Tuache ujima! Tuache Rais Magufuli asemwe, kukosolewa hata kushauriwa. Tuache vitisho

CCM original

JF-Expert Member
Apr 28, 2013
373
68
Mimi ni mwajiri wa Dr. John Pombe Magufuli, nimemwajiri kunitumikia, alete maendeleo kwangu na kwa taifa zima.

Nitakuza kichaa endapo nitaacha kumshauri, kumsema na hata kumkosoa pale anapokosea. Ni ajabu mtu nimemwajiri halafu nisimseme, kumkosoa na kumshauri.

Naona kwa sasa umezuka mchezo wa kumfanya mh. Rais ajione yuko sahihi kwa kila jambo. Na mtu anayetazama kwa mbali kuonekana mhaini, mbaguzi, mwongo, ana inda, ana uchama, ukanda nk.

Kwa hapa niko tofauti na chama changu, chama cha Mapinduzi.

Mbona Kikwete hakulindwa kwa nguvu hizi? Tena hata yeye alikuwa anaona anavyotukanwa, lakini akaruhusu watu waoneshe hasira zao ili ajue wapi kakosea.

Mh. Rais ana kasi nzuri, ya kutia matumaini, ila wanaotofautiana mawazo ktk mambo flani huenda hata kutoa lugha isiyofaa, utumike utashi wa kisiasa, waachwe watapike hasira zao. Hapo tutakuwa tunaona wapi anakosea nasi kama wanachama wa chama cha Mapinduzi kumshauri mh. Rais.

Kidumu Chama Cha Mapinduzi!!
 
Naona kwa sasa umezuka mchezo wa kumfanya mh. Rais ajione yuko sahihi kwa kila jambo. Na mtu anayetazama kwa mbali kuonekana mhaini, mbaguzi, mwongo, ana inda, ana uchama, ukanda nk."
Ebu site mifano basi tukuelewe na tuanze changia maana kwa kuwa mada yako is too general watu wameanza toa mfano wa aliyesema JPM bwege,ingawa kwa uelewa wangu mdogo I guess you meant more than tha.
IN general JPM sio mungu ni binaadamu na ana mapungufu yake ukitumia proper channels kumkosoa litafanyiwa kazi
 
Mimi ni mwajiri wa Dr. John Pombe Magufuli, nimemwajiri kunitumikia, alete maendeleo kwangu na kwa taifa zima.

Nitakuza kichaa endapo nitaacha kumshauri, kumsema na hata kumkosoa pale anapokosea. Ni ajabu mtu nimemwajiri halafu nisimseme, kumkosoa na kumshauri.

Naona kwa sasa umezuka mchezo wa kumfanya mh. Rais ajione yuko sahihi kwa kila jambo. Na mtu anayetazama kwa mbali kuonekana mhaini, mbaguzi, mwongo, ana inda, ana uchama, ukanda nk.

Kwa hapa niko tofauti na chama changu, chama cha Mapinduzi.

Mbona Kikwete hakulindwa kwa nguvu hizi? Tena hata yeye alikuwa anaona anavyotukanwa, lakini akaruhusu watu waoneshe hasira zao ili ajue wapi kakosea.

Mh. Rais ana kasi nzuri, ya kutia matumaini, ila wanaotofautiana mawazo ktk mambo flani huenda hata kutoa lugha isiyofaa, utumike utashi wa kisiasa, waachwe watapike hasira zao. Hapo tutakuwa tunaona wapi anakosea nasi kama wanachama wa chama cha Mapinduzi kumshauri mh. Rais.

Kidumu Chama Cha Mapinduzi!!
Rais wetu yupo sahihi kwa kila jambo, hacha filimbi zako hazitusaidii maana kazi za urais huzijui , kafanye kazi acha longo longo
 
Mimi ni mwajiri wa Dr. John Pombe Magufuli, nimemwajiri kunitumikia, alete maendeleo kwangu na kwa taifa zima.

Nitakuza kichaa endapo nitaacha kumshauri, kumsema na hata kumkosoa pale anapokosea. Ni ajabu mtu nimemwajiri halafu nisimseme, kumkosoa na kumshauri.

