Hivi ni kwanini hadi hivi sasa Waziri Mwigulu Nchemba na Kamanda Lazaro Mambosasa hawajajiuzulu?

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,480
30,152
Najaribu kujiuliza swali hilo kwa kutafakari sana hivi sababu zipi zinazofanya hao watendaji wakuu hawajajiuzulu hadi hivi sasa nafssi zao licha ya Wizara ya Mambo ya Ndani kuwa ndiyo Wizara inayonyooshewa vidole na Umma wa watanzania kwa hivi sasa kutokana na vitendo vya kuuawa watu bila watuhumiwa kukamatwa, vitendo vya utekaji wa watu bila hao watu kuonekana tena, vitendo vya kuokota miili ya watu kwenye viroba, ni baadhi ya visa ambavyo vinatokea nchi hii bila Watuhumiwa kufikishwa mahakamani.

Hebu tujikumbushe nyuma kidogo mnamo mwaka 1977, Rais mstaafu wa awamu ya pili Ali Hassan Mwinyi alijiuzulu uwazili wake wa mambo ya ndani kutokana na mauaji yaliyotokea kule Shinyanga.

Ninajiuliza mbona Rais mstaafu alijiuzulu uwaziri kwa tukio moja tu la mauaji, mbona hivi sasa matukio ni mengi sana, hususani yanayohusu kuonewa kwa chama kikuu cha upinzani cha Chadema, mbona watendaji hao wakuu wa Mambo ya ndani wamegoma kabisa kujiuzulu??

Najiuliza swali lingine la pili, ni kwanini basi watendaji hao wakuu baada ya kugoma kuwajibika kwa kujiuzulu, Rais naye anasita kuwatumbua??

Ifahamike pia kuwa haya mauaji yenye mlengo wa kisiasa hapa nchini yeshapata coverage kubwa kwenye vyombo mbalimbali vikubwa vya nje ya nchi

Kwa jinsi tunavyomfahamu Rais wetu ambavyo hana mchezo hata kidogo kwa kutengua wateule wake hata kwa vijikosa vidogo, iweje kwa Jeshi la Polisi ukiwa wajibu wao no 1 ni kuwalinda raia na Mali zao, iweje sasa kwa hawa watendaji wakuu wa Jeshi la Polisi, wanaonekana wazi kuwa wajibu huo wa kuwalinda raia na mali zao "wamefeli" kabisa, ni kwanini Rais anaonekana anashikwa na "kigugumizi" kuwafukuza kazi??

Iwapo yeye Rais aliweza kutengua mara moja uteuzi wa Waziri wa Habari wa wakati ule, Nape Nnauye kwa "kosa" la kuunda Tume ya kuchunguza tukio ls Mkuu wa Mkoa wa Dar, Paul Makonda kwa kuvamia studio za Clouds akiwa na askari wenye silaha za moto, tunashangaa hii huruma ya wakati huu ya "kulinda" ajira za watu hao wawili inatoka wapi??

Tungependa Rais wetu achukue hatua za haraka za kuwafukuza kazi Waziri wa mambo ya ndani, Mwigulu Nchemba na IGP Simon Sirro ili sisi wananchi turejeshe Imani na serilali yake.

Mungu ibariki Tanzsnia
 
umeandika vizuri, kumbuka kila binadamu hukosea
Ndiyo kila binadamu hukosea, ndiyo sababu tunawaambia hao watendaji wawili wakubwa kabisa wanapaswa kujiudhuru kwa mama ya kuwajibika kutokana na "madudu" yanayofanywa na watendaji wengine walio chini yao,hiyo ndiyo maana ya kuwajibika.

Kitendo cha kugoma kujiuzulu kinaonyesha aina fulani ya kiburi kwa aliyewateua, na hivyo tunaomba Rais ambaye amewateua watu hao awafujuze kazi mara moja maana kilio mtanzania anashinikiza hao wawili waondoke kwenye nafasi zao
 
.....
.....asante Mkuu ila kuna uzi upo live hapo juu karibu kama GT
Asante Mkuu, ila naomba mods wasiunganishe hii thread ili ijitegemee, kwa kuwa inahusu mwito wa watanzania walio wengi wanaotaka hao watendaji wakuu wa wizara ya ndani kuachia ngazi
 
Unaachaje limshahara,mamirupurupu,limgari,masaluti,makutetemekewa,lijiofisi na lijumba likubwa huku ukizingatia bado ni kijana,ataenda ajiriwa na nani? watoto nao baado wadogo!! Kufikia huo utamu watu wametaabika sn,kusema uongo,kupika majungu,kujipendekeza,pengine waganga...Hajiuzulu mtu hapa hata kwanini!
 
Hakuna sababu ya Msingi ya kujiuzulu!

