hivi ni kwanini wengi walio kwenye relation huamini kuwa watu wengine wanawaonea wivu

Red Giant

JF-Expert Member
Mar 9, 2012
15,658
20,889
hasa zaidi ukisikiliza nyimbo utasikia. wanga watasema watachoka sisi tunasonga mbele, mara waache waseme, mara utasikia watakoma na roho zao, taarabu ndo usiseme! pia kwenye nyumba za kupanga/na uswahilini watu wanakua na mashaka kwamba wengine hawautakii mema uhusiano wao, utasikia ntadumu nae hata mkisema. kwanini watu wanakuwa hivi. inafika kipindi mtu anafanya mambo sio kwa kupenda bali ili awakoshe hao anaoona wanamuonea wivu. matatizo yakiwapata wanashindwa kusolve kwa kuamini eti vizabizabina ndo wamesababisha. hivi kuna ukweli katika hili? au ni mambo ya kujishuku. nini uzoefu wako katika hili?
 
Kwenye mahusiano yapo ambayo may be unaweza kufanya kuwaridhisha walimwengu kuwa hata mseme au mfanye lolote uhusiano wao uko imara
Kuna watu hawapendi kuona mahusiano baina ya watu wawili yanadumu na wanatafuta kila njia wahakikishe kuwa mahusiano hayo yanavunjika na ndo maana unakuta watu wanaongea mambo kama hayo waache waseme usiku watalala na watawaona wawikli hao wakidunda tuu
\haya mambo yapo sana
 
  1. kwani wewe huwaonei wivu waliokwenye mahusiano?
  2. kama wewe uko kwenye mahusiano, do you care what 'vizabizabina' think/say about you?
 
yapo sana, ndo yale yale mwanaume kwa upendo wake anaamua kumsaidia mke wake kazi fulani wanasema amepewa limbwata. walimwengu wanapenda kuona watu wanakorofishana kila siku, na hiyo ndo furaha yao.
 
Me nilimsimamia shoga yangu sherehe yake!!yaaan hadi mfanyakazi wa harusi ambaye hamjui mumewe mtarajiwa pia anamwonea wivu.
Mara hajampamba vizuri , mara lipstic kidogo! Ati anamwonea wivu kisa ye ndo anaolewa!! Na hakuwa hivi kabisa alikuwa anajiamini sana sijui hata nn kilimtokea.
 
Mi naona hapo tatizo ni lako we mwenyewe maana usingekuwa na maisha ya showoff usingejali sana hizo makitu au hizo mambo
ishu ya pili ni umaskini wako tu, ungekuwa na utajiri hasa wa elimu na ufahamu isingekuwa ishu kivile maana maarifaa yangekusaidia kwanza kujitambua pili kuelewa kuwa mahusiano ni ya kwako na si ya jamii so why keeping your ears on'em?
ishu ya tatu ni mahali unakoishi, hama uswazi mtu wangu, huko watu hawana kazi na pia hawana mikakati so kutwa kucha wanajadili watu badala ya maswala!! hizi makitu huwezi kuzisikia magetini au mitaa ya upper class, kila mtu na maisha yake na swaga zake
mwisho be you man and not others, live ya real facial and never mask
 
Wengi ufikiri wanapendwa sana tena kuliko wengine, pia ufikiri wengine hawapendwi kwa hiyo udhani wanaweza kuporwa.
 
  1. kwani wewe huwaonei wivu waliokwenye mahusiano?
  2. kama wewe uko kwenye mahusiano, do you care what 'vizabizabina' think/say about you?
kwanza siwaoneagi wivu watu na mahusiano yao ila unaweza muona jamaa anamke mzuri ukamtamani ila haimaanishai unamtakia mabaya! kwani ukitamani gari au nyumba ya mtu au tuseme kipaji chake inamaanisha unamtakia mabaya?. pia hao vizabizabina kuongea kwao ni kwa kawaida ila kama unajishukushuku ndo utahisi wanakutakia mabaya. sasa swali langu ni kwamba kwanini watu wanajishukushuku au ni kweli huwa wanaombewa mabaya?.
 
Back
Top Bottom