Hivi ni kwanini Mwanasheria Mkuu wa serikali hachukuliwi hatua kwa kuonyesha kuipinga hukumu ya Mahakama kuu?

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,483
30,155
Mahakama kuu imefanya uamuzi wa kihistoria, ambao umeungwa mkono na mamilioni ya wapenda demokrasia nchini ya kubatilisha wakurugenzi ambao pia ni.makada wa Chama cha Mapinduzi, kuwa wasimamizi wa uchaguzi nchini

Kilichonishangaza ni kusikia Mwanasheria Mkuu wa serikali, Dr Adeladus Kilangi, kuwa na nia ya kutaka kukata rufaa ya kupinga uamuzi huo wa mahakama kuu wa kutengua uamuzi wa wakurugenzi, kuendelea kuwa wasimamizi wa chaguzi hizo!

Sasa ninachojiuliza ni sababu zipi zinazomfanya Mwanasheria Mkuu wa serikali akate rufaa, wakati yeye kama Mwanasheria Mkuu, akitambua kuwa chombo cha mahakama ndicho chombo pekee nchini, chenye wajibu wa kuzitafsiri sheria na itakapoona baadhi ya sheria zinakiuka haki ya msingi ya kibinadamu au zinakiuka haki ya msingi ya sheria mama, ambayo ni Katiba ya nchi, chombo hicho kina wajibu wa kuzibatilisha??

Nadhani ni wakati muafaka kwa sasa kwa chombo hicho cha mahakama kuwa wakali zaidi kwa watawala wetu ambao wana kiburi cha hali ya juu na hawataki kutii maamuzi ya mahakama hiyo, ingawa maamuzi hayo yanakuwa yanafurahiwa na mamilioni ya wapenda demokrasia nchini na wanaharakati wa nchi hii
 
Nani atamagusa wakati ametumwa na aliye juu ya sheria zote nchini? Na kwa kuwa amewanunulia magari majaji wa mahakama na amewapatia magari bila shaka rufaa itashinda
 
Mahakama kuu imefanya uamuzi wa kihistoria, ambao umeungwa mkono na mamilioni ya wapenda demokrasia nchini ya kubatilisha wakurugenzi ambao pia ni.makada wa Chama cha Mapinduzi, kuwa wasimamizi wa uchaguzi nchini

Kilichonishangaza ni kusikia Mwanasheria Mkuu wa serikali, Dr Adeladus Kilangi, kuwa na nia ya kutaka kukata rufaa ya kupinga uamuzi huo wa mahakama kuu wa kutengua uamuzi wa wakurugenzi, kuendelea kuwa wasimamizi wa chaguzi hizo

Sasa ninachojiuliza ni sababu zipi zinazomfanya Mwanasheria Mkuu wa serikali akate rufaa, wakati yeye kama Mwanasheria Mkuu, akitambua kuwa chombo cha mahakama ndicho chombo pekee nchini, chenye wajibu wa kuzitafsiri sheria na itakapoona baadhi ya sheria zinakiuka haki ya msingi ya kibinadamu au zinakiuka haki ya msingi ya sheria mama, ambayo ni Katiba ya nchi, chombo hicho kina wajibu wa kuzibatilisha

Nadhani ni wakati muafaka kwa sasa kwa chombo hicho cha mahakama kuwa wakali zaidi kwa watawala wetu ambao wana kiburi cha hali ya juu na hawataki kutii maamuzi ya mahakama hiyo, ingawa maamuzi hayo yanakuwa yanafurahiwa na mamilioni ya wapenda demokrasia nchini na wanaharakati wa nchi hii
Achukiliwe hatua haraka iwezekanavyo..nipo tayari kuchangia
 
Nashindwa kuelewa Serikali inakata Rufaa kwa ajili ya nani? Mahakama imeona wananchi wananyimwa haki ya maamuzi yao na Wakurugenzi kwa kukiuka katiba,kwa hiyo serikali inataka wananchi waendelee kuteswa na Wakurugenzi?
 
Mtumwa Hauwawi Ndio Huyo Mwanasheria Ameagizwa Tu
Ni lazima atumie yaaluma yake ya sheria kwa weledi, kama anataka kulinda hadhi yake

Tunajua kuwa kitendo cha Mahakama kuu kutamka kuwa siyo halali kwa wateule wa Rais, ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM, kimemuudhi sana kiasi cha kuamrisha ni lazima ikatwe rufaa!
 
Nashindwa kuelewa Serikali inakata Rufaa kwa ajili ya nani? Mahakama imeona wananchi wananyimwa haki ya maamuzi yao na Wakurugenzi kwa kukiuka katiba,kwa hiyo serikali inataka wananchi waendelee kuteswa na Wakurugenzi?
Absolutely true

Serikali hii inapenda wananchi wake waendelee kuumia kwa hawa wakurugenzi wanaosimamia uchaguzi kutwambia kuwa eti CCM imepata ushindi wa kishindo wa asilimia 100!
 
Mahakama kuu imefanya uamuzi wa kihistoria, ambao umeungwa mkono na mamilioni ya wapenda demokrasia nchini ya kubatilisha wakurugenzi ambao pia ni.makada wa Chama cha Mapinduzi, kuwa wasimamizi wa uchaguzi nchini

Kilichonishangaza ni kusikia Mwanasheria Mkuu wa serikali, Dr Adeladus Kilangi, kuwa na nia ya kutaka kukata rufaa ya kupinga uamuzi huo wa mahakama kuu wa kutengua uamuzi wa wakurugenzi, kuendelea kuwa wasimamizi wa chaguzi hizo!

