Hivi ni kwanini Watanzania ni waoga kufanya manunuzi Mtandaoni?

Mkuu naomba tuwasilianee unifahamishe zaidi tafadhali mkuu.

Naweza kuja pm mana nna shida ya kuagiza kitu flani hivi na sijawahi kufanya chochote kile mtandaoni..
binafsi nafurahi sana mtu kuogopa kufanya manunuzi mtandaoni kwa sababu sitaki wenye vitu vizuri tuwe wengi town.

Kwa mara ya kwanza nilisoma humu Jf kuhusu kufanya manunuzi mtandaoni, nilisoma thread nyingi na tofauti tofauti ili nipate uelewa kwa kiasi kikubwa.

kwa mara ya kwanza niliagiza vitu aliexpress na vikafika bila shida japokuwa nilichelewa sana, nikarudi tena kusoma thread za JF nikagundua kuwa ni lazima kusoma feedback za wanunuzi wengine ili kujua kama bidhaa ni halisi na ina ubora gani.

Kuna ndugu yangu nilimsaidia kuagiza simu yake ya Samsung ambayo kwa hapa TZ mpya ni laki 7 na vijisent ila kwa nje nilipata kwa laki 2 na ushee buti ni used.

kabla ya mzigo kufika wafanyakazi wenzie walikuwa wanamponda sana kuwa hiyo laki mbili imeibiwa tayari, walimcheka sana kwa mujibu wake alivyoniambia ila baada ya 16 days mzigo ukafika aisee ilikuwa ni kama mpya kabisa + free orijino Chaja, sasa anasema kila mtu ana mtamani na anavyosema kuwa ukitoa yeye na mkurugenzi hakuna mwingine mwenye simu kali kama yake.

Wauzaji wengi wa nje sio waongo kama wa Kupatana.

Mtu nikimwambia kuwa hata ukiiba au mzigo kutofika unarudisha mtonyo wako na asipoamini naachana nae atakuwa anaona wenzie wasukuma tunamiliki vitu vya bei mbaya kumbe tumechukua nje kwa bei kama bure.

MBONA MKIAGIZA MAGARI HAMSEMI KAMA KUNA KUIBIWA?

mfanyabiashara wa Kariakoo anakuuzia simu laki 6 wakati ungezama aliepress, ebay au amazoni ungepata kwa laki 4.


Watanzania tuwe tunajaribu vitu sio kusema eti nitaibiwa na hujawahi hata kujaribu kununua hata mbegu za nyanya aliexpress za Tsh 600/-

WOGA WAKO NDIO UMASKINI WAKO.
 
Japo kuwa tupo katika 'information age' lakini naona kuna muamuko mdogo sana, hasa wa sisi watanzania kufanya manunuzi mtandaoni. Mimi binafsi nishafanya mara moja kununua bidhaa mtandaoni. Japo kuwa bidhaa ilifika lakini kipindi naisubiri nilipitiwa na mawazo mengi, ikiwemo hofu ya kutapeliwa au kufikishiwa mzigo sio.

Je kwa upande wako ambae umewahi au hujawahi ni nini hofu yako uliyonayo kukufanya usiendelee au usijaribu kununua bidhaa "online".

Karibu kwa mchango wako. Pia wazoefu mnakaribishwa.
Kuna sababu kuu tatu:

1. Wengi wana vipato vidogo. Hasa ndiyo sababu kubwa.

2. Wengi wana anuwani address ngumu kufikika. Postal code, hakuna mitaa. Maelezo ni mwembe, Msikiti, Kanisa au Bar fulani. Sehemu kubwa hasa Dar haijapimwa

3. Uelewa finyu wa kutumia card za bank (Visa, MasterCard etc.) Wengi ni kuchukulia hela Kwenye ATM. Hawajui vitu Amazon.
 
Tuna tabia ya kuwa wazito kufanya maamuzi na sio ma risk taker (low risk appetite). Angalia tu katika makundi mengi mfano ya whatsapp, ni mangapi mnakubaliana mambo ya msingi na mangapi kweli mnayakamilisha. Ikifika kwenye suala la kufanya maamuzi tunakuwa wazito. Tuna ile ya kwamba product lazima niwe nimeiona na kuigusa ndo ninunue. Kuna culture legacy fulani pia, mfano watu wamezoea bargaining lakini online hakuna bargainining. Pia kuna suala la uelewa. Unakuta mtu anakuta kitu kinauzwa dola moja online. Anataka kununua mzigo wa laki mbili, hapo hajui kwamba ule mzigo ni bila gharamza za usafiri na pengine unaweza kuwa na kodi
 
..... Ila kwa nje ya nchi bado sijawahi kununua na hasa shida IPO kwenye hii kitu credit card/debit visa yaani hapa huwa nahisi nikijaribu tu hackers wanaweza kuchukua mpunga wote .....

Tengeneza M-Pesa Mastercad kupitia M-Pesa, ni rahisi sana.

Ukitaka kununua kitu unahamisha hela kutoka M-Pesa kwenda M-Pesa Mastercard. Mimi naitumia sana kununua vitu ebay na amazon
Screenshot_20190623-180412.jpeg
Screenshot_20190623-180422.jpeg
 
tutafanya manunuzi mtandaoni hadi pale serikali itakapo punguza kodi ya mzigo bandarini. Pia tutafanya manunuzi mtandaoni hadi pale serikali kupitia benki kuu itakapo ruhusu tuweze kupokea pesa kutoka mataifa mengine kupitia PAYPAL. Haiewezekani mtu uweze kufanya malipo alafu kupokea ushindwe.
 
binafsi nafurahi sana mtu kuogopa kufanya manunuzi mtandaoni kwa sababu sitaki wenye vitu vizuri tuwe wengi town.

