Hivi ni kweli "msema kweli ni mpenzi wa Mungu"?

Musundi

JF-Expert Member
Dec 21, 2016
1,583
2,600
Mwenzenu niko njia panda kabisa hata sijui lipi ni lipi sasa. Toka utotoni nilizoea kusikia msemo huu na niliamini huo ndo ukweli maana siamini Mungu anaweza kumpenda Msema-uongo
Na hata sasa msemo huu bado umetamalaki.

LAKINI mbona kivitendo tunafanya kinyume chake kabisa?!! Au zama hizi kuna wanaoruhusiwa kusema ukweli na wengine kusema ukweli ni haramu?

Nimeshangaa kukuta taarifa huko TWITTER ati jalada limefunguliwa kwa ajili kuwashtaki wanaosambaza picha mitandaoni za vitabu vilivyochapishwa vikiwa na makosa.

Labda nasumbuliwa na ujinga wa kutojua sheria. Lakini najiuliza tu: Hizi picha ni za kweli au wanaozisambaza wamezusha tu uongo kwa nia ovu? Kama ni za kweli mchapishaji alikosea, anayejaribu kulionesha kosa hilo ana hatia gani? Sio MSEMA-KWELI huyu?

Naomba kuelimishwa na wajuzi wa sheria.
 
Kwasasa hii nchi ilipo fikia nikwamba, ukisema ukweli utakua umetenda kosa la jinai.
 
Nitasema bila kupindisha ,,,,,,Jambo kama hili ndo linafanya serikali ihangaike kuthibiti mitandao ya kijamii na Uhuru wa vyombo vya habari,,,,,lengo Lao ni kuficha madudu wanayofanya!... ,,uuozo wafanye wao halafu wawasake wengine?.. Kwa nini wasidili na hao wandaaji?.. . Na kwa. Upuuzi hivi vitabu vipo tayari mashuleni,,,, kwa hiyoo mlitaka tusiseme au!.....HII NI NCHI YETU SOTE
 
Selikali ya awamu ya tano ni yakipuhuzi sana kwa sababu inapenda kusifiwa kuliko ata kukosolewa
 
FB_IMG_1525551940691.jpg
 
Hata mjengoni kwa utawala huu ,si ajabu wakabadili sheria kuwabana zaidi na kuondoa kinga kwa wabunge.
Yananayotusibu na yajayo yanasikitisha.
 
Mwenzenu niko njia panda kabisa hata sijui lipi ni lipi sasa. Toka utotoni nilizoea kusikia msemo huu na niliamini huo ndo ukweli maana siamini Mungu anaweza kumpenda Msema-uongo
Na hata sasa msemo huu bado umetamalaki.

LAKINI mbona kivitendo tunafanya kinyume chake kabisa?!! Au zama hizi kuna wanaoruhusiwa kusema ukweli na wengine kusema ukweli ni haramu?

Nimeshangaa kukuta taarifa huko TWITTER ati jalada limefunguliwa kwa ajili kuwashtaki wanaosambaza picha mitandaoni za vitabu vilivyochapishwa vikiwa na makosa.

Labda nasumbuliwa na ujinga wa kutojua sheria. Lakini najiuliza tu: Hizi picha ni za kweli au wanaozisambaza wamezusha tu uongo kwa nia ovu? Kama ni za kweli mchapishaji alikosea, anayejaribu kulionesha kosa hilo ana hatia gani? Sio MSEMA-KWELI huyu?

Naomba kuelimishwa na wajuzi wa sheria.
Usiwe njiapanda, usemakweli hujipi mwenyewe bali unaowaambia ndiyo watakaokuita wewe ni msemakweli, siku zote muwamba ngoma kamba huvutia kwake.
 
Yaani mtoa taarifa anasakwa kama mhalifu,, hivi kweli mama yangu joyce ndalichako, huyu mtoa taarifa asigetoa taarifa hiki si wangefudishiwa watoto wetu mashuleni?? Chonde chonde mama yangu nakuomba umsake mchapishaji wa kitabu na umpongeze mtoa taarifa ili siku nyingine awe na moyo wa kutoa taarifa.
 
Yaani mtoa taarifa anasakwa kama mhalifu,, hivi kweli mama yangu joyce ndalichako, huyu mtoa taarifa asigetoa taarifa hiki si wangefudishiwa watoto wetu mashuleni?? Chonde chonde mama yangu nakuomba umsake mchapishaji wa kitabu na umpongeze mtoa taarifa ili siku nyingine awe na moyo wa kutoa taarifa.
Hii ndiyo hekima yenyewe kiukweli. Kinyume cha hapo ni siasa za maslahi binafsi!
 
Back
Top Bottom