo ambalo kwa kweli linaamsha fikira nyingi sana. Anahoji tutakwenda vipi kwenye Uchaguzi bila kuwepo kwa wasimamizi wa uchaguzi wa kimataifa? Kwasababu kutokana na Janga la corona itasababisha wasimamizi hao kuto kuja mwezi Oktoba, ameenda mbali zaidi kwa kusema kuwa wengine walishauri kuwa uchaguzi huo usogezwe mbele ili kutoa nafasi ya wasimamizi wa kimataifa waweze kushiriki.
Hivi ina maana sisi waafrica hatuwezi kujisimamia wenyewe kwenye chaguzi zetu?
Yani tuahirishe uchaguzi kisa tu mzungu hajaja kutusimamia?
Uko wapi uwezo wetu wa kujitawala na kujiamulia mambo yetu?
Fikira za kikoloni zitaondoka lini vichwani mwa hawa viongozi wetu?
Sasa sisi watanzania awamu hii tutafanya uchaguzi kwa kujisimamia wenyewe hatutaki hao wazungu tuone kama tutashindwa kupata viongozi makini.
Hivi ina maana sisi waafrica hatuwezi kujisimamia wenyewe kwenye chaguzi zetu?
Yani tuahirishe uchaguzi kisa tu mzungu hajaja kutusimamia?
Uko wapi uwezo wetu wa kujitawala na kujiamulia mambo yetu?
Fikira za kikoloni zitaondoka lini vichwani mwa hawa viongozi wetu?
Sasa sisi watanzania awamu hii tutafanya uchaguzi kwa kujisimamia wenyewe hatutaki hao wazungu tuone kama tutashindwa kupata viongozi makini.