Kwa mara ya kwanza nilisoma humu Jf kuhusu kufanya manunuzi mtandaoni, nilisoma thread nyingi na tofauti tofauti ili nipate uelewa kwa kiasi kikubwa.

kwa mara ya kwanza niliagiza vitu aliexpress na vikafika bila shida japokuwa nilichelewa sana, nikarudi tena kusoma thread za JF nikagundua kuwa ni lazima kusoma feedback za wanunuzi wengine ili kujua kama bidhaa ni halisi na ina ubora gani.

Kuna ndugu yangu nilimsaidia kuagiza simu yake ya Samsung ambayo kwa hapa TZ mpya ni laki 7 na vijisent ila kwa nje nilipata kwa laki 2 na ushee buti ni used.

kabla ya mzigo kufika wafanyakazi wenzie walikuwa wanamponda sana kuwa hiyo laki mbili imeibiwa tayari, walimcheka sana kwa mujibu wake alivyoniambia ila baada ya 16 days mzigo ukafika aisee ilikuwa ni kama mpya kabisa + free orijino Chaja, sasa anasema kila mtu ana mtamani na anavyosema kuwa ukitoa yeye na mkurugenzi hakuna mwingine mwenye simu kali kama yake.

Wauzaji wengi wa nje sio waongo kama wa Kupatana.

Mtu nikimwambia kuwa hata ukiiba au mzigo kutofika unarudisha mtonyo wako na asipoamini naachana nae atakuwa anaona wenzie wasukuma tunamiliki vitu vya bei mbaya kumbe tumechukua nje kwa bei kama bure.

MBONA MKIAGIZA MAGARI HAMSEMI KAMA KUNA KUIBIWA?

mfanyabiashara wa Kariakoo anakuuzia simu laki 6 wakati ungezama aliepress, ebay au amazoni ungepata kwa laki 4.


Watanzania tuwe tunajaribu vitu sio kusema eti nitaibiwa na hujawahi hata kujaribu kununua hata mbegu za nyanya aliexpress za Tsh 600/-

WOGA WAKO NDIO UMASKINI WAKO.
Vip kuhusu Kodi?
 
Dah, yaani mimi mtandaoni ndo kama nyumbani. Vitu vingi nanunua na kuagiza mtandaoni.

Nimesha zoea na wala sina wasiwasi. Kikubwa ni kujua kanuni kuu za kununua mtandaoni. Kubwa kuliko yote, unanunua mtandao gani.

Mitandao kama ebay na amazon wanatumia mfumo unaitwa Escrow. Sawa na mtandao kama wa www.ajiras.com wa bongo unaotumia.

Kwa kifupi, hela yako inakuwa secured mpaka upokee mzigo wako. Bila hivyo, muuzaji atatuma tena au utarudishiwa hela yako.
Hiyo escrow inafanyaje kaz mkuu?
 
Hiyo escrow inafanyaje kaz mkuu?
Ipo aina mbili
1. Wewe kama mteja, ukilipia kununua kitu, yule muuzaji, hapokei hela, anapokea tu order, mpaka wewe utakapo dhibitisha kuupata mzigo na kuwa upo sawa, ndiyo anapewa hela yake. Usipopata huduma, unarudishiwa hela yako.

2. Mteja ukilipia kitu, wao kama kampuni au website, wana mdhamini muizaji, yaani, asipo deliver wao watakurudishia hela yako. Alafu wao ndo wata pambana kupata hela yako kutoka kwa muuzaji.
 
Tengeneza M-Pesa Mastercad kupitia M-Pesa, ni rahisi sana.
Ukitaka kununua kitu unahamisha hela kutoka M-Pesa kwenda M-Pesa Mastercard. Mimi naitumia sana kununua vitu ebay na amazonView attachment 1136464View attachment 1136465
Kujiunga amazon, eBay, AliExpress n.k ili uanze kuagiza vitu kunahitaji ujaze email na majina yako. Je, haina shida majina na email ulivyojaza visipofanana na majina ya kwenye tembo card?
 
Kwa kesi ya manunuzi mtandani hapo kuna makundi mawili mkuu kundi lakwanza niwauzaji wandani ya nchi wanaopost bidhaa zao ktk mitandao mbali mbali yakijamii ktk hili nami nimeshawahi kufanya manunuzi simara moja wala mbili sasa kuna hili kundi lapili wale akina ebay,Amazon,Aliexpress n.k Kwakweli hawa mimi sijawahi kuagiza japo one day nitajilipua kila nikickia kua mzigo ukifika Tz TRA wanataka cjui % ngap yathamani namzigo hapo ndo najiuliza sasa apa nitakua nimesev kias gani..je ww ulivyoagiza iyo bidhaa kama uliagiza toka nje kwa akina Amazon uliokoa pesa kias gani tofauti nakama ungenunulia tu hapa hapa nchini?
Posta unalipia 1500 kwa parcel. Parcel nyingine unachukua kwa free bila malipo usiogope.
 
Kujiunga amazon, eBay, AliExpress n.k ili uanze kuagiza vitu kunahitaji ujaze email na majina yako. Je, haina shida majina na email ulivyojaza visipofanana na majina ya kwenye tembo card?
Haina shida Kama Mimi address yangu nimeandika jina la baba watoto , visa card jina langu so mzigo ukija unakuja kwa jina lake anaenda kunichukulia.
 
Haina shida Kama Mimi address yangu nimeandika jina la baba watoto , visa card jina langu so mzigo ukija unakuja kwa jina lake anaenda kunichukulia.
Nashukuru Mkuu.
Vipi majina yote yakitofautiana?, yaani ya kwenye email yawe A B, niliyojaza yawe C D, na ya kwenye tembo card yawe E F?
 
Back
Top Bottom