Askarimtu
JF-Expert Member
- Sep 7, 2019
- 277
- 185
Katika mihangaiko ya hapa na pale nimeona kitu hiko hapo juu, ambacho kweli sijawahi kupata ushuhuda/ habari za maana ili kukiamini.
Lakini nikakumbuka kuwa mwaka fulani niliambiwa kuwa katika shule moja ya wasichana ya bweni, kuna msichana alikuwa ni mwanamke kwa nje lakini kwa ndani ni mwanaume ila baadhi ya wenzie walimfichia hii siri kwa sababu zao wenyewe, na wala walimu hawakujua hii kitu. Nikamuuliza yule aliyekuwa ananiambia, ''wewe, ni hapa hapa Tanzania au?''' Mara nikaona stori imepeperuka na upepo, lakini hiki kitu nilikiweka kichwani japo sikukiamini mpaka leo siamini.
Juzi tu hapo, nimeona pia habari kuna msichana kafanyiwa upasuaji ili kukamilisha sehemu yake ya kiume iliyoota juu ya sehemu ya kike; Uganda.
Ukiacha hizo hapo juu, kuna jamaa katika mtandao mmoja amesema kuwa; kuna msichana wa kazi alidai kuwa amepewa mimba na boss wake wa kike, watu wakamwambia wewe umechanganyiwa, hakuna kitu kama hicho; msichana akajibu ni kwasababu hamjui kama boss wangu ni mwanaume kwenye viungo lakini ni mwanamke kwa mwonekano (nywele ndefu, matiti, nyonga, sauti, mwendo)
Sasa: Madaktari kama hi hali ipo kweli, hii hali inasababishwa na nini? Na, kama watu hawa wapo kweli katika jamii wanatambulikaje au ndio wanafichwa tu?
Assume sasa, kijana ndio kakutana na huyu bidada wa aina hii na kampenda kwelikweli; na vijana wa sasa hivi tulivyo ving'ang'anizi, daah!
Nasikia pia katika Uislamu kuna kitu kinaitwa KHUNTHA ndicho kinachowatambulisha watu wa aina hii (sina uhakika).
Ambao mmeshakutana au kusikia habari hizi tusaidieni kutoa stori zenu labda tutapata picha kamili kwa mawazo ya wengi!
NB: Nataka elimu tu na taarifa, sipo katika kukejeli kundi fulani la watu.
Lakini nikakumbuka kuwa mwaka fulani niliambiwa kuwa katika shule moja ya wasichana ya bweni, kuna msichana alikuwa ni mwanamke kwa nje lakini kwa ndani ni mwanaume ila baadhi ya wenzie walimfichia hii siri kwa sababu zao wenyewe, na wala walimu hawakujua hii kitu. Nikamuuliza yule aliyekuwa ananiambia, ''wewe, ni hapa hapa Tanzania au?''' Mara nikaona stori imepeperuka na upepo, lakini hiki kitu nilikiweka kichwani japo sikukiamini mpaka leo siamini.
Juzi tu hapo, nimeona pia habari kuna msichana kafanyiwa upasuaji ili kukamilisha sehemu yake ya kiume iliyoota juu ya sehemu ya kike; Uganda.
Ukiacha hizo hapo juu, kuna jamaa katika mtandao mmoja amesema kuwa; kuna msichana wa kazi alidai kuwa amepewa mimba na boss wake wa kike, watu wakamwambia wewe umechanganyiwa, hakuna kitu kama hicho; msichana akajibu ni kwasababu hamjui kama boss wangu ni mwanaume kwenye viungo lakini ni mwanamke kwa mwonekano (nywele ndefu, matiti, nyonga, sauti, mwendo)
Sasa: Madaktari kama hi hali ipo kweli, hii hali inasababishwa na nini? Na, kama watu hawa wapo kweli katika jamii wanatambulikaje au ndio wanafichwa tu?
Assume sasa, kijana ndio kakutana na huyu bidada wa aina hii na kampenda kwelikweli; na vijana wa sasa hivi tulivyo ving'ang'anizi, daah!
Nasikia pia katika Uislamu kuna kitu kinaitwa KHUNTHA ndicho kinachowatambulisha watu wa aina hii (sina uhakika).
Ambao mmeshakutana au kusikia habari hizi tusaidieni kutoa stori zenu labda tutapata picha kamili kwa mawazo ya wengi!
NB: Nataka elimu tu na taarifa, sipo katika kukejeli kundi fulani la watu.