Naona kwa sasa umezuka mchezo wa kumfanya mh. Rais ajione yuko sahihi kwa kila jambo. Na mtu anayetazama kwa mbali kuonekana mhaini, mbaguzi, mwongo, ana inda, ana uchama, ukanda nk.

Kwa hapa niko tofauti na chama changu, chama cha Mapinduzi.

Mbona Kikwete hakulindwa kwa nguvu hizi? Tena hata yeye alikuwa anaona anavyotukanwa, lakini akaruhusu watu waoneshe hasira zao ili ajue wapi kakosea.

Mh. Rais ana kasi nzuri, ya kutia matumaini, ila wanaotofautiana mawazo ktk mambo flani huenda hata kutoa lugha isiyofaa, utumike utashi wa kisiasa, waachwe watapike hasira zao. Hapo tutakuwa tunaona wapi anakosea nasi kama wanachama wa chama cha Mapinduzi kumshauri mh. Rais.

Kidumu Chama Cha Mapinduzi!!
Peleka ujinga Monduli.
 
Can you dare to call your father "bwege"????
Uongozi ni ustahamilivu jamani. Kuna kina Obama wameitwa majina mengi saana, kina Nyerere na hivi karibuni Kikwete. Lakini katika hali yoyote Rais hawezi kufanana na baba yangu. My dad is my dad whether he is a farmer au ombaomba kwa Makonda, his value and recognition is beyond the person who last for 10 years and only through ballot box.
 
Kumkosoa Rais si kosa ila kosa ni kumdhalilisha Rais mbele ya wananchi wake.Hivyo kukosoa kwa kutumia lugha ya matusi si sahihi! Angetumia maneno yenye
staha angefikisha ujumbe wake.Lakini hili
la BWEGE hata mimi siliafiki.




Umeongea jambo la msingi mifano ipo humu humu jamvini unaweza anzisha uzi au kuchangia lakini kuna watu ambao hawana staha na nidhamu inafanya hata Great Thinkers kuonekana hawana maana.

Matusi si jambo la kulishabikia hata huyo aliyetukana yeye mwenye akitukaniwa mzazi wake aliye mlea hata akakosa staha mbele ya jamii hata vumilia.

Mara nyingi ni bora unitukane mimi kuliko mzazi wangu. Sasa yeye amemtukana mzazi wa mtu ambaye havumilii huu udhalilishaji kama yeye ambavyo asingevumilia.
 
Tatizo lenu mkisikia kitu mnaanza kutafuta hoja za kukosoa....BTW hujakatazwa kukosoa au unataka kutukana
 
Asifiwe tu jamani? Ukikubali kusifiwa ukubali kukosolewa pia, na wengine watakuita bwege, Fala, chizi, ndiyo aina yao ya ukosoaji . Vumilia uliipenda siasa, anze kukataa kusifiwa pia
 
Huyu mleta hoja aache Rais wetu achape kazi ,tokea lini wewe umekuwa mshauri wa Rais, Rais ana washauri wake kama Baraza la Mawaziri ,wewe ni nani ushauri utenda kazi wa Rais wetu watu wa namna hii ndio wana chelewesha maendeleo ,wewe ni mshauri wa familia yako .Na wala Rais hujamwajiri wewe bali waTanzania kwa umoja wetu anayoyafanya yote yana kibali cha sisi wananchi .Tulia mzee afanye kazi arudishe nchi kwenye mustari ,
 
Naona mmeanza kutimiza yale yaliyoandikwa na magazeti juzi.

Ngoja nisubiri bunge lianze nijionee.
 
Mleta hoja alikimbia jukwaa miaka miwili iliyopita baada ya kuumbuka. Aliandaa mkakati wa kutaka wana CCM waliopo JF tufahamiane na tupeane namba za simu. Tena alienda mbali akataka tuandae kikao ili tubadilishane mawazo. Hakika aliumbuka sana baada ya kubainika kuwa kumbe jamaa ni CHADEMA damu. Naona amefufuka na amekuja kwa style ile ile. Tumekushtukia
 
Back
Top Bottom