Hivi ni kweli Net zinatunkinga na malaria?

akoe

New Member
Feb 6, 2008
3
0
nimekuwa nikiperuzi mara kwa mara kuhusu mada za kila siku za wana JF.nakosa raha zaidi ninapoona hakuna mabadiliko yoyote yanayofanyika licha ya malalamiko kuhusu EPA,TICS,Kiwira,ATCL na mengine mengi.Labda tuseme tunapiga tu gita lakini mbuzi(Sirikali) hana hata mpango wa kuelewa na kucheza ngoma yetu.

Mimi nimeamua kwa mara ya kwanza kabisa nizungumzie mambo ya afya.inabidi tukubali kwamba malaria inaua na inatisha zaidi ya Ukimwi.ila naskitika sana nikskia hatua zinazochukuliwa na vyombo husika.Pia sikubaliani na baadhi ya kauli zinazoitwa za wataalam kuhusu malaria.Hivi kweli NET(chandarua) zinaweza kuondoa ugonjwa huu ambao ni hatari hapa nchini, au ni kuganja njaa,au tunataka tuwe wateja wa mbu na chandarua?

Ukiangalia kiasi cha pesa zinazotumiwa na serikali na pamoja na misaada haioneshi mafanikio yaliyo makubwa sana.N bado wala hakuna dalili za kupambana kutokomeza kabisa gonjwa hilihatari.

Mimi nilitarajia Serikali iziwezeshe halmashauri zote nchini kupambana na mazalia ya mbu na sio kuwekeza kwenye viwanda vya NET(chandarua).pesa hizi nyingi zingetumika kusafisha na kunyunyizia dawa mazingira yanayotuzunguka katika kila muda maalum,natumai tungekuwa tumepiga hatua moja kubwa sana ktk kupamba na ugonjwa huu.

Kuna kauli ambazo nimetangulia kuziita zinaitwa za kitaalam kuhusu mbu eti,"mbu anaye ambukiza malaria ni jike na anauma usiku wa manane", sidhani kama ina ukweli,yaani mbu wanaambiana "jamaani eeh usiku wa manane umefika" hivi inaingia akilini?hizi ni kauli za kuwataka watu wadhani malaria yanaambukizwa kitandani tu ilihali mbu ni mdudu wa shari hata mchana kweupe anauma bila haya.

nawaomba wana habari wote mlipe mtazamo wa kipekee wazo langu hili,wana JF tusaidiane kubadili mkandamizo wa mawazo kwa jamii mpaka mbu wajue wanachukiwa na sio kuwaacha wanatamba wanazaliana eti kwa vile ninayo chandarua.

Karibuni
 
Net haikingi ila inapunguza maambukizo na kuenea kwa malaria. Fikiria kama last form of defence. Sasa labda huu ni mwanzo na huko mbeleni watafanya kazi ya kuweka dawa kwenye mzaingira kama unavyo suggest. Mimi mwenyewe ningependa sana nilale bila net na mbu wote watoweke.
 
kama neti inakinga malaria basi ni very small percentage.
Haya mambo ya neti ni kunufaisha miradi ya watu na wazungu wanajua fika neti ni kudumaza na kufanya malaria iendelee kuwa sugu ili waendelee kutuuzia madawa yao kina arinate, metakelfin and God knows what.

My take:
Serikali isimamie kodi za wananchi kwa kuboresha makazi ie kuhakikisha mitaro ipo, inapitisha maji na maji hayatuami.

Warudishe ule mfumo wa miaka ya 80 ya kufanya fumigation mtaa kwa mtaa kwenye septic tanks na chambers. I remember by then we were not sleeping on this stupid net materials, mbu were there but very few.

Kila mtu kwa nafasi yake ahakikishe mazingira yake yapo safi, akate nyasi, kusiwe na maji yanayotuama wala matakataka kupunguza uwezekano wa mazalia ya mbu. Kama tunaweza kuafford tuweke mosquito wires on our windows.


very last, last option ndio iwe net lakini tuking'ang'ana nahii mineti bila kufight vyanzo vya mazalia tutakuwa tunatwanga maji.

by the way, miaka ile kulikuwa na research moja ilifanyika maeneo ya Tanga Bombo if am not mistaken where people were vaccinated against malaria and it is said those who got vaccinated have never caught malaria ever since, what happened to that research?au ndio one of the masharti from super countries?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom