Amiliki
JF-Expert Member
- May 6, 2011
- 2,085
- 1,004
Enyi Wabunge wa CCM, hivi hamjui kwamba mnachezewa kete ya hatari na Chadema ili mbele ya macho ya Watanzania muonekane kwamba hamna maana! Siku mtakapokuja kustuka itakuwa too late! Wanachokifanya Chadema ni kuleta hoja ambazo zina-reflect kilio cha Wananchi lakini nyie kwa Upofu wa kusahau wajibu wenu kama wabunge, mmeingiza ushabiki wa Kichama kwa kutetea kila kitu cha Serikali wakati wajibu wenu ni kukaa upande wa Wananchi waliowachagua ili kuibana Serikali. Kwa kufanya mnachokifanya kumepelekea sisi wananchi kuona kwamba kuna Watetezi wetu ambao ni Chadema wapo upande wetu wananchi tukipambana na Serikali wakisaidiwa na Wabunge wa CCM kwa upande wa pili. Kwa kifupi mnadhani mnajenga kumbe mnabomoa.
Ngojeni matokeo mtayaona 2015.
Ngojeni matokeo mtayaona 2015.