pomo
JF-Expert Member
- Jun 26, 2011
- 267
- 31
niaje wana jf, mimi ni kijana wa miaka 28, mnamo mwaka 2002 nilikuwa na mpenzi wangu wa kike alikuwa kamaliza A level na mimi nilikuwa nimemaliza o level na nilikuwa nafanya kazi za vibarua(kazi zisizo na ujuzi).wakati anamaliza shule nilimuahidi nita mnunulia zawadi za sherehe. kwa bahati mbaya sikupata fedha na mawasiliano yalikuwa ni barua kwa wakati huo na sikuweza kumjulisha. matokeo yake ya A level yalipotoka alikuwa amefaulu kwa kupata division 1, baada ya hapo alianza visa na kusema mimi ni bahili na siwezi kupata mwanamke kama nikiendelea hivi. chakushangaza ni kuwa nilikuwa namsaidia hapo mwanzo na bado ninampenda hadi hii leo. kuna siku nilikutana nae(2008) akiwa kamaliza chuo, nilijaribu kumwambia bado nampenda lakini yeye akasema eti wakati ule alikuwa bado mdogo na hakuwa na maamuzi na mimi nataka kumlipizia kisasi, anasema nimpe muda wa kujifikiria. mimi najiuliza ni kweli alikuwa hana maamuzi wakati huo? je amekuwa na jeuri hiyo baada ya yeye kufaulu A level nakuwa na uhakika wa kwenda chuo? na mimi ni kibarua sina muelekeo? mimi sikuwa na nia ya kulipa kisasi