Hivi Ni Kweli Kabisa TABIA Haina Dawa??.....hebu tujadiliane!!

SnowBall

JF-Expert Member
Sep 13, 2011
3,054
2,840
Kuhusu dhana ya TABIA waswahili wana misemo mingi tu...mfano kuna msemo kama 'TABIA NI KAMA NGOZI HAIBADILIKI'....lakini hawajaishia hapo tu wakati mwingine utasikia msemo kama 'MAZOEA HUJENGA TABIA'...Hizi zote ni semi zinazobeba MAANA kubwa tu, na zote ukizifuatilia kwa Makini utaona zinaongelea kitu kile kile... Binafsi naamini kuwa TABIA inaweza kubadilika au mtu mwenye TABIA flani anaweza badilishwa na ninawashangaa wanaosema haiwezekani!!...kwa mfano ninaamini TABIA hujengwa na kama kitu kinajengwa naamini pia kinaweza KUBOMOLEWA!!!...Unaweza ukajijengea TABIA ya Ulevi na ukawa MLEVI lakini kupitia mafundisho na maonyo unaweza kuacha ulevi na ukawa mtu safi kabisa..

Kinachonisukuma kuandika hii thread ni tabia flani ambazo nimeziona kwenye MAHUSIANO...Unakuta mwenzio ana katabia flani ambako labda kanakukera na uzuri au ubaya ukute hata yeye mwenyewe anakiri kuwa hiyo ni TABIA yake...na labda ukiongea naye Utasikia anakuambia NIZOEE tu hii ni TABIA yangu..Sasa Jamani wanaJAMVI....Hivi ni KWELI KABISA KUNA TABIA HAZIWEZI BADILIKA!!!...Na kama jibu ni NDIYO..Hivi sasa utaishije na mtu ambaye ameshakiri kuwa hawezi badilika????...Hainihusu personally but nimeona nishee uzoefu wenu kupitia hili!!!..Na swali langu ni hili...''Ni kweli TABIA HAINA DAWA''??????............
 
Mkuu ahsante kwa maada nzuri,

Najua siyo vema kuuliza swali juu ya swali lakini kuna mjadala kama huu niliwahi kuukuta nikajikuta unaniachia maswali na hapa nisingependa kujichanganya kwanza kabla sijapata mawazo ya wadau hapa juu ya swali kama hili.....

Kuna tofauti gani kati ya "TABIA" na "HULKA" au vyote ni kitu kimoja?
 
Ahsante mkuu nadhani utakuwa tu umepanua WIGO wa MJADALA...na kama wadau watatiririka basi tunaweza kuchora mstari kati ya TABIA na HULKA...Binafsi hata mimi natatizwa na haya makitu....

Mkuu ahsante kwa maada nzuri,

Najua siyo vema kuuliza swali juu ya swali lakini kuna mjadala kama huu niliwahi kuukuta nikajikuta unaniachia maswali na hapa nisingependa kujichanganya kwanza kabla sijapata mawazo ya wadau hapa juu ya swali kama hili.....

Kuna tofauti gani kati ya "TABIA" na "HULKA" au vyote ni kitu kimoja?
 
Ahsante mkuu nadhani utakuwa tu umepanua WIGO wa MJADALA...na kama wadau watatiririka basi tunaweza kuchora mstari kati ya TABIA na HULKA...Binafsi hata mimi natatizwa na haya makitu....

Ni kweli wakati mwingine ni muhimu kuanzia mahali kama hapa kwa sababu kuna kimoja ni "social construct" na kingine ni "nature" (japo tafsiri yake huwa inanipa tabu kidogo ya hili neno nature) na kwa kutambua huwa naona kama itarahisisha kupata jibu sawia MAANA KUNA WAKATI unaweza kutaka kum-mend mtu ukajikuta unakata tamaa maana "Tabia haina dawa" na ni "sawa na ngozi kwenye mwili"
 
Kuna Tabia mtu alikuwa nayo Babu yake,Baba yake na yeye mwenyyewe...
utambadili utaweza?...

Binafsi naamini njia ya kumbadili mtu ni kuanza utotoni..

na sometimes kuchanganya damu...

kama ukoo wenu mna tabia za uvivu na kuuupalilia umasikini....basi nenda kaoe mbaali huko
ikiwezekana nje ya kabila....ili watoto wasiathirike na tabia hizo..

Kwenu wagogo....kaoe wachaga na kadhalika...lol
 
Kuna Tabia mtu alikuwa nayo Babu yake,Baba yake na yeye mwenyyewe...
utambadili utaweza
?...

Binafsi naamini njia ya kumbadili mtu ni kuanza utotoni..

na sometimes kuchanganya damu...

kama ukoo wenu mna tabia za uvivu na kuuupalilia umasikini....basi nenda kaoe mbaali huko
ikiwezekana nje ya kabila....ili watoto wasiathirike na tabia hizo..

Kwenu wagogo....kaoe wachaga na kadhalika...lol

Mkuu The Boss, hivi hii itakuwa ni "Tabia" au ni "Hulka"
 
Mkuu naona umekuja na SOLUTION Kabisa..but nilichotaka kabla haujahitimisha ni kuona kwamba Je? Kuna mazingira ambamo mtu anakiri kabisa kuwa kwa hili siwezi BADILIKA!!...yaani kwamba na yeye kesha give-up

Kuna Tabia mtu alikuwa nayo Babu yake,Baba yake na yeye mwenyyewe...
utambadili utaweza?...

Binafsi naamini njia ya kumbadili mtu ni kuanza utotoni..

na sometimes kuchanganya damu...

kama ukoo wenu mna tabia za uvivu na kuuupalilia umasikini....basi nenda kaoe mbaali huko
ikiwezekana nje ya kabila....ili watoto wasiathirike na tabia hizo
..

