ZINDAGI
JF-Expert Member
- Dec 5, 2015
- 1,117
- 1,424
Acha tulipe tuu ili tuwasaidie wenye nyumba, maana wamegharamika kujenga hizi nyumba tunazopanga.
Sent using Jamii Forums mobile app
Sent using Jamii Forums mobile app
Hili balaa lianze mkoa wa mtwara, nyumba kupanga bei ghalii mnoooo ukilinganisha na ubora wa nyumba yenyewe
Sent using Jamii Forums mobile app
Hiyo hela wewe hujagaramika kuipata ! Na ikalimwa na kodi km cyo kuibiwa masaa ya kazi.Acha tulipe tuu ili tuwasaidie wenye nyumba, maana wamegharamika kujenga hizi nyumba tunazopanga.
Sent using Jamii Forums mobile app
Hukuna sababu ya kupiga marufuku watu kujenga. Hio serikali ijenge hizo nyumba Bora na nafuu kuliko ambazo watu wanajenga,waziuze kwa mikopo nafuu uone kama watu watahangaika kujenga makazi holela.Ifikie mahala sasa hii biashara isifanywe tu kiholela na kila mtu, kuwe na standard maalum ya nyumba za kupangishwa na pia kuwe na controlling..
NHC iwe na kitengo maalum cha kufuatilia standard za nyumba za biashara na viwango vya gharama za upangishaji kila mahala..Kusiwe tena na madalali bali kuwe na madalali waliosajili na lazima wawe na website itakayoweka picha za nyumba zote baada ya ukaguzi wa NHC ionyeshwe ina nini na nini kwa maana ya kiwango chake na bei yake..
Serikali ipige marufuku raia kujenga majumba baadala yake kazi hiyo ifanywe na Estate agencies kwenye maeneo elekezi na wananchi wakopeshwe nyumba na waruhusiwe kuishi huku wanalipa with reasonable price, hii itaondoa ujenzi holela na usiofuata taratibu na pia miji yetu itakuwa imepangiliwa na nyumba standard na mitaa itakuwa ya kisasa..
Location,location,location.Nakubaliana nawe, japo hapo kupiga marufuku watu kupangisha nyumba kidogo naona itakuwa harsh. Watu waruhusiwe kufanya hiyo biashara ila tu wafuate utaratibu utakaowekwa. Hilo la kupanga viwango vya kodi kulingana na standard ni la msingi sana. Unakuta nyumba ya zamani kabisa, Chumba, sebule, jiko na choo eti inapangishwa 350,000 Tshs kwa mwezi, kisa ipo Sinza, K.nyama au Kinondoni.
Hukuna sababu ya kupiga marufuku watu kujenga. Hio serikali ijenge hizo nyumba Bora na nafuu kuliko ambazo watu wanajenga,waziuze kwa mikopo nafuu uone kama watu watahangaika kujenga makazi holela.
Ntwara oil and gas iliwadumaza wakapandisha vitu mabei bila uhalisia, oil and gas is no longer now bado akili zao ziko huko kisaikolojia.
Kodi kubwa nhc.
Nyerere alijali wafanyakazi kupata nyumba za kuishi kwa Bei nafuu. Including kota
Kabisa mkuuHivi katika kufikiri kwako,hao wanaotaka kupitisha hiyo sheria hawana nyumba za kupanga,tuendelee kujikongoja tu mkuu ili tujenge za kwetu...
Wala hatukatai kuwa waligharamika, tunataka tu kuwe na utaratibu kisheria. Kama ilivyo mtu akitaka kufanya biashara ya Bus amegharamika kulinnua, lakini lazima afuate bei elekezi zilizowekwa pamoja na kuhudumia watu kwa utaratibu.Acha tulipe tuu ili tuwasaidie wenye nyumba, maana wamegharamika kujenga hizi nyumba tunazopanga.
Sent using Jamii Forums mobile app
Nilidhani serikali sasa iko kwenye kazi ya urasimishaji makazi? Tuseme Waziri Lukuvi hakusema ukweli?Huwezi kuregulate makazi yasiyo rasmi. Huyajui, Sasa utaregulste vipi?
Hivyo sivyo inavyopaswa kuwa ndugu. Kwenye hiyo 300 yake inakatwa 30, na anapaswa kuwa na mashine ya efd....Hizi mambo naziona Masaki, Obey, Mikocheni. Mzungu huwezi kumpangisha nyumba kizembe bila receipt.Halafu msisahau. Kodi kwenye pango zipo.
