Hivi ni kwanini Missions nyingi za Kijasusi za Ulaya na Marekani ni ngumu kujulikana ila za Kiafrika hujulikana mapema sana?

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,544
108,869
Ni kwamba Ulaya na Marekani mipango mingi ya ' Kuwaangamiza ' wale ' Maadui ' tishio wa nchi zao wa ndani au wa nje hufanyika kwa ' Usiri ' mkubwa, uratibu wa Kitaalam zaidi na umakini wa hali ya juu kiasi kwamba hata Kitendo Kikifanyika kuja Kuamini kuwa kimefanya ' Kijasusi ' huwa ni ngumu tofauti na ambavyo kwa nchi za Kiafrika ( ukiziondoa tu Uganda, Rwanda na Tanzania ambazo hazina huu mchezo kwakuwa Wao ni Watu wa Mungu na wanamuogopa sana Mungu ) mipango yao hujulikana kiurahisi na hata Mtoto mdogo.

Hapa huwa kuna udhaifu gani kwa upande wa nchi nyingi za Kiafrika na unadhani ni wapi ambapo nchi nyingi za Ulaya kama Uingereza, Ufaransa na Urusi bila kuisahau na Marekani wanatushindia hasa katika masuala mazima ya Ujasusi / Unjagu hasa katika suala zima la ' Kuwaangamiza ' kama siyo ' Kuwapoteza ' kabisa wale ' Maadui ' wao wa ndani na wa nje?

Karibuni Wajuvi ( Pundits ) wa haya masuala ili kama kawaida Yetu Sisi wengine tuweze Kujifunza mawili matatu kutoka Kwenu.

Nawasilisha.
 
Mkuu jibu mbona lipo kwenye Maelekezo yako ya awali

"Ni kwamba Ulaya na Marekani mipango mingi ya ' Kuwaangamiza ' wale ' Maadui ' tishio wa nchi zao wa ndani au wa nje hufanyika kwa ' Usiri ' mkubwa, uratibu wa Kitaalam zaidi na umakini wa hali ya juu kiasi kwamba hata Kitendo Kikifanyika kuja Kuamini kuwa kimefanya ' Kijasusi ' huwa ni ngumu"
 
Mafunzo, weledi na maslahi pia namna ya kuwapata hao majasusi, kuna wakati kigezo kinakuwa "huyu mtoto wa Fulani" badala ya uwezo wa mtu

Eti Mkuu kuna ukweli wowote ule kwamba Ulaya na Marekani ndiyo kuna ' Majasusi ' na Afrika ' Wapelelezi ' tu pekee?
 
Mafunzo, weledi na maslahi pia namna ya kuwapata hao majasusi, kuna wakati kigezo kinakuwa "huyu mtoto wa Fulani" badala ya uwezo wa mtu
Wahehe wengi kuna wakati walikuwa wanajazana kwenye tasisi yetu ya kijasusi TISS sijui kwa nini?
 
Mkuu jibu mbona lipo kwenye Maelekezo yako ya awali

"Ni kwamba Ulaya na Marekani mipango mingi ya ' Kuwaangamiza ' wale ' Maadui ' tishio wa nchi zao wa ndani au wa nje hufanyika kwa ' Usiri ' mkubwa, uratibu wa Kitaalam zaidi na umakini wa hali ya juu kiasi kwamba hata Kitendo Kikifanyika kuja Kuamini kuwa kimefanya ' Kijasusi ' huwa ni ngumu"

Kuna ukweli wowote ule Mkuu kwamba Afrika kuna Wapelelezi tu ila Ulaya na Marekani ndiko kuna Majasusi?
 
Wahehe wengi kuna wakati walikuwa wanajazana kwenye tasisi yetu ya kijasusi TISS sijui kwa nini?

Mkuu kumbe na Sisi Tanzania tuko vizuri kwani tunao hadi hao Majasusi kabisa. Kuna Mtu alinidanganya kuwa Afrika hatuna Majasusi bali tuna Wapelelezi tu pekee ila baada ya Wewe sasa kunihakikishia katika hili kuwa nasi kumbe tunao Majasusi ngoja nimjibu sasa na nimwambie akome kabisa kutudharau Waafrika kwani hata Sisi tuna uwezo ule ule kama unaopatikana huko Uingereza, Ufaransa, Urusi na hadi Marekani.
 
Mkuu kumbe na Sisi Tanzania tuko vizuri kwani tunao hadi hao Majasusi kabisa. Kuna Mtu alinidanganya kuwa Afrika hatuna Majasusi bali tuna Wapelelezi tu pekee ila baada ya Wewe sasa kunihakikishia katika hili kuwa nasi kumbe tunao Majasusi ngoja nimjibu sasa na nimwambie akome kabisa kutudharau Waafrika kwani hata Sisi tuna uwezo ule ule kama unaopatikana huko Uingereza, Ufaransa, Urusi na hadi Marekani.
Wapelelezi ni wafuatilia infor na kung'amua source la majasusi ni wale wapelelezi ambao wapo full equipped kimafunzo,dhana,na hata uzalendo.HIYO NDO TAFSIRI YANGU MZEE
 
Back
Top Bottom