kwenyula
Member
- Aug 28, 2016
- 43
- 118
Hakuna kitu roho inaniuma kama kuona Upinzani nchi hii wakiwa wanazongwa kila kona. Wanaonekana hawaitakii mema nchi hii; wananyanyasika, hata wakipata matatizo wanachekwa, wamerundikiwa kesi lukuki kila kukicha mahakamani mara polisi yaani hata zile haki zao za kikatiba wananyimwa na Watanzania wanaona sawa tu.
Hivi tumesahau hata Rais huyu wa sasa CCM walilazimika kumpa nafasi ya kugombea 2015 kutokana na kuwepo Upinzani imara (UKAWA)?
Hivi tunadhani hii shauku na moyo wa kujituma alionao Rais na CCM kwa Watanzania siku upinzani ukifa moyo huo utakuepo?
Hivi tunadhani kwamba hawa wanasiasa wa Upinzani ambao wamekuwa wakijitoa kila kukicha kuishauri serikali, kuikosoa na kuipa changamoto za fikra za kimaendeleo wakisema wote wahamie CCM watakosa ulaji?
Hivi kweli Tundu Lissu akiamua kuwa kama Dr. Slaa atapoteza nini? Hivi Zitto akiamua kuwa kama Prof Kitila atapoteza nini? Hivi Mbowe akiamua kuwa kama Mrema atapoteza nini!?
Saivi kila msanii anaimba wimbo wa kuwazodoa upinzani kama vile wanamlani shetani.
CCM hii bila upinzani imara itabweteka, itatunyanyasa Watanzania, watatuibia sana hawa. Hivi vinavyofanyika saivi vilitakiwa vifanyike kipindi cha CCM ya Nyerere.
Watanzania kuna siku tutakuja kujuta. Wapinzani walipaswa wapewe moyo kwani wana mchango mkubwa sana katika hili Taifa.
Hivi tumesahau hata Rais huyu wa sasa CCM walilazimika kumpa nafasi ya kugombea 2015 kutokana na kuwepo Upinzani imara (UKAWA)?
Hivi tunadhani hii shauku na moyo wa kujituma alionao Rais na CCM kwa Watanzania siku upinzani ukifa moyo huo utakuepo?
Hivi tunadhani kwamba hawa wanasiasa wa Upinzani ambao wamekuwa wakijitoa kila kukicha kuishauri serikali, kuikosoa na kuipa changamoto za fikra za kimaendeleo wakisema wote wahamie CCM watakosa ulaji?
Hivi kweli Tundu Lissu akiamua kuwa kama Dr. Slaa atapoteza nini? Hivi Zitto akiamua kuwa kama Prof Kitila atapoteza nini? Hivi Mbowe akiamua kuwa kama Mrema atapoteza nini!?
Saivi kila msanii anaimba wimbo wa kuwazodoa upinzani kama vile wanamlani shetani.
CCM hii bila upinzani imara itabweteka, itatunyanyasa Watanzania, watatuibia sana hawa. Hivi vinavyofanyika saivi vilitakiwa vifanyike kipindi cha CCM ya Nyerere.
Watanzania kuna siku tutakuja kujuta. Wapinzani walipaswa wapewe moyo kwani wana mchango mkubwa sana katika hili Taifa.