Hivi ni kipi kilipaswa kujengwa kwanza, ni kuinua daraja la Jangwani au kujenga Daraja jipya la Salenda hadi Coco beach?

Hizo porojo za kajima tunazifahamu. Ila kabla ya ujenzi huu wa BRT maji yalikuwa hayapandi juu ya daraja. Maji yameanza kupanda juu ya daraja baada ya huu ujenzi kwa kuwa wameyang'anya maji sehemu ya kutulia bahari inapokuwa imejaa.

Kumbuka wakati huu ujenzi unaanza vifusi vyote walivyokuwa wanafukua barabara ya zamani walikuwa wanavileta hapa jangwani wakawa wanasawazisha mpaka wakapa_level na kujenga karakana moja iliyokuwa na mabomba mengi sana pale nje. Ile karakana baadae walikuja kuiondoa lakini damage ilikuwa imeshafanyika kwani lile bonde lilikuwa limesaminywa na kupunguza uwezo wake wa kuhifadhi maji. Ndio maana tangu hapo hili tatizoo limeanza.
Nakushukuru sana! Environmental Impact Assessment nani alifanya? Je, waliruhusiwa na NEMC?
 
Ubalozi wa UK uko wapi?
hakuna daraja linalounganisha Salender na Coco Beach... daraja linaanzia Sea View linakuja sambamba na Salender, linaishia Ubalozi wa UK ambao uko karibu na mataa ya Salender njia panda ya Kinondoni, ambapo ndio Oysterbay inapoanzia. Coco Beach ipo kwenye edge ya Masaki, Oysterbay inapoishia. Kwa hiyo hili daraja litakuwa linachukua traffic ya Kinondoni na Mwenge pia.

hakuna njia ya jangwani inayounganisha Magomeni na jijini D'Salaam kwa sababu Magomeni ipo jijini D'Salaam...

tuuelewe kwanza mji na mabarabara kabla ya kupendekeza na kukosoa madaraja na mafuriko.....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Uliwahi toa maoni yako kabla ya mchakato?,au ndio ile kutafuta sifa jukwaani
Baada ya kuona haya mateso makubwa wanayopata wanabchi kwa kufunga barabara inayounganisha jijini Dar na Magomeni ikijirudia Mara kwa Mara kutokana na mvua kunyesha, nimekuwa nikijiuliza hivi hawa watawala wetu walitumia busara kweli kuamua kujenga daraja la kuunganisha coco beach na selander, badala ya kutoa kipaumbele cha kuliinua daraja la Jangwani?

Imekuwa ni kawaida sana kwa siku za karibuni kila mvua inaponyesha, hata kama ni ndogo, tunaambiwa kuwa barabara ya Morogoro, inayounganisha Magomeni na jijini Dar imefungwa

Hebu tujaribu ku-imagine ni madhara kiasi gani yanayopatikana kiuchumi kila barabara hiyo inapofungwa?

Hebu pia tujaribu ku-imagine ni wakazi wangapi wanapata usumbufu wa kutokwenda kutibiwa kwenye hospitali ya Muhimbili au kwenda waona wapendwa wao waliolazwa katika hospitali hiyo kubwa hapa nchini kutokana na kadhia hiyo?

Lakini kwa kuwa nchi hii hivi sasa tunajua kuwa inaendeshwa kwa "misifa" ya ONE MAN SHOW, kila alitakalo bwana yule ni lazima litekelezwe, bila kwanza kuangalia ni kitu gani cha kutoa kipaumbele kwa muda tulionao

Nina hakika watu maelfu kwa maelfu, wanaathirika sana na hii barabara ya Morogoro ya kipande cha daraja la Jangwani kinachounganisha Magomeni na jijini Dar

Pia soma:

1). Magufuli: Tutajenga flyover Salender Bridge
2). Yaliyojiri Uwekaji wa jiwe la msingi Daraja la Selander
3). Wabunge pingeni na kataeni kujengwa kwa Daraja la Juu ya Bahari kutoka Coco Beach to Agakhan

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hili daraja la jangwani ni mipango tu ya upigaji
Vipi toka lijengwe halijasafishwa ilikua kazi ya kuliondolea mchanga nakuliachia kile kina cha zamani ili maji yapite kwa kasi ileile sio kuwa hawajui nini kinahitajika ila ni kusudi tu za kukomoa ili wapate utaji

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naomba kuuliza kwani njia za kuingilia City Center zipo ngap?

Watanzania tuache Majungu na Umbea tupige kazi yaaani we Umeona jangwani tu.

