Hivi ni kweli bodi (HESLB) haina fedha?

Page 94

JF-Expert Member
Oct 22, 2015
5,205
15,162
Salaam Wakuu,

Hii imekuwa ni tofauti kama utaratibu unavyopasa. Kikawaida,wanufaika wote wa mikopo kutoka HESLB wamekuwa wakipewa fedha za kujikimu kila baada ya siku 60 yaani miezi miwili. Lakini mpaka sasa kuna vyuo ambavyo imeshapita mpaka miezi mitatu na huu tunaelekea wa 4 (yaani mwezi mmoja mbele zaidi ya kipindi kinachopaswa) hakuna fedha za kujikimu kwa wanufaika.

Kila jitihada zinapofanyika bodi wanadai fedha hakuna mpaka wazipate kutoka hazina. Sasa cha kujiuliza,je hazina haioni umuhimu wa kutoa hizi fedha? Je,ni kweli hazina haijatoa fedha au bodi ndo inazingua?

Hali imekuwa mbaya vyuoni. Hakuna pesa kwa ajili ya matumizi ya chakula. Mbaya zaidi kuna wengine wanategemea kutumia fedha hizo kwa ajili ya kulipia ada (sehemu iliyobaki). Mitihani inatarajia kuanza wiki ijayo na wale ambao hawajakamilisha malipo ya ada hawaruhusiwi kufanya mitihani.

Jamani,Hazina tunaomba roho ya huruma iwaingie. Hizi fedha hatuzipati kama msaada. Ni za kuzirudisha tena ikiwa na riba. Hii ni haki yetu ya Msingi kabisa.

Dada zetu huku chuoni wanaangamia. Hatujui kinachowaweka mjini kwa sasa. Hakika kuna kitu kinaendelea nyuma ya pazia ambacho siyo kwa matakwa yao Bali ni hali mbaya ya kiuchumi inayotokana na kuchelewa kwa fedha hizo.

Mh Rais uliahidi kwamba wanafunzi watapewa fedha zao kwa wakati. Hazina ipo chini yako na hakika kauli yako ndo itawalazimu kutoa hizo fedha. Tunakuomba Mkuu wetu utusaidie. Hali inasikitisha.

Hata kupiga msuli hauingii. Madude hayapandi kichwani kwa sababu tumboni kupo empty.[/COLOR=RED]

Nimeandika kwa rangi nyekundu maana hakika Uzi huu ni wa masikitiko.
 
Ingekua vizuri kama ungetaja hivyo vyuo ambavyo mpaka sasa wanafunzi wake hawajapata mkopo... huwezi jua labda wale mashushu wa Mheshimiwa wanaweza wakapitia humu na kufikisha taarifa yako kwake.. .
 
Ingekua vizuri kama ungetaja hivyo vyuo ambavyo mpaka sasa wanafunzi wake hawajapata mkopo... huwezi jua labda wale mashushu wa Mheshimiwa wanaweza wakapitia humu na kufikisha taarifa yako kwake.. .
Vyuo ambavyo havijapata mkopo mpaka sasa ni TIA (DSM) ,MUHIMBILI na SAUT (sina uhakika Sana) na vyuo vingine vingi tu.
 
Kweli kabisa taja vyuo..usalama wamo huku kuwafatilia vijana wa CDM kwahiyo ni rahisi kuchukua taarifa na kupeleka panapousika
 
Miezi miwili hakuna boom, inawezekana itakuwa wanaendelea na uhakiki wa watumishi hewa kwa hiyo wamethitisha kila kitu!!!!!! Kazi mnayo.
 
Miezi miwili hakuna boom, inawezekana itakuwa wanaendelea na uhakiki wa watumishi hewa kwa hiyo wamethitisha kila kitu!!!!!! Kazi mnayo.
Mkuu uhakiki wameshafanya. Taarifa wanazotoa ni kwamba tuwe wavumilivu maana hazina ndo hawajawapa fedha. Hali ni mbaya sana mkuu!
 
sitawaangusha nitahakikisha mnapata mikopo tena kwa wakati..... september, 2015 kwenye kampeni morogoro
 
sitawaangusha nitahakikisha mnapata mikopo tena kwa wakati..... september, 2015 kwenye kampeni morogoro
Cha kushangaza ndo mikopo imechelewa zaidi Mara mbili ya inavyochelewaga.
 
hii hali inasikitsha sana kwenye suala nyeti kama hili unaingzwa mchezo mchafu wa siasa, ni kitu kinachohitaji kujitoa kidogo akili ili usadiki haya majawabu,eti hazina haijawapatia pesa HESLB wakati huohuo kuna vyuo washapata pesa zaoje hyo hazina haina pesa kwa hiv vyuo 30 tu? hadi sasa ni vyuo 30 havijapatiwa hzo pesa vikiwemo
-TIA (DSM)
-MHIMBILI
-SAUT
-AMUCTA(Tabora)

Kwa mfano TIA mitihani inatarajiwa kuanza next week na juz ndio ilkuwa deadline ya kulipa ada na wimbi kubwa la wanafunz lilikuwa linategemea kias kutoka kwenye hyo pesa kumalzia ada kwa sasa kimekuwa kitendawili,kuhusu maisha ya kila siku namaanisha pesa ya kula imekuwa mtihani mkubwa sana,plz wakubwa wenye uwezo tupenyezeen hz taarifa sehemu husika tafadhali huku hali sio hali
 
Ingekua vizuri kama ungetaja hivyo vyuo ambavyo mpaka sasa wanafunzi wake hawajapata mkopo... huwezi jua labda wale mashushu wa Mheshimiwa wanaweza wakapitia humu na kufikisha taarifa yako kwake.. .
Bodi wanadai vipo vyuo zaidi ya 15 havizidi 20.
 
hii hali inasikitsha sana kwenye suala nyeti kama hili unaingzwa mchezo mchafu wa siasa, ni kitu kinachohitaji kujitoa kidogo akili ili usadiki haya majawabu,eti hazina haijawapatia pesa HESLB wakati huohuo kuna vyuo washapata pesa zaoje hyo hazina haina pesa kwa hiv vyuo 30 tu? hadi sasa ni vyuo 30 havijapatiwa hzo pesa vikiwemo
-TIA (DSM)
-MHIMBILI
-SAUT
-AMUCTA(Tabora)

Kwa mfano TIA mitihani inatarajiwa kuanza next week na juz ndio ilkuwa deadline ya kulipa ada na wimbi kubwa la wanafunz lilikuwa linategemea kias kutoka kwenye hyo pesa kumalzia ada kwa sasa kimekuwa kitendawili,kuhusu maisha ya kila siku namaanisha pesa ya kula imekuwa mtihani mkubwa sana,plz wakubwa wenye uwezo tupenyezeen hz taarifa sehemu husika tafadhali huku hali sio hali
Hali ni mbaya kwa kweli. Lazima harakati za haraka zifanyike kulinusuru janga hili.
 
Ingekua vizuri kama ungetaja hivyo vyuo ambavyo mpaka sasa wanafunzi wake hawajapata mkopo... huwezi jua labda wale mashushu wa Mheshimiwa wanaweza wakapitia humu na kufikisha taarifa yako kwake.. .
Muhas, sfuchas, cuhas
 
Back
Top Bottom