1.withholding tax ambayo ni 10%
2.stamp duty 1%
Mwenye nyumba atakuongezea wewe tu, yeye hataumia. Mfano Kodi yako 300,000/- ukiongeza tax inabidi iwe 330,000/- ili kulipa 10% na yeye abaki na 300,000/- yake. Je mpangaji utachagua ulipe 300,000 au 330,000/- ?
Wengine Wakawahonga Mademu ZaoBaada ya nyerere kuna washenzi wakajiuzia hizo nyumba kwa bei ya boda boda.. huku wakijua wafanyakazi watakosa pa kuishi
Sent using Jamii Forums mobile app
Wewe wasema. Mwenye nyumba kashaamua apate 300,000/- hio 10% utalipa wewe anaongeza kwenye Kodi. Mwisho wa siku mpangaji ndio anabeba mzigo. Wewe unaona Masaki Sisi tunalipa hivyo humu uswahilini kwasababu tra ukienda kwenye makadirio ya Kodi lazima ulete mkataba wa pango na ulipiwe 10+1%Hivyo sivyo inavyopaswa kuwa ndugu. Kwenye hiyo 300 yake inakatwa 30, na anapaswa kuwa na mashine ya efd....Hizi mambo naziona Masaki, Obey, Mikocheni. Mzungu huwezi kumpangisha nyumba kizembe bila receipt.
Kwa kuongea, sawa.Nilidhani serikali sasa iko kwenye kazi ya urasimishaji makazi? Tuseme Waziri Lukuvi hakusema ukweli?
Mkuu kama wapangaji wenyewe mmeshindwa kujiunga na kutetea maslahi yenu mnatarajia wenye nyumba ndo wawa tetee?au mnatarajia serikali ndo iwatetea.Kama mnataka kuondokana na kero basi hakikisheni kwanza mnaungana na kuunda Chama cha Wapangaji.Kisha muwe na Viongozi wenu muwe na ofisi zenu,Mlipe ada za uanachama kisha mtatewa na maslahi yenu mtapata.Zaidi ya asilimia 80 ya wananchi hasa mijini wanaishi nyumba za kupanga. Kwa mji kama DSM ambapo bado kuna uhitaji mkubwa wa makazi bora, watu hutumia zaidi ya robo ya vipato vyao kulipia kodi za nyumba kila mwezi, lakini cha kushangaza, serikali haioni unyeti wa kuingilia na kusimammia sehemu hii. Hapa nina hakika serikali ingeweza kukusanya kodi ya kutosha kabisa kutoka kwa wenye nyumba iwapo wangeweka utaratibu mzuri wa usimamizi.
Tunaelekea kumaliza miaka 5 ya awamu ya kwanza ya JPM, lakini waziri Lukuvi na wizara yake wamekuwa wakiimba tu mapambio juu ya kanuni za upangishaji nyumba. Ugumu uko wapi kuleta sheria na kanuni zake ili kuwaondolea kero wananchi wanaopanga nyumba? Watu wanalazimishwa kulipa kodi mpaka ya mwaka mzima kisa tu hakuna kanuni husika.
Tutengeneze sheria, kama mtu akiamua kupangisha nyumba yake basi akubali kufuata kanuni za serikali, moja wapo ni kutolazimisha mtu kulipa kodi ya miezi 6/mwaka.
Kuna issue ya madalali wa nyumba, ambao kwanza wengi wao huku uswahilini hawajasajiliwa, maana yake wanafanya kazi bila utaratibu maalum. Matokeo yake wamejitengenezea utaratibu usio haki wala halali wa kudai kodi ya mwezi mmoja kama mtu ataamua kupanga nyumba husika. Wizara ya Ardhi kama wangekuwa wanatimiza wajibu wao, leo hii tungekuwa na muongozo wa kuwasajili na kutengeneza viwango vya malipo halali kwao pamoja na kukusanya kodi kutoka kwenye vipato vyao.
Haiwezekani mtu apewe kodi ya mwezi mmoja ambayo hata haikatwi kodi mahali popote na serikali kisa tu alisimama katikati ya mwenye nyumba na mpangaji.
Waziri Lukuvi, hizi ni petty issues kwako, ambazo ukiamua tu ndani ya muda mchache solution inapatikana na impact inakuwa kubwa.