Usifanye Mawazo yako yakawa ndiyo kipaumbele Cha Jiji kwanini wasijenge Jangwan wamejenga sarenda hayo Ni matumizi Mabaya ya akili.

Tafuta pesa usiipangie Serikalin Nini Cha kufanya we tulia watashughulikia wao.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ubalozi wa UK uko wapi?

Sent using Jamii Forums mobile app

Ubalozi wa UK toka Uhuru ni nyumba ya kwanza mtaa wa Kenyatta Drive kwenye mataa ya Ally Hassan Mwinyi na Kinondoni Road.

Kwenye nyanja za diplomasia nyumbani pia ni ubalozi ndio maana unaweza kukimbilia nyumbani kwa balozi nyakati za uchaguzi wa vi third world dictatorships vyetu ( remember comrade Morgan Tsvangirai, RIP).

Anyhow, ndipo daraja jipya litakapoishia. Haliendi Coco Beach. Coco Beach iko Masaki. Hili daraja halitoki Sea View kwenda Masaki, I mean, hatujengi Kun Shan Grand Bridge la China!

Now, the pressing question is litapunguza vipi foleni ya kutoka mjini kama magari yake hayapitilizi, yanakuja kumwagwa mataa ya Ubalozi wa UK, hapo Ally Mwinyi na Kinondoni Road / Stanbic Bank?
 
Baada ya kuona haya mateso makubwa wanayopata wanabchi kwa kufunga barabara inayounganisha jijini Dar na Magomeni ikijirudia Mara kwa Mara kutokana na mvua kunyesha, nimekuwa nikijiuliza hivi hawa watawala wetu walitumia busara kweli kuamua kujenga daraja la kuunganisha Coco beach na Salenda, badala ya kutoa kipaumbele cha kuliinua daraja la Jangwani?

Imekuwa ni kawaida sana kwa siku za karibuni kila mvua inaponyesha, hata kama ni ndogo, tunaambiwa kuwa barabara ya Morogoro, inayounganisha Magomeni na jijini Dar imefungwa

Hebu tujaribu ku-imagine ni madhara kiasi gani yanayopatikana kiuchumi kila barabara hiyo inapofungwa?

Hebu pia tujaribu ku-imagine ni wakazi wangapi wanapata usumbufu wa kutokwenda kutibiwa kwenye hospitali ya Muhimbili au kwenda waona wapendwa wao waliolazwa katika hospitali hiyo kubwa hapa nchini kutokana na kadhia hiyo?

Lakini kwa kuwa nchi hii hivi sasa tunajua kuwa inaendeshwa kwa "misifa" ya ONE MAN SHOW, kila alitakalo bwana yule ni lazima litekelezwe, bila kwanza kuangalia ni kitu gani cha kutoa kipaumbele kwa muda tulionao

Nina hakika watu maelfu kwa maelfu wanaathirika sana na hii barabara ya Morogoro ya kipande cha daraja la Jangwani kinachounganisha Magomeni na jijini Dar

Pia soma:
1). Magufuli: Tutajenga flyover Salender Bridge
2). Yaliyojiri Uwekaji wa jiwe la msingi Daraja la Selander
3). Wabunge pingeni na kataeni kujengwa kwa Daraja la Juu ya Bahari kutoka Coco Beach to Agakhan

Ahsante sana kiongozi,Naomba mimi mchango wangu ujikite kwenye chanzo.

Mto Msimbazi ni miongoni mwa mito ya jiji la Dar es Salaam,mto huu chanzo chake ni kwenye vilima vya pugu na mdomo wa mto huu ndio pale daraja la Selander.

Kulingana na kukua kwa shughuli za binadamu tumeshuhudia uharibifu mkubwa sana wa mazingira kwenye vyanzo vya mto huu kule Pugu ,uharibifu huu unafanya mvua zikinyesha zilete mchanga ambao unaishia Jangwani,hivyo ni muhimu sana kwa serikali na washika dau wengine kupanda miti na kutunza mazingira ya mto huu kwanza kwa sababu madhara ya mchanga huu ni kukua kwa kiwango cha mafuriko hii ikimaanisha Kariakoo pia hatarini kupata mafuriko miaka inavyozid kwenda mbele.
 
Nilisema ingekuwa busara hata kama kungejengwa daraja lingine Hananasif mpaka Upanga/ Muhimbili.

Na bado, sasa hivi wanataka kujenga daraja kwenda Zanzibar!
Hili jambo nimekuwa nikifikiria toka siku nyingi sana, hii stratergically ingepunguza msongomano na pia kufupisha safari.
 
Back
Top Bottom