Hivi ni kwanini Wakristo wengi hawasomi Agano la Kale kama wasomavyo lile Jipya?

Online Pastor

JF-Expert Member
Sep 7, 2017
1,948
1,515
Nimefanya huduma karibu Tanzania yote na hivyo nimepata wasaa wakubadilishana mawazo na watu wengi.


Baada ya miaka mingi kwenye huduma nimegundua:


1)Ni wakristo wachache sana wanaolisoma Agano lote la Kale.


2)Ukiacha Wasabato,karibu wakristo wote hufuatilia Agano Jipya.


3)Kuna mambo mengi yaliyo katika Agano Jipya ambalo msingi wake huko Agano la Kale,hivyo wale wasiolisoma hawawezi unganisha uhusiano wake wafikapo katika Agano la Kale.

Ningependa kujua;ni kwanini Wakristo walio wengi huwa hawalisomi Agano la Kale?
 
Nitangulie kujibu hv,
Moja watu wa siku hz ni wavivu wa kusoma,
Jambo jingine huko makanisani huambiwa kuwa hilo lilihusu wa Israel tu!

Wengine huridhika na usomaji wa kiongozi wao!
Hivyo Agano LA kale kushindwa kuvuka vigezo hivyo!
 
ndayilagije

Kabisa.

Uvivu wa kujisomea Biblia hasa Agano la Kale unaligharimu sio tu kanisa,bali hata waumini.

Na mbaya zaidi ukosefu wa nia ya kujitafutia maarifa ya kimungu ndiyo unaotugharimu sana
 
ndayilagije

Kabisa.

Uvivu wa kujisomea Biblia hasa Agano la Kale unaligharimu sio tu kanisa,bali hata waumini.

Na mbaya zaidi ukosefu wa nia ya kujitafutia maarifa ya kimungu ndiyo unaotugharimu sana
Lakini pastor hata nyie mnalo la kujibu kwa Mungu. Mimi mwenyewe nitawalisha kondoo wangu,nitawalaza,na kuwaongoza walio wadhaifu kwa upole! Mnahubiri mno sadaka mpaka mnatuchosha. BTW mtu apandacho si ndicho avunacho? Ikiwa mtu hataishi kwa mkate tu bali kwa kila neno la Mungu,mbona mnapenda sana kutusikilizia kutoka kwa Mungu as if sisi hatukupewa masikio?
 
Nimefanya huduma karibu Tanzania yote na hivyo nimepata wasaa wakubadilishana mawazo na watu wengi.


Baada ya miaka mingi kwenye huduma nimegundua:


1)Ni wakristo wachache sana wanaolisoma Agano lote la Kale.


2)Ukiacha Wasabato,karibu wakristo wote hufuatilia Agano Jipya.


3)Kuna mambo mengi yaliyo katika Agano Jipya ambalo msingi wake huko Agano la Kale,hivyo wale wasiolisoma hawawezi unganisha uhusiano wake wafikapo katika Agano la Kale.

Ningependa kujua;ni kwanini Wakristo walio wengi huwa hawalisomi Agano la Kale?

Umesahau kuwa ya kale yamepita na tazama yamekuwa mapya..
 
Kadhi Mkuu 1

Kwahiyo kumbe shida siyo Agano Kale,ila ni siye binadamu kushindwa kuliishi kwa wakati huu?

Btw,hata Yesu alinukuliwa akisema kuwa hakuna kuipangua Torati bali kuitimiliza.

Kama hautojali,waweza nionyesha mstari usemao kuwa ni vibaya kuliishi Agano lote la Kale?
 
Umesahau kuwa ya kale yamepita na tazama yamekuwa mapya..
Yamepita ni kweli,lakini mwana wa Adam hakuja kutengua torati bali kuitimiza. Huwezi kuelewa agano jipya pasipo agano la kale. Mf. Nyoka wa shaba aliyeinuliwa na Musa jangwani utajuaje kuwa ndiye kristo aliyeangikwa msalabani usiposoma kitabu cha kutoka mpaka injili ya Yohana.
 
ndayilagije

Naunga mkono hoja yako.

Na kuna uzi wangu humu ulizungumzia changamoto zinazowavunja moyo waumini kwenda kanisani.

Utoaji usiyo na staha ni kikwazo kikubwa dhidi ya waumini wetu.

Miye kwa upande wangu nitaufaanyia kazi ushauri wako!
 
Nimeuona pastor, back to the topic!Ni muhimu sana kutofautisha kanisa kama kusanyiko na Mungu kama muumbaji,hilo ni somo jingine ambalo halifundishwi kabisa!
 
Wanasoma sana tu, hakuna agano jipya bila la kale wala hakuna agano la kale bila jipya biblia takatifu inakamilishwa na agano jipya na la kale ili uwe mkristo kamili ni lazima usome maagano yote yani la kale na jipya.
 
Kadhi Mkuu 1

Kwahiyo kumbe shida siyo Agano Kale,ila ni siye binadamu kushindwa kuliishi kwa wakati huu?

Btw,hata Yesu alinukuliwa akisema kuwa hakuna kuipangua Torati bali kuitimiliza.

Kama hautojali,waweza nionyesha mstari usemao kuwa ni vibaya kuliishi Agano lote la Kale?
Huwezi kuhesabiwa haki kwa matendo ya sheria. Yesu alizaliwa chini ya sheria ili awakomboe waliokuwa chini ya sheria. (Kiufupi kushika sheria haiwezekani)tunaishi kwa neema.
 
Back
Top Bottom