Hivi ni kweli serikali ya CCM haiwajali wananchi wake??

mva

Member
Dec 18, 2013
13
4
Nasikitishwa na kauli iliyotolewa na nchimbi kuwa hakuna tume huru itakayoundwa kuchunguza mlipuko wa bomu la soweto arusha . Kauli hii ilinifanya niamini kuwa kunakitu serikali inakijua kuhusiana na mlipuko ule .ukusikia nchi za wenzetu wanavyopambana kulinda raiya wake utafadhaika sana na kauli hizi za serikali nakumbuka wakati bom lilipolipuka, waziri wa nchi alilitangazia taifa kuwa chadema ndio wamejilipua wenyewe akafuatiwa na mwigulu nchemba kwa kauli hiyohiyo cdm wao wakatoka na kauli kuwa serikali inahusika na bomu lile na ushahidi wanao wanachotaka ni tume huru ili wakabizi ushahidi sasa kutokana na malumbano haya nilitegemea serikali ifanye mambo matatu kwa wananchi wake 1. Nilitegemea serikali iwakamate hao wanacdm waliolipua bom ili kuwadhihirishia wananchi kuwa cdma ndio inayouwa watanzania hivyo sio chama cha kukishabikia
2. Nilitegemea serikali iunde hiyo tume huru ili kuwahakikishia wananchi kuwa hawahusiki na ulipuaji huo wa bomu
3. Nilitegemea serikali iunde tume huru ili kuwahakikishia wananchi kuwa si kweli kuwa cdm wanamfahamu aliyerusha bomu na si kweli kuwa cdm wana ushahidi.
Kwakufanya hivyo serikali ingejisafisha na matope haya wanayopakwa na cdm hivyo kuendelea kungara mbele ya wananchi na pia ingewahakikishia wananchi kuwa cdm sio chama cha ukeli na ni chama hatari hivyo kukifanya kichukiwe na wananchi jambo ambalo lingekiinua ccm lakini kwa kauli hii ya nchimbi serikali imezidi kujigaragaza kwenye matope hivyo kiifanya cdm izidi kupendwa

naomba kuwasilisha.
 
itafika pahala hata ukienda chooni kujisaidia unataka serkal ije ikutawaze.shame on you
 
itafika pahala hata ukienda chooni kujisaidia unataka serkal ije ikutawaze.shame on you

nakusikitikia kwasababu ushabiki umekuathiri,kwahiyo swala la watu kupoteza maisha pale soweto wewe umelifananisha na mtu kwenda chooni?mungu akusamehe hujitambui
 
Ngoja kasi ya kuwamaliza watu aina ya Mabina iongezeke tutasikia tume huru zinaundwa
 
ngoja kasi ya kuwamaliza watu aina ya mabina iongezeke tutasikia tume huru zinaundwa
kweli kabisa nadhani hilo ndilo serikali inalisubiri. Serikali isiyoons matatizo ya nchi sijui wanaongoza nini
 
itafika pahala hata ukienda chooni kujisaidia unataka serkal ije ikutawaze.shame on you

Wewe hujitambui,unaandika kama umepalia mpini wa wanaume na umeishaingia ndani. Yaani unafanya dhihaka na maisha ya watu kuuwawa kinyama na policcm? So long as unaishi yatakuja kukuta tu,hiyo ni laana. Nyo.ko wewe,embu jitambue!
 
itafika pahala hata ukienda chooni kujisaidia unataka serkal ije ikutawaze.shame on you

hvi kama uhalifu unatokea mbaya zaidi mbele ya vyombo vya dola..then mnagoma kufanya uchngzi na kutoa taarifa ya kilichotokea...hv kweli hapo waonaje weye? watzania wana mamlaka ya kujiswafi wakienda toilet ila hawana mamlaka ya kufanya uchnguzi wa uhalifu...amasivyo kusingekuwa hata na haja yakuwa na vymbo vya dola. unapojaribu kutetea ni vyema ukatafakari unachokitetea na namna unavyo present utetez wako. ile ni damu ya wtzania ilimwagika au uwewaz kuwa tzania ni ya wapenz na washbk wa chama chako tuu...TANZANIA KWANZA..UTU KWANZA..tafakari
 
Nchimbi siyo tu ametoa kauli, bali pia amedhihirisha dharau yake kwa watanzania maskini waliotaka kujua ukweli kupitia uchunguzi wa tume huru.
Sijiu kwanini serikali inaona ugumu kuunda tume huru ya kijaji
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom