Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,477
- 30,137
Kuna msamiati mpya umetungwa hususani na watawala wetu wa serikali ya awamu ya 5 kwa kuwaita nchi za wazingu kuwa ni mabeberu, pale wanapotoa "constructive criticism" yenye lengo la kututaka tujirekebishe ili nchi yetu ipate ufanisi wa hali ya juu.
Hata hivyo ajabu ni kuwa wazungu hao hao, wanapokaa kimya bila kusema lolote kutokana na maovu tunayoyafanya, tunawasifu sana na kuwaita kuwa ni wahisani wetu wa maendeleo.
Tunafahamu kuwa katika vitabu vyote vya dini vinatwambia kuwa mkamilifu ni mmoja pekee, ambaye ni Mungu aliyetuumba na sisi binadamu wengine wote, tuna mapungufu yetu, ambayo tunapaswa tuelezane ili tujirekebishe.
Sasa hili la watawala wetu kuchukua "capacity" ya Mungu wetu na kutotaka kabisa kukosolewa ni kujiletea laana, kwa kuwa watakuwa wanapingana na maandiko matakatifu ambayo yanampa Mungu pekee, ambaye hapaswi kukosolewa kwa lolote na sisi binadamu tunafahamu kuwa ni yeye pekee Mungu wetu, ambaye yuko "perfect by 100 percent"
Vile vile kuna kumezuka propaganda za kitoto sana za watawala wetu za kudai kuwa tupo kwenye vita ya kiuchumi na hao wazungu, ndiyo sababu ya hao wazungu aka mabeberu kutuonea wivu na kutupiga vita.
Hivi sisi kanchi tunaoagiza hata vijiti tu vya kuchokonoa "tooth picks" tunawezaje kupigwa vita na nchi kama Marekani, yenye uwezo wa kutengeneza kila kitu tunachotumia kuanzia magari ya kifahari tunayotembelea hadi hayo madege tunayoyaita "dreamliners" tunayotamba nayo kuwa tumeyanunua kwa fedha taslimu?
Vile vile hii nchi yetu tunapenda sana kujimwambafai kuwa eti nchi yetu tuna uwezo wa kuwa "donor country" kwa hizo nchi za mabeberu.
Sasa mbona serikali yetu imeanza kuhaha na kuweweseka sana, baada tu ya hizo nchi za mabeberu za EU, kuonyesha dalili za kutukatia misaada baada ya wao kubaini kuwa nchi yetu imeuvuruga mno mfumo wa kidemokrasia na uchaguzi mkuu uliopita na inakiuka mno haki za binadamu?
Tunapaswa tujisahihishe, wazungu wanapotukosoa tukae chini na kuangalia ni wapi tulipokosea na tujirekebishe, badala ya hii hali tunayoendelea nayo ya kujiona sisi tuko 100 percent perfect na kila wazungu wanapotukosoa tuwaite majina mabaya kuwa wao ni mabeberu, lakini wanapokaa kimya kama China, tunawasifu na kuwaita ni washirika na wahisani wetu wazuri wa maendeleo.
Hata hivyo ajabu ni kuwa wazungu hao hao, wanapokaa kimya bila kusema lolote kutokana na maovu tunayoyafanya, tunawasifu sana na kuwaita kuwa ni wahisani wetu wa maendeleo.
Tunafahamu kuwa katika vitabu vyote vya dini vinatwambia kuwa mkamilifu ni mmoja pekee, ambaye ni Mungu aliyetuumba na sisi binadamu wengine wote, tuna mapungufu yetu, ambayo tunapaswa tuelezane ili tujirekebishe.
Sasa hili la watawala wetu kuchukua "capacity" ya Mungu wetu na kutotaka kabisa kukosolewa ni kujiletea laana, kwa kuwa watakuwa wanapingana na maandiko matakatifu ambayo yanampa Mungu pekee, ambaye hapaswi kukosolewa kwa lolote na sisi binadamu tunafahamu kuwa ni yeye pekee Mungu wetu, ambaye yuko "perfect by 100 percent"
Vile vile kuna kumezuka propaganda za kitoto sana za watawala wetu za kudai kuwa tupo kwenye vita ya kiuchumi na hao wazungu, ndiyo sababu ya hao wazungu aka mabeberu kutuonea wivu na kutupiga vita.
Hivi sisi kanchi tunaoagiza hata vijiti tu vya kuchokonoa "tooth picks" tunawezaje kupigwa vita na nchi kama Marekani, yenye uwezo wa kutengeneza kila kitu tunachotumia kuanzia magari ya kifahari tunayotembelea hadi hayo madege tunayoyaita "dreamliners" tunayotamba nayo kuwa tumeyanunua kwa fedha taslimu?
Vile vile hii nchi yetu tunapenda sana kujimwambafai kuwa eti nchi yetu tuna uwezo wa kuwa "donor country" kwa hizo nchi za mabeberu.
Sasa mbona serikali yetu imeanza kuhaha na kuweweseka sana, baada tu ya hizo nchi za mabeberu za EU, kuonyesha dalili za kutukatia misaada baada ya wao kubaini kuwa nchi yetu imeuvuruga mno mfumo wa kidemokrasia na uchaguzi mkuu uliopita na inakiuka mno haki za binadamu?
Tunapaswa tujisahihishe, wazungu wanapotukosoa tukae chini na kuangalia ni wapi tulipokosea na tujirekebishe, badala ya hii hali tunayoendelea nayo ya kujiona sisi tuko 100 percent perfect na kila wazungu wanapotukosoa tuwaite majina mabaya kuwa wao ni mabeberu, lakini wanapokaa kimya kama China, tunawasifu na kuwaita ni washirika na wahisani wetu wazuri wa maendeleo.