Rufaro
JF-Expert Member
- May 7, 2022
- 222
- 340
Mbona sasa maisha ya mtanzania yanazidi kua magumu, au ile kauli ya tuhamie burundi walikua wanamanisha.. tuhamie Burundi ili wazidi kujineemesha wao kupitia rasilimali za nchi hii
Mtanzania umkamue roho kupitia tozo, bado tena usimpe umeme wa uhakika ( umuibie), hapo hapo umpandishie bidhaa haswa vyakula, kwamba unataka tufe tu mana chakula ndio uhai, umeona haitoshi sasa unamuibia MAJI na tunavyojua maji ni uhai. Sithubutu kuzungumza kwenye ajira na kodi utitiri kwenye biashara, bado sijathubutu kuzungumzia miradi mikubwa ya JPM ambayo ghafla imeanza kusuasua.
Ni kweli wananchi hatuhitajiki nchi hii? Dah , wakati haya yanatokea hua sauti marehemu JPM ya "mtanikumbuka" hua inajirudia masikioni mwangu..embu kila mtanzania ambaye anaumizwa na haya apige goti tuwashtakie kwa Mungu hawa wadhalimu.
Malipo ni hapa hapa duniani.
Mtanzania umkamue roho kupitia tozo, bado tena usimpe umeme wa uhakika ( umuibie), hapo hapo umpandishie bidhaa haswa vyakula, kwamba unataka tufe tu mana chakula ndio uhai, umeona haitoshi sasa unamuibia MAJI na tunavyojua maji ni uhai. Sithubutu kuzungumza kwenye ajira na kodi utitiri kwenye biashara, bado sijathubutu kuzungumzia miradi mikubwa ya JPM ambayo ghafla imeanza kusuasua.
Ni kweli wananchi hatuhitajiki nchi hii? Dah , wakati haya yanatokea hua sauti marehemu JPM ya "mtanikumbuka" hua inajirudia masikioni mwangu..embu kila mtanzania ambaye anaumizwa na haya apige goti tuwashtakie kwa Mungu hawa wadhalimu.
Malipo ni hapa hapa duniani.