Kuna Siku mtakuja na thread za kuwataka Mababa wajiuzulu kwa kuwa Watoto wao wamepata Mimba!
 
Mwingulu njaa tu.ametanguliza tumbo na yule mke wa GEORGE ndio kazaa naye.alimpa kesi ya kuuwa GEORGE hadi leo yuko magereza na WAZIRI anaendelea kutanua na mke wa mtu kama sisonje



Swissme
Sasa kama hataki kujiuzulu ni kwanini basi Bosi wake hamfukuzi kazi??

Tunajua Rais wetu alivyo hana mchezo kwa wasaidizi wake, inakuwaje "anawagwaya" hao kuwafukuza kazi, wakati wameonyesha kuwa nafasi hizo aliziwapa wameshindwa kuzimudu??
 
Mkuu tatizo ni moja tu,

Hakuna passion kutoka moyoni ya uongozi ya watu uliowataja hapo juu,

Wapo hapo walipo kama mimi na wewe tulivyo na kazi fulani,

Yaani wanategemea mishahara na kila kitu katika huo uwaziri

Halafu kaa ukijua hiki ninkizazi cha panya baba mwizi mama mwizi na watoto wezi

Hayo matukio yote yanafanyika makusudi na sio kwa bahati mbaya kama unavyohisi

Nchi hii ili tufike mbali lazima tuwe na mageuzi ya kimfumo
 
Mkuu tatizo ni moja tu,

Hakuna passion kutoka moyoni ya uongozi ya watu uliowataja hapo juu,

Wapo hapo walipo kama mimi na wewe tulivyo na kazi fulani,

Yaani wanategemea mishahara na kila kitu katika huo uwaziri

Halafu kaa ukijua hiki ninkizazi cha panya baba mwizi mama mwizi na watoto wezi

Hayo matukio yote yanafanyika makusudi na sio kwa bahati mbaya kama unavyohisi

Nchi hii ili tufike mbali lazima tuwe na mageuzi ya kimfumo
Sasa ndiyo tunasema kuwa ni lazima Rais awafukuze kazi, na kama hatawafukuza kazi basi naye "atahusishwa" na matukio haya maovu yanayotokea.
 
Kamanda Mambosasa must go.........

Kwa kuwa hata kama mimi ndiye ningekuwa Kamanda wa Polisi wa Dar, nisingeendesha ile operation ya kuzima yale maandamano ya Chadema kwa staili ile ya siku ile.

Kwa vile na kuwa na magari yale ya washawasha nisingelazimika kuamrisha wale askari wapige risasi za moto ovyo kiasi kile siku ile, kwa kuwa zile gari za washawasha tu zingetosha kuzima maandamano.

Kwa kuwa hata mimi najua kuwa kuwa askari huwa anatumia risasi za moto kama "last resort" baada ya juhudi zote za kuzima maandamano hayo imeshindikana.

Sasa swali ninalojiuliza hivi ni kweli askari yule alilazimika kutumia zile risasi za moto hadi kusababisha kifo cha yule binti asiye na hatia na wala hakuwa sehemu ya yale maandamano??
 
Muwe mnaangalia makosa ya wote nadhan aliyehamasisha na kuongoza maandamano nae ajiuzulu. Kuwajibika ni kuwajibika tu,kila maandamano wanamwaga damu na kuziachia familia majonzi,ukiwa,upweke,ujane,etc

Wimbo wa fulani ajiuzulu uimbwe kwa pande zote bila ubaguzi wala upendeleo
 
Sasa ndiyo tunasema kuwa ni lazima Rais awafukuze kazi, na kama hatawafukuza kazi basi naye "atahusishwa" na matukio haya maovu yanayotokea.
Hivi mkuu unataka nini hasa?

Huu mjadala nafikiri unajua kabisa tatizo liko wapi na bado umekomaa wafukuzwe
 
Muwe mnaangalia makosa ya wote nadhan aliyehamasisha na kuongoza maandamano nae ajiuzulu. Kuwajibika ni kuwajibika tu,kila maandamano wanamwaga damu na kuziachia familia majonzi,ukiwa,upweke,ujane,etc

Wimbo wa fulani ajiuzulu uimbwe kwa pande zote bila ubaguzi wala upendeleo
Wewe unajua ni kwanini wanachadema.waliandamana??

Ni kwa sababu ya upendekeo wa wazi wa "kada" wenu Mkurugenzi kwa kutotoa viapo vya mawakala hadi siku ile moja kabla ya uchaguzi, wakati wapinzani wao wakuu wa CCM keshawapa "kilaini" wiki moja kabla!

Hivi hata wewe ungekuwa ndiye Mbowe usingehamasisha Yale maandamano kweli??
 
Back
Top Bottom