Sasa ninachojiuliza ni sababu zipi zinazomfanya Mwanasheria Mkuu wa serikali akate rufaa, wakati yeye kama Mwanasheria Mkuu, akitambua kuwa chombo cha mahakama ndicho chombo pekee nchini, chenye wajibu wa kuzitafsiri sheria na itakapoona baadhi ya sheria zinakiuka haki ya msingi ya kibinadamu au zinakiuka haki ya msingi ya sheria mama, ambayo ni Katiba ya nchi, chombo hicho kina wajibu wa kuzibatilisha??

Nadhani ni wakati muafaka kwa sasa kwa chombo hicho cha mahakama kuwa wakali zaidi kwa watawala wetu ambao wana kiburi cha hali ya juu na hawataki kutii maamuzi ya mahakama hiyo, ingawa maamuzi hayo yanakuwa yanafurahiwa na mamilioni ya wapenda demokrasia nchini na wanaharakati wa nchi hii
[/QUOTE
We jamaa rufaa ni haki ya msingi
 
Hata chadema hupinga hukumu ambazo zinawatia hatiani mahakamani. Kosa liko wapi kwa mwanasheria wa serikali kupinga hiyo hukumu mahakamani??
 
Mahakama kuu imefanya uamuzi wa kihistoria, ambao umeungwa mkono na mamilioni ya wapenda demokrasia nchini ya kubatilisha wakurugenzi ambao pia ni.makada wa Chama cha Mapinduzi, kuwa wasimamizi wa uchaguzi nchini

Kilichonishangaza ni kusikia Mwanasheria Mkuu wa serikali, Dr Adeladus Kilangi, kuwa na nia ya kutaka kukata rufaa ya kupinga uamuzi huo wa mahakama kuu wa kutengua uamuzi wa wakurugenzi, kuendelea kuwa wasimamizi wa chaguzi hizo!

Sasa ninachojiuliza ni sababu zipi zinazomfanya Mwanasheria Mkuu wa serikali akate rufaa, wakati yeye kama Mwanasheria Mkuu, akitambua kuwa chombo cha mahakama ndicho chombo pekee nchini, chenye wajibu wa kuzitafsiri sheria na itakapoona baadhi ya sheria zinakiuka haki ya msingi ya kibinadamu au zinakiuka haki ya msingi ya sheria mama, ambayo ni Katiba ya nchi, chombo hicho kina wajibu wa kuzibatilisha??

Nadhani ni wakati muafaka kwa sasa kwa chombo hicho cha mahakama kuwa wakali zaidi kwa watawala wetu ambao wana kiburi cha hali ya juu na hawataki kutii maamuzi ya mahakama hiyo, ingawa maamuzi hayo yanakuwa yanafurahiwa na mamilioni ya wapenda demokrasia nchini na wanaharakati wa nchi hii
Adeladus Kilangi anajaribu kufuta aibu kwa nini ashindwe kesi na hijana wadogo kama akina Bob Chacha Wangwe. Ukweli anaujua lakini Tumbo Mbele akili Nyuma.
 
Absolutely true

Serikali hii inapenda wananchi wake waendelee kuumia kwa hawa wakurugenzi wanaosimamia uchaguzi kutwambia kuwa eti CCM imepata ushindi wa kishindo wa asilimia 100!

hii ndio inadhihirisha kua hua tunazugwa kwenda kupanga foleni eti tunapiga kura na nashangaaga vyama kushiriki upuuzi huu, na kama itarudishwa tena kwa kukatiwa rufaa nikisikia Siku ya uchaguzi mi naenda shambani kupiga kazi, poleni wadanganyika😂😂
 
Hata chadema hupinga hukumu ambazo zinawatia hatiani mahakamani. Kosa liko wapi kwa mwanasheria wa serikali kupinga hiyo hukumu mahakamani??
Huo uamuzi wa mahakama kuu, umepokewa kwa furaha kubwa na wapenda demokrasia wa nchi hii

Sasa kinachoshangaza ni kwanini Mwanasheria Mkuu wa serikali anaipinga??
 
Hata ukiangalia sakata la kuuawa mwanafunzi wa chuo cha usafirishaji cha NIT, Akwilina Akwiline, chanzo chake ni huyo Mkurugenzi wa CCM Aron Kagurumjuli, kuzuia viapo vya mawakala wa Chadema, wakati keshawapa wenzao wa CCM!

Wakati chama cha Chadema kilipoamua kuandamana ili kuvifuata viapo hivyo ndiyo yakatokea hayo yaliyotokea
 
Huo uamuzi wa mahakama kuu, umepokewa kwa furaha kubwa na wapenda demokrasia wa nchi hii

Sasa kinachoshangaza ni kwanini Mwanasheria Mkuu wa serikali anaipinga??
Kwani ukishtakiwa mahakamakuu ukashindwa kesi ukiwa upande wa serikali hutakiwi kupinga? Wanashangilia ni wachache na wanaopinga kila kitu. Mwacheni mwanasheria apinge hata kama yuko peke yake ili mradi havunji sheria,
 
Back
Top Bottom