Kwenu wagogo....kaoe wachaga na kadhalika...lol
 
Dhana ya 'Social Construct' na 'Nature' nimeipenda....

Ni kweli wakati mwingine ni muhimu kuanzia mahali kama hapa kwa sababu kuna kimoja ni "social construct" na kingine ni "nature" (japo tafsiri yake huwa inanipa tabu kidogo ya hili neno nature) na kwa kutambua huwa naona kama itarahisisha kupata jibu sawia MAANA KUNA WAKATI unaweza kutaka kum-mend mtu ukajikuta unakata tamaa maana "Tabia haina dawa" na ni "sawa na ngozi kwenye mwili"


Mkuu Cathode Rays kuna kitu Ngabu kaongeza hapa chini...hebu jaribu kuona kama kajibu hilo la HULKA...yeye kalipeleka kwenye DNA....

Kuna mambo mengine huwa yapo kwenye DNA na mojawapo ni baadhi ya tabia za mtu.

Hivyo ni vigumu sana kuyabadilisha.
 
Last edited by a moderator:
TABIA = Mazoea yanayotokana na kurudiarudia hali, mwenendo au matendo

HULKA = Tabia ya mtu, mwenendo wa mtu, maumbile. Pengine huluka.

Kwa mujibu wa Kamusi ya Kiswahili sanifu
 
Nakubaliana na The Boss na Nyani Ngabu

Naamini wamekujibu vizuri sana, labda tu niongeze kuwa inawezekana kabisa mtu kubalidilika kama ana tabia mbaya, kwani ile kujua kuwa una tabia mbaya ambayo inalalamikiwa na watu waliokuzunguka ni hatua mojawapo ya kuelekea kubadilika, iwapo utaamua kufanya hivyo.

Ni pale tu utakapokuwa na dhamira ya dhati ya kubadilika ndipo utakapofanya hivyo.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu naona umekuja na SOLUTION Kabisa..but nilichotaka kabla haujahitimisha ni kuona kwamba Je? Kuna mazingira ambamo mtu anakiri kabisa kuwa kwa hili siwezi BADILIKA!!...yaani kwamba na yeye kesha give-up

Kwa mujibu wa TB ambao naona ndio ukweli ni kuwa huyo mtu anakuwa mtumwa wa tabia yake au tuseme ndio inakuwa hulka, kwamba ndivyo alivyo toka kwenye mizizi hata yeye anajishangaa.
 
Kimsingi hakuna tabia ambayo haiwezi kubadilika ikifanyiwa kazi. Ila urahisi au ugumu wa kubadilika tabia inategemea mzizi wa tabia yenyewe ulivyojikita ndani ya nafsi ya mtu. Kwa mfano kuna tabia za kurithi kutoka kwa wazazi, mf. hasira, ukali, nk. Hizi ndo tabia-hulka (nature). Tabia hizi zina mzizi mrefu sana, ili mtu aweze kubadilika anahitaji kusaidiwa sana, kutumia nguvu nyingi na njia nyingi, mazoezi mengi, na pia muda mrefu wa kutosha. Hata hivyo mtu hatabadilika kwa asilimia 100 lakini anaweza ku-improve.

Kuna tabia si za kurithi ila mtu kazipata kwenye mazingira aliyopitia mf. shuleni, vikundi vya marika, nk. Tabia hizi zina mizizi si mirefu sana japo zinaweza zikawa zimemkolea sana mhusika. Hizi zaweza kubadilika kirahisi kidogo ukilinganisha na zile za kwanza kwani hizi ni za kujifunza. Mtu akitumia nguvu, akajitahidi na kusaidiwa na wengine anaweza kubadilika.

Mtu anayekimbilia kusema: "we niache tu ndo tabia yangu" ni mtu aliyekata tamaa kufanya safari ya mabadiliko. Ni mtu anayetafuta udhuru, na asiye tayari kuumia ktk zoezi zima la kujibabadua na tabia yake (au kilema chake). Ni mvivu au mtu mwenye majivuno.
 
TABIA = Mazoea yanayotokana na kurudiarudia hali, mwenendo au matendo

HULKA = Tabia ya mtu, mwenendo wa mtu, maumbile. Pengine huluka.

Kwa mujibu wa Kamusi ya Kiswahili sanifu

Kwa hiyo mkuu kwa Lugha hii nikijumlisha na alichosema Nyani Ngabu hapo juu ninaweza kupata picha kuwa

Hulka - ni nature au ambacho NN anaita kama genetic thing kwa maana ya kitu kinachorithishwa toka kizazi kimoja hadi kingine. Sawa na alichosema The Boss kwamba unakuta jamii fulani by nature ni wavivu au jamii fulani by nature hawatulii kwenye ndoa and other predispositions

Tabia - Hii ni social construct ambayo mtu anatengenezewa na jamii iliyomzunguka lakini it has nothing at all to do with his/her "nature/genetic" thing.....Mfano mtu anaweza kuwa mlevi kwa kuwa yuko exposed na walevi, au mtu anaweza kuwa mpenda ngono sana kwa kuwa amaezungukwa na wafanya ngono sana au mtu anaweza kuwa mvuta sigara kwa kuwa kampani yake iko hivyo

Saying so, na kama niko sahihi kwenye assumptions zangu hapo juu, basi inamaana kuwa "Hulka" ni ngumu sana ku-deal nayo lakini "tabia" inaweza kudhibitiwa ikiwa mtu atakuwa exposed kwenye mazingira ambayo yataondoa zile tabia ambazo awali zilitengenezwa na mazingira "environments" tofauti

Stand to be corrected hapa
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom