Hivi ni kwanini Serikali hii inawafanyia hila mbalimbali wagombea wa upinzani kwenye chaguzi zinazoendelea nchini?

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,478
30,141
Tumesikia vituko na hila mbalimbali wanazofanyiwa wagombea wa upinzani, hususani wa chama kikuu cha upinzani nchini cha Chadema katika uchaguzi wa serikali za mitaa, unaotarajiwa kufanyika hapa nchini, tarehe 24 mwezi Novemba, mwaka huu

Vituko kama vile wasimamizi wa uchaguzi "kuzikimbia" ofisi zao katika siku ambayo ndiyo iliyoelezwa kuwa rasmi ya kuchukua fomu za kugombea uongozi wa serikali za mitaa, ndiyo habari ya mjini hivi sasa

Wagombea wa upinzani kupewa fomu, na wasimsmizi wa uchaguzi, ambazo hazijapigwa mihuri, ndiyo habari nyingine inayo- trend sana hivi sasa

Nimekuwa nikijiuliza maswali kadhaa, hivi hiki ninachokiona kwenye uchaguzi huu, ndicho kinachoshabiana na tambo zote za wanaccm kuwa upinzani nchini kwetu umejifia wenyewe, kutokana na juhudi kubwa zinazofanywa na Rais Magufuli za kujenga reli ya SGR, Bwawa la umeme kutoka mto Rufiji na kununua ma-dreamlimer ambapo watetezi hao wa utawala huu wa awamu ya tano, umekuwa ukidai kuwa maendeleo aliyoyafanya Mheshimiwa Rais Magufuli, katika kipindi hiki, hayakuwahi fanyika katika tawala zote za awamu zilizopita!

Ningependa kuwauliza hao watetezi wakubwa wa utawala wa awamu hii, hivi si mnaijua ile methali isemayo kizuri chajiuza na kibaya chajitembeza??

Sasa ningependa kuwauliza hao wapambe, ni kitu gani mnachokihofia, wakati mnajua kuwa mazuri mnayoyafanya yanaonekana hadi na kipofu??

Hivi hii hali inayoendelea, tukiunganisha dots, tutakuwa tunakosea tukisema natokana na vitisho alivyovitoa Jiwe, alipowatamkia kuwa nyiye maDED ninawapa magari ya kifahari ya kutembelea, nyumba nzuri za kuishi na mishahara minono............

Halafu nisikie umemtangaza mpinzani kashinda katika eneo lako, utakuwa umejifukuzisha kazi wewe mwenyewe!

Nchi yetu kikatiba ni ya mfumo wa vyama vingi, na kwa maana hiyo kwa mwananchi kuchagua kiongozi wa upinzani siyo dhambi......

Kama nyiye watawala wetu mlikula kiapo cha kuitii Katiba hiyo, kwa hiyo ni vyema sisi wananchi tukaona KWELI Katiba hiyo inatekelezwa kwa vitendo
 
Mbali na kasoro za tume lakini pia ndani ya vyama vyetu vya upinzani kuna kasoro ktk ukamilishaji wa taratibu za mchakato wa chaguzi. Vyama vimekua vikiingia katika mchakato kwa kukurupuka sababu ya kutokuwa na maandalizi ya kupata wagombea (Hakuna kalenda ya kuteua wagombea wa vyama) Wengine wanapatikana siku ya kuanza zoezi la kuchukua fomu. Mara kadhaa mbali na uchukuaji fomu utakuta hata urudishaji, sababu ya kukurupuka wanasahau hata kutimisha masharti ya ujazaji hivyo wanakosa sifa. Sharti la kupewa fomu ni lazima uwe na barua rasmi ya utambulisho wa Chama (sio kwenda na kiongozi) msimamizi hakupi fomu. Ilitokea uchaguzi mdogo Songwe, wagombea wawili wa chadema wote wawili wana barua za utambulisho, aliyewahi akapewa fomu na mwingine anatokea baadaye yeye ndiye halali akanyimwa. Matokeo yake analaumiwa msimamizi badala ya viongozi wao waliotoa barua za utambulisho.
 
Hawajaamini kuwa CCM itashinda bila kuwafanyia figisu figisu ..Mbona Wanasema wamefanya mambo makubwa kuliko awamu zote?
Ndicho kinachoshangaza sana.........

Hivi Serikali inayodai imewafanyia mambo makubwa sana kimaendeleo wananchi wake, ni kwa vipi iogope kupita kiasi na kuwafanyia vitimbwi vyote hivi wagombea wa upinzani??
 
Kadri wapinzani watakavyochukua fomu na kushiriki uchaguzi wowote ule ndivyo watakavyozidi kumalizwa kwa kuonekana kuwa eti wameshindwa uchaguzi.
 
Mbali na kasoro za tume lakini pia ndani ya vyama vyetu vya upinzani kuna kasoro ktk ukamilishaji wa taratibu za mchakato wa chaguzi. Vyama vimekua vikiingia katika mchakato kwa kukurupuka sababu ya kutokuwa na maandalizi ya kupata wagombea (Hakuna kalenda ya kuteua wagombea wa vyama) Wengine wanapatikana siku ya kuanza zoezi la kuchukua fomu. Mara kadhaa mbali na uchukuaji fomu utakuta hata urudishaji, sababu ya kukurupuka wanasahau hata kutimisha masharti ya ujazaji hivyo wanakosa sifa. Sharti la kupewa fomu ni lazima uwe na barua rasmi ya utambulisho wa Chama (sio kwenda na kiongozi) msimamizi hakupi fomu. Ilitokea uchaguzi mdogo Songwe, wagombea wawili wa chadema wote wawili wana barua za utambulisho, aliyewahi akapewa fomu na mwingine anatokea baadaye yeye ndiye halali akanyimwa. Matokeo yake analaumiwa msimamizi badala ya viongozi wao waliotoa barua za utambulisho.
Wapeni fomu watu wote wanaoomba uongozi wa kitongoji,kijiji na wapiga kura wanataamua na kuwachagua viongozi wawapendao,tuache kuweka vikwazo amabayo si kura.Kule Kenya waliwahi kuwa na uchaguzi wa mlolongo,mimi naona huo mfumo ni bora kuliko huu wa kwetu maana mlolongo ni wa wazi na gharama zake ni ndogo.Nawaza tu!
Mbona ni kama kuna chama kinaogopa kivuli chake?Wekeni na tengenezeni uwanja sawa watu waamue na kuchagua viongozi wao.Watanzania siyo wajinga,ni waumini wa amani na utulivu kwa kuzaliwa.Punguzeni figisu,drama,stress na vitisho mambo yaende.
 
Wapeni fomu watu wote wanaoomba uongozi wa kitongoji,kijiji na wapiga kura wanataamua na kuwachagua viongozi wawapendao,tuache kuweka vikwazo amabayo si kura.Kule Kenya waliwahi kuwa na uchaguzi wa mlolongo,mimi naona huo mfumo ni bora kuliko huu wa kwetu maana mlolongo ni wa wazi na gharama zake ni ndogo.Nawaza tu!
Mbona ni kama kuna chama kinaogopa kivuli chake?Wekeni na tengenezeni uwanja sawa watu waamue na kuchagua viongozi wao.Watanzania siyo wajinga,ni waumini wa amani na utulivu kwa kuzaliwa.Punguzeni figisu,drama,stress na vitisho mambo yaende.
Eti hao maccm wameweka condition hadi ukiwa mgombea hujachangia Mwenge, unakuwa disqualified kupewa fomu za kugombea!

Ukiwauliza wakuonyeshe kifungu katika kanuni zao, kinachoonyesha huo "upuuzi" wao, wanabaki kung'aa tu mimacho yao!
 
Tumesikia vituko na hila mbalimbali wanazofanyiwa wagombea wa upinzani, hususani wa chama kikuu cha upinzani nchini cha Chadema katika uchaguzi wa serikali za mitaa, unaotarajiwa kufanyika hapa nchini, tarehe 24 mwezi Novemba, mwaka huu

Vituko kama vile wasimamizi wa uchaguzi "kuzikimbia" ofisi zao katika siku ambayo ndiyo iliyoelezwa kuwa rasmi ya kuchukua fomu za kugombea uongozi wa serikali za mitaa, ndiyo habari ya mjini hivi sasa

Wagombea wa upinzani kupewa fomu, na wasimsmizi wa uchaguzi, ambazo hazijapigwa mihuri, ndiyo habari nyingine inayo- trend sana hivi sasa

Nimekuwa nikijiuliza maswali kadhaa, hivi hiki ninachokiona kwenye uchaguzi huu, ndicho kinachoshabiana na tambo zote za wanaccm kuwa upinzani nchini kwetu umejifia wenyewe, kutokana na juhudi kubwa zinazofanywa na Rais Magufuli za kujenga reli ya SGR, Bwawa la umeme kutoka mto Rufiji na kununua ma-dreamlimer ambapo watetezi hao wa utawala huu wa awamu ya tano, umekuwa ukidai kuwa maendeleo aliyoyafanya Mheshimiwa Rais Magufuli, katika kipindi hiki, hayakuwahi fanyika katika tawala zote za awamu zilizopita!

Ningependa kuwauliza hao watetezi wakubwa wa utawala wa awamu hii, hivi si mnaijua ile methali isemayo kizuri chajiuza na kibaya chajitembeza??

Sasa ningependa kuwauliza hao wapambe, ni kitu gani mnachokihofia, wakati mnajua kuwa mazuri mnayoyafanya yanaonekana hadi na kipofu??

Hivi hii hali inayoendelea, tukiunganisha dots, tutakuwa tunakosea tukisema natokana na vitisho alivyovitoa Jiwe, alipowatamkia kuwa nyiye maDED ninawapa magari ya kifahari ya kutembelea, nyumba nzuri za kuishi na mishahara minono............

Halafu nisikie umemtangaza mpinzani kashinda katika eneo lako, utakuwa umejifukuzisha kazi wewe mwenyewe!

Nchi yetu kikatiba ni ya mfumo wa vyama vingi, na kwa maana hiyo kwa mwananchi kuchagua kiongozi wa upinzani siyo dhambi......

Kama nyiye watawala wetu mlikula kiapo cha kuitii Katiba hiyo, kwa hiyo ni vyema sisi wananchi tukaona KWELI Katiba hiyo inatekelezwa kwa vitendo
Mkuu binafsi nilideclare kutohusika na Uchaguzi wowote hapa Tazania kwa Katiba ya kijinga hii.
Nitafikiria kupiga Kura pale itakapoanza kufanya kazi na bila Kubadilishwa Chochote.
 
Kusema ukweli sisi ccm..tumeishiwa hoja..hatuwezi mikiki mikiki ya kisiasa..na tunajua wananchi wametuchoka..sema tamaa tu ya madaraka..mana bila nguvu ya dola na figisufigisu sisi ni hohe hahe.
 
Back
Top Bottom